< 2 Samweli 23 >

1 Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
Mais voici les dernières paroles de David. David, fils d’Isaï, a parlé; l’homme institué le christ du Dieu de Jacob, l’excellent psalmiste d’Israël, a dit:
2 “Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
L’Esprit du Seigneur s’est fait entendre par moi, et sa parole par ma langue.
3 Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
Le Dieu d’Israël m’a dit: le Fort d’Israël a parlé: le dominateur des hommes, le juste dominateur dans la crainte de Dieu sera
4 yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
Comme la lumière de l’aurore, qui, au soleil levant, le matin, brille sans nuages, et comme l’herbe qui germe de la terre par les pluies.
5 “Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
Et ma maison n’était pas si grande devant Dieu, pour qu’il fit avec moi un pacte éternel, ferme en toutes choses et assuré; car ce pacte est tout mon salut et toute ma volonté; et rien n’en provient qui ne porte ses fruits.
6 Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
Mais les prévaricateurs seront extirpés tous comme des épines que l’on n’arrache pas avec les mains.
7 Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
Et si quelqu’un veut les toucher, il s’arme de fer, et d’un bois de lance, et brûlées par le feu, elles sont consumées jusqu’à néant.
8 Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
Voici le nom des braves de David. Celui qui était assis dans la chaire, le plus sage, le premier entre les trois; c’est lui qui, comme le petit ver le plus tendre du bois, tua huit cents hommes en une seule fois.
9 Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
Après lui, Éléazar, Ahohite, fils de son oncle paternel, était entre les trois braves qui étaient avec David, lorsqu’ils insultèrent les Philistins, et qu’ils s’assemblèrent en ce lieu pour le combat.
10 lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
Et lorsque les hommes d’Israël eurent monté, lui se présenta, et battit les Philistins, jusqu’à ce que sa main se lassât et demeurât attachée à son glaive; et le Seigneur donna une grande victoire à Israël en ce jour-là, et le peuple, qui avait fui, retourna pour enlever les dépouilles des morts.
11 Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
Et après lui venait Semma, fils d’Agé, d’Arari. Et les Philistins s’assemblèrent au poste; car il y avait là un champ plein de lentilles. Et lorsque le peuple se fut enfui devant les Philistins,
12 Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
Semma se tint au milieu du champ, le défendit et battit les Philistins; et le Seigneur accorda une grande victoire.
13 Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Et déjà auparavant étaient descendus les trois qui étaient les premiers entre les trente, et ils étaient venus au temps de la moisson vers David, dans la caverne d’Odollam; mais le camp des Philistins était placé dans la Vallée des Géants.
14 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
Et David était dans la forteresse; mais l’armée des Philistins était alors à Bethléhem.
15 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
David donc fit un souhait, et dit: Oh! si quelqu’un me donnait à boire de l’eau de la citerne qui est à Bethléhem, près de la porte:
16 Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Les trois braves passèrent donc à travers le camp des Philistins, et puisèrent de l’eau dans la citerne de Bethléhem qui était près de la porte, et l’apportèrent à David; et David n’en voulut pas boire, mais il l’offrit en libations au Seigneur,
17 Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
Disant: Que le Seigneur me soit propice, pour que je ne fasse pas cela: boirai-je le sang de ces hommes qui sont allés la chercher, et le péril de leurs âmes? Il ne voulut donc pas boire. Voilà ce que firent ces trois hommes très vigoureux.
18 Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Abisaï aussi, frère de Joab, fils de Sarvia, était le premier de trois autres: c’est lui qui leva sa lance contre trois cents, qu’il tua: il était renommé parmi ces trois,
19 Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
Et le plus noble d’entre ces trois, et leur chef; mais il n’atteignait pas les premiers.
20 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Ensuite Banaïas de Cabséel, fils de Joïada, homme très vaillant, et aux grands exploits; c’est lui qui tua les deux lions de Moab, et lui qui descendit et tua le lion au milieu de la citerne, dans les jours de la neige.
21 Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
C’est lui qui tua l’Egyptien: homme digne d’être en spectacle et ayant en main une lance; c’est pourquoi, lorsqu’il fut descendu vers lui avec sa verge, il arracha de force la lance de la main de l’Egyptien, et le tua de sa lance.
22 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Voilà ce que fit Banaïas, fils de Joïada.
23 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Et il était renommé entre les trois vaillants les plus nobles entre les trente; cependant il n’atteignait pas les trois premiers; et David le fit son conseiller intime.
24 Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
Asaël, frère de Joab, était entre les trente; Eléhanan de Bethléhem, fils de l’oncle paternel d’Asaël;
25 Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
Semma de Harodi, Elica de Harodi,
26 Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
Hélès de Phalti, Hira, fils d’Accès de Thécua;
27 Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
Abiézer d’Anathoth, Mobonnaï de Husati,
28 Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
Selmon, l’Ahohite, Maharaï, le Nétophathite;
29 Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
Héled, fils de Baana, lui aussi Nétophatite, Ithaï, fils de Ribaï de Gabaath des enfants de Benjamin;
30 Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
Banaï, le Pharathonite, Heddaï du torrent de Gaas,
31 Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
Abialbon, l’Arbathite, Azmaveth de Béromi,
32 Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
Eliaba de Salaboni. Les fils de Jassen, Jonathan,
33 mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
Semma d’Orori; Ahiam, fils de Sarar, l’Arorite;
34 Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
Eliphélet, fils d’Aasbaï, fils de Machati; Eliam, fils d’Achitophel, le Gélonite,
35 Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
Hesraï du Carmel, Pharaï d’Arbi,
36 Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
Igaal, fils de Nathan de Soba, Bonni de Gadi,
37 Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
Sélec d’Ammoni, Naharaï, le Bérothite, écuyer de Joab, fils de Sarvia,
38 Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
Ira, le Jéthrite, Gareb, lui aussi Jéthrite,
39 na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.
Urie, l’Héthéen. En tout trente-sept.

< 2 Samweli 23 >