< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
E hizo David una canción para el Señor con estas palabras, el día en que el Señor lo liberó de las manos de todos sus enemigos, y de la mano de Saúl:
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Y él dijo: El Señor es mi roca, mi fortaleza, y mi salvador;
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Dios mío, roca mía, en él pondré mi fe; mi coraza y el poder de mi salvación, mi torre alta y mi lugar seguro; Mi salvador, que me mantiene a salvo del hombre violento.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Enviaré mi clamor al Señor, quien es digno de alabanza; Así me protegeré de los que están contra mí.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Porque las olas de la muerte me rodearon, y los mares del mal me hicieron temer;
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Los lazos del infierno me rodearon: las redes de la muerte cayeron sobre mí. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
En mi angustia mi voz subió al Señor, y mi clamor a mi Dios: mi voz llegó a su oído en su santo Templo, y mi oración llegó a sus oídos.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Entonces la tierra se conmovió con un golpe violento; Las bases del cielo se movieron y temblaron, porque él estaba enojado.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
De su nariz salía humo, y de su boca salía un fuego de destrucción: encendía carbones.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Se doblaron los cielos para que descendiera; y estaba oscuro bajo sus pies.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Y atravesó el aire, sentado en una nube de tormenta, yendo rápidamente sobre las alas del viento.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
E hizo a su alrededor la oscuridad su tabernáculo, una masa de aguas, gruesas nubes de los cielos.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Un fulgor de resplandor salió de su presencia, lloviendo hielo y carbones de fuego.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
El Señor hizo truenos en los cielos, y la voz del Altísimo estaba sonando.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Y él envió sus flechas, llevándolas en todas direcciones; por sus llamas de fuego mis enemigos se turbaron.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Luego se vieron los canales profundos del mar, y se descubrieron las bases del mundo, debido a la ira del Señor, a causa del fuerte soplo del aliento de su nariz.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Me tendió la mano desde de lo alto, me tomó y me sacó de las grandes aguas.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Me liberó de mi fuerte odiador, de los que estaban contra mí, porque eran más fuertes que yo.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Ellos vinieron sobre mí en el día de mi problema, pero el Señor fue mi apoyo.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Me sacó a un lugar espacioso; Él era mi salvador porque se deleitaba en mí.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
El Señor me da la recompensa de mi justicia, porque mis manos están limpias delante de él.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Porque he guardado los caminos del Señor; No he sido apartado de mi Dios.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Porque todas sus decisiones estaban delante de mí, y no aparté de mí sus leyes.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Y fui recto delante de él, y me guardé del pecado.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Por esto el Señor me ha dado la recompensa de mi justicia, porque mis manos están limpias en sus ojos.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Sobre el que tiene misericordia, tú tendrás misericordia; para los rectos serás recto;
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
El que es santo verá que tú eres santo; Pero para el hombre cuyo camino no es recto, serás un juez duro.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Porque tú eres el salvador de los que están en problemas; Pero tus ojos están puestos en los hombres de orgullo, para humillarlos.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Porque tú eres mi luz, oh Señor; y el Señor alumbra mi oscuridad.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Con tu ayuda, me abrí paso a través de un ejército, con la ayuda de mi Dios, he saltado sobre muros.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
En cuanto a Dios, su camino es perfecto, la palabra del Señor es purificada; Él es un escudo seguro para todos aquellos que ponen su fe en él.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Porque ¿quién es Dios sino el Señor? ¿Y quién es la roca, sino nuestro Dios?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Dios me ciñe de poder, guiándome de manera directa.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Hace mis pies ligeros como de ciervo, y me pone en lugares altos.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Él hace que mis manos sean expertas en la guerra, de modo que un arco de bronce se doble por mis brazos.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Me has dado la coraza de tu salvación, y tu misericordia me ha hecho grande.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Has ensanchado mis pasos debajo de mí, para que mis pies no se deslicen.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Voy tras mis enemigos y los alcancé; No volviendo atrás hasta que todos sean vencidos.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Les he enviado destrucción y les he dado heridas para que no puedan levantarse: están bajo mis pies.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Porque he sido armado por ti con fuerza para el combate; has abatido a los que salieron contra mí.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Has hecho que mis enemigos huyan delante de mí, y a los que me odiaban destruí.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Estaban gritando, pero no había nadie que acudiera en su ayuda: ni siquiera él Señor, les respondió.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Entonces fueron aplastados tan pequeños como el polvo de la tierra, pisoteados bajo mis pies como él lodo de las calles.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Me has liberado de las luchas de mi pueblo; Tú me has hecho cabeza de las naciones; un pueblo del cual no tenía conocimiento serán mis siervos.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Los extranjeros de otros países, se pondrán bajo mi autoridad: desde el momento en que mi nombre llegue a sus oídos, me obedecerán.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Los extranjeros se debilitarán y saldrán de sus lugares secretos temblando de miedo.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
El Señor está vivo; Alabado sea mi roca, exaltado sea él Dios de mi salvación.
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Es Dios quien envía castigo a mis enemigos, y pone a los pueblos bajo mi gobierno.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Me libera de mis enemigos. Me levanto sobre los que me atacan: me has liberado del hombre violento.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Por eso te alabaré, oh Señor, entre las naciones, y cantaré alabanza a tu nombre.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
La gran salvación da a su rey. Y muestra su fidelidad a su pacto; tiene misericordia del rey de su elección, David, y de su descendencia para siempre.

< 2 Samweli 22 >