< 2 Samweli 23 >
1 Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
И сия словеса Давидова последняя. Верен Давид сын Иессеов, и верен муж, егоже возстави Господь в христа Бога Иаковля, и благолепны псалмы Израилевы.
2 “Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
И Дух Господень глагола во мне, и слово Его на языце моем.
3 Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
Глаголет Бог Израилев: мне глагола хранитель Израилев притчу: рех в человецех: како удержите страх Божий?
4 yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
И во свете Божии утреннем, и возсия солнце заутра, не прейде от сияния, и яко от дождя злачна от земли.
5 “Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
Не тако бо дом мой с Крепким: завет бо вечен положи ми, готов во всяком времени сохранен: яко все спасение мое и все хотение во Господе, яко не имать прозябнути беззаконный.
6 Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
Якоже терние извержено вси сии, яко не возмутся рукою,
7 Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
и муж не потрудится в них: и множество железа, и древо копийное, и огнем сожжет, и попалятся в срамоту свою.
8 Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
Сия имена сильных Давидовых: Иевосфей Хананеанин князь третияго есть: адинон асоней, сей обнажи мечь свой на осмь сот воинов (и победи) единою.
9 Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
И по нем Елеазар, сын отца брата его, в триех сильных братиях, сей бе со Давидом (во сирране) внегда поносити ему во иноплеменницех: и иноплеменницы собрашася тамо на брань,
10 lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
и изыдоша мужие Израилевы противу лица их, и той воста и убиваше иноплеменники, дондеже утрудися рука его и прильпе рука его к мечу: и сотвори Господь спасение велико в той день: и людие обратишася вслед его токмо совлачати.
11 Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
И по нем Самаиа сын Асы, Арухейский: и собрашася иноплеменницы во Фирию: и бе тамо часть села исполнь лящи: и людие бежаша от лица иноплеменнича:
12 Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
и ста аки столп посреде части, и исхити ю, и порази иноплеменники: и сотвори Господь спасение велико.
13 Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
И снидоша три князи от тридесятих, и приидоша в касон к Давиду в вертеп Одоллам: и чинове иноплеменник ополчишася во юдоли Рафаинстей.
14 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
И Давид тогда бе во обдержании, и стан иноплеменническ бе тогда в Вифлееме.
15 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
И возжада Давид и рече: кто напоит мя водою из рова, иже в Вифлееме при вратех? Стан же бе тогда иноплеменничь в Вифлееме.
16 Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
И расторгоша трие сильнии ополчение иноплеменничо, и почерпоша воды из рова Вифлеемскаго, иже при вратех: и взяша, и приидоша ко Давиду, и не восхоте пити ея: и возлия ю Господу
17 Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
и рече: милостив мне, Господи, еже сотворити сие, кровь ли мужей пошедших в душах своих пити имам? И не восхоте пити ея. Сия сотвориша трие сильнии.
18 Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
И Авесса брат Иоавль сын Саруин, сей бе князь в триех, и сей воздвиже копие свое на триста язвеных, и тому имя есть в триех.
19 Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
От триех оных славный, и бысть им князь, и даже до триех не прииде.
20 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
И Ванеа сын Иодаев, муж сей премног в делех, от Кавасаила, и сей уби два сына Ариила Моавскаго: и той сниде, и уби льва посреде рова в день снежен:
21 Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
и той порази мужа Египтянина, мужа красна, в руце же Египтянина копие яко древо лествицы корабленыя: и сниде к нему со палицею, и исторже копие из руку Египтянина, и уби его копием его:
22 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
сия сотвори Ванеа сын Иодаев, и тому имя в триех сильных,
23 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
от триех славный, и ко трием не прииде: и постави его Давид над таинники своими.
24 Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
И сия имена сильных Давида царя: Асаил брат Иоавль, сей в тридесятих: Елеанан сын отца брата его от Вифлеема:
25 Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
Семоф Ародиин:
26 Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
Хеллис Келофийский: Ира сын Еккиса Фекоитскаго:
27 Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
Авиезер Анафофитский: Савухей иже от Асофиты:
28 Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
Еллон Алонитский: моей Нетофафитянин:
29 Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
Ели сын Ваань, иже от Нетофафит: Еффи сын Ривань от Гаваона сынов Вениаминих:
30 Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
Ванеас Фарафонитский: Урий от Наалгеа:
31 Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
Ариил сын Аравофитянина: Заор Варсамитский:
32 Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
Елеаса сын Салавонитский: Васей гонитский:
33 mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
Ионафан сын Самана Ароритскаго: Ахиан сын Арати Арафурскаго:
34 Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
Елифалаф сын Маахиавль: Елиав сын Ахитофела Гелонитскаго:
35 Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
Асараи Кармилский: Урем сын Асви:
36 Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
и Гала сын Нафанов: и Ваан сын Агарин:
37 Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
Елли Амманитский: Гелорей Вирофийский, носяй оружие Иоава сына Саруина:
38 Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
Ирас Еффирский: Гарев Иерфейский: и Уриа Гефейский.
39 na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.
Всех тридесять и седмь.