< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
E fallou David ao Senhor as palavras d'este cantico, no dia em que o Senhor o livrou das mãos de todos os seus inimigos e das mãos de Saul.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Disse pois: O Senhor é o meu rochedo, e o meu logar forte, e o meu libertador.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Deus é o meu rochedo, n'elle confiarei: o meu escudo, e a força da minha salvação, o meu alto retiro, e o meu refugio. O meu Salvador, de violencia me salvaste.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
O Senhor, digno de louvor, invoquei, e de meus inimigos fiquei livre.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Porque me cercaram as ondas de morte: as torrentes de Belial me assombraram.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Cordas do inferno me cingiram; encontraram-me laços de morte. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Estando em angustia, invoquei ao Senhor, e a meu Deus clamei: do seu templo ouviu elle a minha voz, e o meu clamor chegou aos seus ouvidos.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Então se abalou e tremeu a terra, os fundamentos dos céus se moveram e abalaram, porque elle se irou.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Subiu o fumo de seus narizes, e da sua bocca um fogo devorador: carvões se incenderam d'elle.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
E abaixou os céus, e desceu: e uma escuridão havia debaixo de seus pés.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
E subiu sobre um cherubim, e voou: e foi visto sobre as azas do vento.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
E por tendas poz as trevas ao redor de si: ajuntamento d'aguas, nuvens dos céus.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Pelo resplendor da sua presença brasas de fogo se accendem.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Trovejou desde os céus o Senhor: e o Altissimo fez soar a sua voz.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
E disparou frechas, e os dissipou: raios e os perturbou.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
E appareceram as profundezas do mar, os fundamentos do mundo se descobriram: pela reprehensão do Senhor, pelo sopro do vento dos seus narizes.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Desde o alto enviou, e me tomou: tirou-me das muitas aguas.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Livrou-me do meu possante inimigo, e d'aquelles que me tinham odio, porque eram mais fortes do que eu.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Encontraram-me no dia da minha calamidade: porém o Senhor se fez o meu esteio.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
E tirou-me á largura, e arrebatou-me d'ali; porque tinha prazer em mim.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Recompensou-me o Senhor conforme á minha justiça: conforme á pureza de minhas mãos me retribuiu.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Porque guardei os caminhos do Senhor: e não me apartei impiamente do meu Deus.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Porque todos os seus juizos estavam diante de mim: e de seus estatutos me não desviei.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Porém fui sincero perante elle: e guardei-me da minha iniquidade.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
E me retribuiu o Senhor conforme á minha justiça, conforme á minha pureza diante dos seus olhos.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Com o benigno te mostras benigno: com o varão sincero te mostras sincero.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Com o puro te mostras puro: mas com o perverso te mostras avesso.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
E o povo afflicto livras: mas teus olhos são contra os altivos, e tu os abaterás.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Porque tu, Senhor, és a minha candeia: e o Senhor esclarece as minhas trevas.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Porque comtigo passo pelo meio d'um esquadrão: pelo meu Deus salto um muro.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
O caminho de Deus é perfeito, e a palavra do Senhor refinada; e é o escudo de todos os que n'elle confiam.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Porque, quem é Deus, senão o Senhor? e quem é rochedo, senão o nosso Deus?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Deus é a minha fortaleza e a minha força, e elle perfeitamente desembaraça o meu caminho.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Faz elle os meus pés como os das cervas, e me põe sobre as minhas alturas.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Instrue as minhas mãos para a peleja, de maneira que um arco de cobre se quebra pelos meus braços.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Tambem me déste o escudo da tua salvação, e pela tua brandura me vieste a engrandecer.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Alargaste os meus passos debaixo de mim, e não vacillaram os meus artelhos.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Persegui os meus inimigos, e os derrotei, e nunca me tornei até que os consumisse.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
E os consumi, e os atravessei, de modo que nunca mais se levantaram, mas cairam debaixo dos meus pés.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Porque me cingiste de força para a peleja, fizeste abater-se debaixo de mim os que se levantaram contra mim.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
E deste-me o pescoço de meus inimigos, d'aquelles que me tinham odio, e os destrui.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Olharam, porém não houve libertador: sim, para o Senhor, porém não lhes respondeu.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Então os moí como o pó da terra; como a lama das ruas os trilhei e dissipei.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Tambem me livraste das contendas do meu povo; guardaste-me para cabeça das nações; o povo que não conhecia me servirá.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Os filhos de estranhos se me sujeitaram; ouvindo a minha voz, me obedeceram.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Os filhos de estranhos descairam; e, cingindo-se, sairam dos seus encerramentos.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Vive o Senhor, e bemdito seja o meu rochedo; e exaltado seja Deus, a rocha da minha salvação:
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
O Deus que me dá inteira vingança, e sujeita os povos debaixo de mim.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
E o que me tira d'entre os meus inimigos: e tu me exaltas sobre os que contra mim se levantam; do homem violento me livras.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Por isso, ó Senhor, te louvarei entre as gentes, e entoarei louvores ao teu nome.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Elle é a torre das salvações do seu rei, e usa de benignidade com o seu ungido, com David, e com a sua semente para sempre.

< 2 Samweli 22 >