< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
David cantó las palabras de este cántico al Señor el día en que el Señor lo salvó de todos sus enemigos y de Saúl.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Entonces cantó: El Señor es mi roca, mi fortaleza y mi salvador.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Él es mi Dios, mi roca que me protege. Él me protege del mal, su poder me salva, me mantiene seguro. Él es mi protector; es mi salvador; me libra de la violencia.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Pido ayuda al Señor, merecedor de alabanza, y me salva de los que me odian.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Las olas de la muerte me arrastran, las aguas de la destrucción me inundan;
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
El sepulcro enrolló sus cuerdas en torno a mí; la muerte me tendió trampas. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
En mi desesperación invoqué al Señor; clamé a mi Dios. Él escuchó mi voz desde su Templo; mi grito de auxilio llegó a sus oídos.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
La tierra se estremeció, los cimientos de los cielos temblaron por su cólera
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Humo salía de sus narices, y fuego de su boca, carbones ardientes que ardían ante él.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Apartó los cielos y descendió, con nubes oscuras bajo sus pies.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Montado en un ser celestial voló, abalanzándose sobre las alas del viento.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Se escondió en las tinieblas, cubriéndose con negras nubes de lluvia.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
De su resplandor brotaron carbones ardientes.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
El Señor tronó desde el cielo; resonó la voz del Altísimo.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Disparó sus flechas, dispersando a sus enemigos, los derrotó con sus rayos.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
El Señor rugió, y con el viento del aliento de su nariz se vieron los valles del mar y se descubrieron los cimientos de la tierra.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Bajó su mano desde arriba y me agarró. Me sacó de las aguas profundas.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Me rescató de mis poderosos enemigos, de los que me odiaban y eran mucho más fuertes que yo.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Se abalanzaron sobre mí en mi peor momento, pero el Señor me sostuvo.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Me liberó, me rescató porque es feliz conmigo.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
El Señor me recompensó por hacer lo correcto; me pagó porque soy inocente.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Porque he seguido los caminos del Señor; no he pecado apartándome de mi Dios.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
He tenido presente todas sus leyes; no he ignorado sus mandamientos.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Soy irreprochable a sus ojos; me guardo de pecar.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
El Señor me ha recompensado por hacer lo justo. Soy inocente ante sus ojos.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Demuestras tu fidelidad a los que son fieles; demuestras integridad a los que son íntegros,
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Te muestras puro a los que son puros, pero te muestras astuto con los astutos.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Tú salvas a los humildes, pero tus ojos vigilan a los soberbios para abatirlos.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Tú, Señor, eres mi lámpara. El Señor ilumina mis tinieblas.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Contigo puedo abatir una tropa de soldados; contigo, Dios mío, puedo escalar un muro de la fortaleza.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
El camino de Dios es absolutamente correcto. La palabra del Señor es digna de confianza. Es un escudo para todos los que acuden a él en busca de protección.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Porque ¿quién es Dios sino el Señor? ¿Quién es la Roca, sino nuestro Dios?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Dios me hace fuerte y me mantiene seguro.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Me hace seguro como el ciervo, capaz de caminar por las alturas con seguridad.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Me enseña a luchar en la batalla; me da la fuerza para tensar un arco de bronce.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Me protege con el escudo de su salvación; su ayuda me ha engrandecido.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Me diste espacio para caminar y evitaste que mis pies resbalaran.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Perseguí a mis enemigos y los alcancé. No me devolví hasta haberlos destruido.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Los derribé y no pudieron levantarse. Cayeron a mis pies.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Me hiciste fuerte para la batalla; hiciste que los que se levantaron contra mí se arrodillaran ante mí.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Hiciste que mis enemigos huyeran; destruí a todos mis enemigos.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ellos clamaron por ayuda, pero nadie vino a rescatarlos. Incluso clamaron al Señor, pero él no les respondió.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Los convertí en polvo, como el polvo de la tierra. Los aplasté y los arrojé como lodo en la calle.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Me rescataste de los pueblos rebeldes; me mantuviste como gobernante de las naciones: gente que no conocía ahora me sirve.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Los extranjeros se acobardan ante mí; en cuanto oyen hablar de mí, me obedecen.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Se desalientan y salen temblando de sus fortalezas.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
¡El Señor vive! ¡Bendita sea mi Roca! ¡Alabado sea el Dios que me salva!
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Dios me vindica, pone a los pueblos bajo mis pies,
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Y me libera de los que me odian. Me mantiene a salvo de los que se rebelan contra mí, me salva de los hombres violentos.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Por eso te alabaré entre las naciones, Señor; cantaré alabanzas sobre lo que tú eres.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Has salvado al rey tantas veces, mostrando tu amor fiel a David, tu ungido, y a sus descendientes por siempre.

< 2 Samweli 22 >