< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
וידבר דוד ליהוה את דברי השירה הזאת ביום הציל יהוה אתו מכף כל איביו ומכף שאול
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
ויאמר יהוה סלעי ומצדתי ומפלטי לי
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
אלהי צורי אחסה בו מגני וקרן ישעי משגבי ומנוסי משעי מחמס תשעני
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
מהלל אקרא יהוה ומאיבי אושע
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
כי אפפני משברי מות נחלי בליעל יבעתני
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
חבלי שאול סבני קדמני מקשי מות (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
בצר לי אקרא יהוה ואל אלהי אקרא וישמע מהיכלו קולי ושועתי באזניו
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
ותגעש (ויתגעש) ותרעש הארץ מוסדות השמים ירגזו ויתגעשו כי חרה לו
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
עלה עשן באפו ואש מפיו תאכל גחלים בערו ממנו
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
ויט שמים וירד וערפל תחת רגליו
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
וירכב על כרוב ויעף וירא על כנפי רוח
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
וישת חשך סביבתיו סכות חשרת מים עבי שחקים
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
מנגה נגדו בערו גחלי אש
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
ירעם מן שמים יהוה ועליון יתן קולו
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
וישלח חצים ויפיצם ברק ויהמם (ויהם)
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
ויראו אפקי ים יגלו מסדות תבל בגערת יהוה מנשמת רוח אפו
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
ישלח ממרום יקחני ימשני ממים רבים
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
יצילני מאיבי עז משנאי כי אמצו ממני
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
יקדמני ביום אידי ויהי יהוה משען לי
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
ויצא למרחב אתי יחלצני כי חפץ בי
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
יגמלני יהוה כצדקתי כבר ידי ישיב לי
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
כי שמרתי דרכי יהוה ולא רשעתי מאלהי
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
כי כל משפטו לנגדי וחקתיו לא אסור ממנה
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
ואהיה תמים לו ואשתמרה מעוני
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
וישב יהוה לי כצדקתי כברי לנגד עיניו
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
עם חסיד תתחסד עם גבור תמים תתמם
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
עם נבר תתבר ועם עקש תתפל
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
ואת עם עני תושיע ועיניך על רמים תשפיל
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
כי אתה נירי יהוה ויהוה יגיה חשכי
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
כי בכה ארוץ גדוד באלהי אדלג שור
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
האל תמים דרכו אמרת יהוה צרופה-- מגן הוא לכל החסים בו
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
כי מי אל מבלעדי יהוה ומי צור מבלעדי אלהינו
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
האל מעוזי חיל ויתר תמים דרכו (דרכי)
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
משוה רגליו (רגלי) כאילות ועל במתי יעמדני
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
מלמד ידי למלחמה ונחת קשת נחושה זרעתי
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
ותתן לי מגן ישעך וענתך תרבני
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
תרחיב צעדי תחתני ולא מעדו קרסלי
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
ארדפה איבי ואשמידם ולא אשוב עד כלותם
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
ואכלם ואמחצם ולא יקומון ויפלו תחת רגלי
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
ותזרני חיל למלחמה תכריע קמי תחתני
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
ואיבי תתה לי ערף משנאי ואצמיתם
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
ישעו ואין משיע אל יהוה ולא ענם
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
ואשחקם כעפר ארץ כטיט חוצות אדקם ארקעם
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
ותפלטני מריבי עמי תשמרני לראש גוים עם לא ידעתי יעבדני
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
בני נכר יתכחשו לי לשמוע אזן ישמעו לי
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
בני נכר יבלו ויחגרו ממסגרותם
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
חי יהוה וברוך צורי וירם אלהי צור ישעי
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
האל הנתן נקמת לי ומריד עמים תחתני
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
ומוציאי מאיבי ומקמי תרוממני מאיש חמסים תצילני
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
על כן אודך יהוה בגוים ולשמך אזמר
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
מגדיל (מגדול) ישועות מלכו ועשה חסד למשיחו לדוד ולזרעו עד עולם

< 2 Samweli 22 >