< 2 Samweli 22 >
1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Und David redete zu dem HERRN die Worte dieses Liedes, am Tage, als der HERR ihn aus der Hand aller seiner Feinde und aus der Hand Sauls errettet hatte.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Er sprach: Der HERR ist meine Felsenkluft, meine Burg und meine Zuflucht;
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
mein Gott ist mein Fels, darin ich mich berge, mein Schild und das Horn meines Heils, meine Festung und meine Zuflucht, mein Erretter, der mich von Gewalttat befreit.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Den HERRN, den Hochgelobten, rief ich an und wurde von meinen Feinden errettet.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Todeswehen umfingen mich, Bäche Belials schreckten mich;
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
Stricke der Unterwelt umschlangen mich, Todesschlingen kamen mir entgegen. (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
In meiner Angst rief ich den HERRN an und schrie zu meinem Gott; er hörte in seinem Tempel meine Stimme, mein Schreien kam vor ihn zu seinen Ohren.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Die Erde bebte und erzitterte, die Grundfesten des Himmels wurden erschüttert und bebten, weil er zornig war.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Rauch stieg auf von seiner Nase und verzehrendes Feuer aus seinem Mund, Feuerglut brannte daraus hervor.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Er neigte den Himmel und fuhr herab, und Dunkel war unter seinen Füßen;
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
er fuhr auf dem Cherub und flog daher, er schwebte auf den Fittichen des Windes.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Er machte Finsternis um sich her zu seinem Gezelt, dunkle Wasser, dichte Wolken.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Vom Glanz vor ihm brannte Feuerglut;
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
und der HERR donnerte vom Himmel, der Höchste ließ seine Stimme erschallen;
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
er schoß seine Pfeile und zerstreute sie, [schleuderte] Blitze und schreckte sie.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Da sah man die Betten des Meeres, und die Gründe des Erdbodens wurden aufgedeckt von des HERRN Schelten, von dem Schnauben seines grimmigen Zorns!
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Er langte herab aus der Höhe und ergriff mich, er zog mich aus großen Wassern;
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
er rettete mich von meinem mächtigen Feind und von meinen Hassern; denn sie waren mir zu stark;
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
sie hatten mich überfallen zur Zeit meines Unglücks; aber der HERR ward mir zur Stütze
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
und führte mich heraus in die Weite, er befreite mich; denn er hatte Wohlgefallen an mir.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Der HERR vergalt mir nach meiner Gerechtigkeit, nach der Reinheit meiner Hände lohnte er mir;
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
denn ich habe die Wege des HERRN bewahrt und bin nicht abgefallen von meinem Gott,
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
sondern ich hatte alle seine Rechte vor mir und stieß seine Satzungen nicht von mir,
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
und ich hielt es ganz mit ihm und hütete mich vor meiner Sünde.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Darum vergalt mir der HERR nach meiner Gerechtigkeit, nach der Reinheit meiner Hände vor seinen Augen.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Gegen den Frommen erzeigst du dich fromm, gegen den Redlichen redlich,
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
gegen den Reinen erzeigst du dich rein, aber den Hinterlistigen überlistest du.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Denn du rettest alles elende Volk, aber du erniedrigst die Augen aller Stolzen.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Denn du, HERR, bist meine Leuchte; der HERR macht meine Finsternis licht;
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
denn mit dir kann ich Kriegsvolk zerschmeißen und mit meinem Gott über die Mauern springen.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Dieser Gott! Sein Weg ist vollkommen, die Rede des HERRN ist geläutert; er ist ein Schild allen, die ihm vertrauen.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Denn wer ist Gott, außer dem HERRN, und wer ist ein Fels, außer unserm Gott?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Gott umgürtet mich mit Kraft und macht meinen Weg unsträflich,
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
er macht meine Füße den Hirschen gleich und stellt mich auf meine Höhen;
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
er lehrt meine Hände streiten und meine Arme den ehernen Bogen spannen;
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
du gabst mir den Schild deines Heils, und deine Herablassung machte mich groß;
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
du machtest mir Raum zum Gehen, daß meine Knöchel nicht wankten.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Ich jagte meinen Feinden nach und vertilgte sie und kehrte nicht um, bis sie aufgerieben waren;
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
ich rieb sie auf und zerschmetterte sie, daß sie nicht mehr aufstehen konnten; sie fielen unter meine Füße.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Du hast mich gegürtet mit Kraft zum Streit, du hast unter mich gebeugt, die sich wider mich setzten.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Du wandtest mir den Rücken meiner Feinde zu, und meine Hasser habe ich vertilgt.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Sie schrieen, aber da war kein Retter; zu dem HERRN, aber er antwortete ihnen nicht.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Und ich zerrieb sie wie Erdenstaub, zertrat sie wie Straßenkot und warf sie hinaus.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Du rettetest mich aus den Zänkereien des Volkes und bewahrtest mich auf zum Haupt der Heiden; ein Volk, das ich nicht kannte, dient mir;
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
die Kinder der Fremden schmeicheln mir, sie folgen mir aufs Wort;
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
die Kinder der Fremden verzagen und kommen zitternd hervor aus ihren Schlössern.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Es lebt der HERR, und gepriesen sei mein Fels, und erhoben werde der Gott meines Heils!
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Der Gott, der mir Rache verlieh und mir die Völker unterwarf;
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
der mich meinen Feinden entrinnen ließ und mich trotz meiner Widersacher erhöhte, mich errettete von dem gewalttätigen Mann!
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Darum will ich dich, o HERR, loben unter den Heiden und deinem Namen singen,
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
der seinem Könige große Siege verliehen hat und seinem Gesalbten Gnade erweist, David und seinem Samen bis in Ewigkeit!