< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Locutus est autem David Domino verba carminis huius, in die qua liberavit eum Dominus de manu omnium inimicorum suorum, et de manu Saul,
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
et ait: Dominus petra mea, et robur meum, et salvator meus.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Deus fortis meus sperabo in eum: scutum meum, et cornu salutis meæ: elevator meus, et refugium meum: salvator meus, de iniquitate liberabis me.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Laudabilem invocabo Dominum: et ab inimicis meis salvus ero.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Quia circumdederunt me contritiones mortis: torrentes Belial terruerunt me.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Funes inferni circumdederunt me: prævenerunt me laquei mortis. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
In tribulatione mea invocabo Dominum, et ad Deum meum clamabo: et exaudiet de templo suo vocem meam, et clamor meus venit ad aures eius.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Commota est et contremuit terra: fundamenta montium concussa sunt, et conquassata, quoniam iratus est eis.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Ascendit fumus de naribus eius, et ignis de ore eius vorabit: carbones succensi sunt ab eo.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Inclinavit cælos, et descendit: et caligo sub pedibus eius.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Et ascendit super cherubim, et volavit: et lapsus est super pennas venti.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Posuit tenebras in circuitu suo latibulum: cribrans aquas de nubibus cælorum.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Præ fulgore in conspectu eius, succensi sunt carbones ignis.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Tonabit de cælo Dominus: et Excelsus dabit vocem suam.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Misit sagittas et dissipavit eos: fulgur, et consumpsit eos.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Et apparuerunt effusiones maris, et revelata sunt fundamenta orbis ab increpatione Domini, ab inspiratione spiritus furoris eius.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Misit de excelso, et assumpsit me: et extraxit me de aquis multis.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Liberavit me ab inimico meo potentissimo, et ab his qui oderant me: quoniam robustiores me erant.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Prævenit me in die afflictionis meæ, et factus est Dominus firmamentum meum.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Et eduxit me in latitudinem: liberavit me, quia complacui ei.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Retribuet mihi Dominus secundum iustitiam meam: et secundum munditiam manuum mearum reddet mihi.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Quia custodivi vias Domini, et non egi impie, a Deo meo.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Omnia enim iudicia eius in conspectu meo: et præcepta eius non amovi a me.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Et ero perfectus cum eo: et custodiam me ab iniquitate mea.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Et restituet mihi Dominus secundum iustitiam meam: et secundum munditiam manuum mearum, in conspectu oculorum suorum.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Cum sancto sanctus eris: et cum robusto perfectus.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Cum electo electus eris: et cum perverso perverteris.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Et populum pauperem salvum facies: oculisque tuis excelsos humiliabis.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Quia tu lucerna mea Domine: et tu Domine illuminabis tenebras meas.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
In te enim curram accinctus: in Deo meo transiliam murum.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Deus, immaculata via eius, eloquium Domini igne examinatum: scutum est omnium sperantium in se.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Quis est Deus præter Dominum: et quis fortis præter Deum nostrum?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Deus qui accinxit me fortitudine: et complanavit perfectam viam meam.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Coæquans pedes meos cervis, et super excelsa mea statuens me.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Docens manus meas ad prælium, et componens quasi arcum æreum brachia mea.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Dedisti mihi clypeum salutis tuæ: et mansuetudo tua multiplicavit me.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Dilatabis gressus meos subtus me: et non deficient tali mei.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Persequar inimicos meos, et conteram: et non convertar donec consumam eos.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Consumam eos et confringam, ut non consurgant: cadent sub pedibus meis.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Accinxisti me fortitudine ad prælium: incurvasti resistentes mihi subtus me.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Inimicos meos dedisti mihi dorsum: odientes me, et disperdam eos.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Clamabunt, et non erit qui salvet, ad Dominum, et non exaudiet eos.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Delebo eos ut pulverem terræ: quasi lutum platearum comminuam eos atque confringam.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Salvabis me a contradictionibus populi mei: custodies me in caput Gentium: populus, quem ignoro, serviet mihi.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Filii alieni resistent mihi, auditu auris obedient mihi.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Filii alieni defluxerunt, et contrahentur in angustiis suis.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Vivit Dominus, et benedictus Deus meus: et exaltabitur Deus fortis salutis meæ.
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Deus qui das vindictas mihi, et deiicis populos sub me.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Qui educis me ab inimicis meis, et a resistentibus mihi elevas me: a viro iniquo liberabis me:
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Propterea confitebor tibi Domine in gentibus: et nomini tuo cantabo.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Magnificans salutes regis sui, et faciens misericordiam Christo suo David, et semini eius in sempiternum.

< 2 Samweli 22 >