< 2 Samweli 24 >

1 Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
Tedy opět prchlivost Hospodinova popudila se proti Izraelovi; nebo byl ponukl satan Davida na ně, řka: Jdi, sečti lid Izraelský a Judský.
2 Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
Protož řekl král Joábovi, hejtmanu vojska svého: Projdi i hned všecka pokolení Izraelská od Dan až k Bersabé, a sečtěte lid, abych věděl počet jeho.
3 Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
Ale Joáb řekl králi: Přidejž Hospodin Bůh tvůj k lidu, jakž ho koli mnoho, stokrát více, a to aby oči pána mého krále viděly. Ale proč pán můj král jest toho tak žádostiv?
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
A však přemohla řeč králova Joába i knížata vojska. Protož vyšel Joáb a knížata vojska od tváři královy, aby sečtli lid Izraelský.
5 Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
A přepravivše se přes Jordán, položili se při Aroer po pravé straně města, kteréž jest u prostřed potoka Gád, a při Jazer.
6 Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
Potom přišli do Galád a do země dolejší nové, odkudž šli do Dan Jáhan a do okolí Sidonského.
7 Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
Přišli také ku pevnosti Týru, a ke všem městům Hevejských a Kananejských; odkudž šli na poledne země Judské do Bersabé.
8 Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
A když schodili všecku zemi, přišli po přeběhnutí devíti měsíců a dvadcíti dní do Jeruzaléma.
9 Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
I dal Joáb počet sečteného lidu králi. Bylo pak lidu Izraelského osmkrát sto tisíc mužů silných, kteříž mohli vytrhnouti meč k bitvě. Mužů také Judských pětkrát sto tisíc.
10 Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
Potom padlo to těžce na srdce Davidovi, když již sečtl lid. I řekl David Hospodinu: Zhřešilť jsem těžce, že jsem to učinil, ale nyní, ó Hospodine, odejmi, prosím, nepravost služebníka svého, nebť jsem velmi bláznivě učinil.
11 Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
Když pak vstal David ráno, stalo se slovo Hospodinovo k Gádovi proroku, vidoucímu Davidovu, řkoucí:
12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
Jdi a rci Davidovi: Toto praví Hospodin: Trojíť věci podávám, vyvol sobě jednu z nich, kteroužť bych učinil.
13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
Protož přišed Gád k Davidovi, oznámil mu to, a řekl jemu: Chceš-li, aby přišel na tebe hlad za sedm let v zemi tvé? čili abys za tři měsíce utíkal před nepřátely svými, a oni aby tě honili? čili aby za tři dni byl mor v zemi tvé? Pomysliž spěšně, a viz, jakou mám odpověd dáti tomu, kterýž mne poslal.
14 Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
I řekl David k Gádovi: Úzkostmi sevřín jsem náramně; nechať, prosím, upadneme v ruku Hospodinovu, neboť jsou mnohá slitování jeho, jediné ať v ruce lidské neupadám.
15 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
A tak uvedl Hospodin mor na Izraele od jitra až do času uloženého, a zemřelo jich z lidu od Dan až do Bersabé sedmdesáte tisíc mužů.
16 Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
A když vztáhl anděl ruku svou na Jeruzalém, aby hubil jej, litoval Hospodin toho zlého, a řekl andělu, kterýž hubil lid: Dostiť jest, již přestaň. Anděl pak Hospodinův byl u humna Aravny Jebuzejského.
17 Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
I mluvil David Hospodinu, když uzřel anděla, an bije lid, a řekl: Aj, já jsem zhřešil, a já jsem neprávě učinil, ale tito, jsouce jako ovce, co učinili? Nechť jest, prosím, ruka tvá proti mně a proti domu otce mého.
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
Potom navrátiv se Gád k Davidovi v ten den, řekl jemu: Vstup a vzdělej Hospodinu oltář na humně Aravny Jebuzejského.
19 Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
I šel David vedlé řeči Gádovy, jakož byl přikázal Hospodin.
20 Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
A vyhlédaje Aravna, uzřel krále s služebníky jeho, an jdou k němu; protož vyšed Aravna, poklonil se králi tváří svou až k zemi.
21 Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
I řekl Aravna: Proč přišel pán můj král k služebníku svému? Odpověděl David: Abych koupil od tebe humno toto, na němž bych vzdělal oltář Hospodinu, aby přestala rána tato v lidu.
22 Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
Opět řekl Aravna Davidovi: Nechť vezme a obětuje pán můj král, což se mu za dobré vidí. Aj, teď volové k oběti zápalné, a smyky vozové i přípravy volů na drva.
23 Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
Všecky ty věci dával králík Aravna králi. Řekl ještě Aravna králi: Hospodin Bůh tvůj zalibiž tě sobě.
24 Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
Řekl pak král Aravnovi: Nikoli, ale raději koupím od tebe, a zaplatím, aniž budu obětovati Hospodinu Bohu svému oběti zápalné darem dané. A tak koupil David humno a voly za padesáte lotů stříbra.
25 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.
A vzdělav tu David oltář Hospodinu, obětoval oběti zápalné a pokojné. I byl milostiv Hospodin zemi, a přestala zhouba v Izraeli.

< 2 Samweli 24 >