< 2 Samweli 24 >

1 Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
Men HERRENS vrede blussede atter op mod Israel, saa at han æggede David mod dem og sagde: »Gaa hen og hold Mandtal over Israel og Juda!«
2 Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
Kongen sagde da til Joab og Hærførerne, der var hos ham: »Drag rundt i alle Israels Stammer fra Dan til Be'ersjeba og hold Mønstring over Folket, for at jeg kan faa Tallet paa det at vide!«
3 Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
Men Joab svarede Kongen: »Maatte HERREN din Gud forøge Folket hundredfold, og maatte min Herre Kongen selv opleve det — men hvorfor har min Herre Kongen sat sig sligt for?«
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
Men Joab og Hærførerne maatte bøje sig for Kongens Ord. Joab og Hærførerne forlod derfor Kongen for at holde Mønstring over Israels Folk.
5 Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
De gik over Jordan og begyndte ved Aroer og Byen, der ligger midt i Dalen; drog ad Gad til og i Retning af Ja'zer;
6 Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
saa kom de til Gilead og til Hetiternes Land hen imod Kadesj, derpaa til Dan, og fra Dan vendte de sig hen mod Zidon;
7 Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
saa kom de til Fæstningen Tyrus og alle Hivviternes og Kana'anæernes Byer, hvorfra de gik til Be'ersjeba i det judæiske Sydland.
8 Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
Efter at de var draget hele Landet rundt i ni Maaneder og tyve Dage, kom de tilbage til Jerusalem.
9 Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
Joab opgav derpaa Kongen Tallet, der var fundet ved Folketællingen, og Israel talte 800 000 kraftige, vaabenføre Mænd, Juda 500 000 Mænd.
10 Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
Men efter at David havde holdt Mandtal over Folket, slog Samvittigheden ham, og han sagde til HERREN: »Jeg har syndet svarlig i, hvad jeg har gjort! Men tilgiv nu, HERRE, din Tjeners Brøde, thi jeg har handlet som en stor Daare!«
11 Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
Da David stod op om Morgenen kom HERRENS Ord til Profeten Gad, Davids Seer, saaledes:
12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
»Gaa hen og sig til David: Saa siger HERREN; Jeg forelægger dig tre Ting; vælg selv, hvilken jeg skal lade times dig!«
13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
Gad kom da til David og kundgjorde ham det og sagde: »Skal der komme tre Hungersnødsaar over dig i dit Land, eller vil du i tre Maaneder jages paa Flugt, forfulgt af din Fjende, eller skal der komme tre Dages Pest i dit Land? Overvej nu, hvad jeg skal svare ham, der har sendt mig!«
14 Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
David svarede Gad: »Jeg er i saare stor Vaande — lad os saa falde i HERRENS Haand, thi hans Barmhjertighed er stor; i Menneskehaand vil jeg ikke falde!«
15 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
Saa valgte David da Pesten. Ved Hvedehøstens Tid begyndte Soten at ramme Folket; og der døde 70 000 Mand af Folket fra Dan til Be'ersjeba.
16 Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
Da Engelen udrakte sin Haand mod Jerusalem for at ødelægge det, angrede HERREN det onde, og han sagde til Engelen, som ødelagde Folket »Nu er det nok, drag din Haand tilbage!« HERRENS Engel var da ved Jebusiten Aravnas Tærskeplads.
17 Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
Men da David saa Engelen, som slog Folket, sagde han til HERREN: »Det er mig, der har syndet, mig, der har begaaet Brøden; men Faarene der, hvad har de gjort? Lad din Haand dog ramme mig og mit Fædrenehus!«
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
Samme Dag kom Gad til David og sagde: »Gaa op og rejs HERREN et Alter paa Jebusiten Aravnas Tærskeplads!«
19 Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
Og David gik derop efter Gads Ord, saaledes som HERREN havde paabudt.
20 Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
Da Aravna, der var ved at tærske Hvede, saa ned og fik Øje paa Kongen og hans Folk, som kom hen imod ham, gik han ud og kastede sig paa sit Ansigt til Jorden for ham;
21 Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
og Aravna sagde: »Hvorfor kommer min Herre Kongen til sin Træl?« David svarede: »For at købe Tærskepladsen af dig og bygge HERREN et Alter, at Folket maa blive friet fra Plagen!«
22 Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
Da sagde Aravna til David: »Min Herre Kongen tage den og ofre, hvad ham tykkes ret! Her er Okserne til Brændoffer og Tærskeslæderne og Oksernes Stavtøj til Brændsel!
23 Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
Min Herre Kongens Træl giver Kongen det hele!« Og Aravna sagde til Kongen: »Maatte HERREN din Gud have Behag i dig!«
24 Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
Men Kongen svarede Aravna: »Nej, jeg vil købe det af dig for dets fulde Værdi; jeg vil ikke bringe HERREN min Gud Brændofre, som intet koster mig!« Saa købte David Tærskepladsen og Okserne for halvtredsindstyve Sølvsekel;
25 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.
og David byggede HERREN et Alter der og ofrede Brændofre og Takofre. Da forbarmede HERREN sig over Landet, og Israel blev friet fra Plagen.

< 2 Samweli 24 >