< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Or, David dit au Seigneur les paroles de ce cantique, au jour où le Seigneur le délivra de la main de tous ses ennemis et de la main de Saül.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Et il dit: Le Seigneur est mon rocher, et ma force, et mon sauveur.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Dieu est mon fort, j’espérerai en lui; il est mon bouclier, l’appui de mon salut; c’est lui qui m’élève, et qui est mon refuge; mon Sauveur, vous me délivrerez de l’iniquité.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
J’invoquerai le Seigneur, digne de louanges, et je serai délivré de mes ennemis.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Parce que les brisements de la mort m’ont environné, les torrents de Bélial m’ont épouvanté.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Les liens de l’enfer m’ont environné, les lacs de la mort m’ont enveloppé. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Dans ma tribulation, j’invoquerai le Seigneur, et c’est vers mon Dieu que je crierai, et il exaucera ma voix de son temple, et mon cri viendra jusqu’à ses oreilles.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
La terre s’est émue et a tremblé; les fondements des montagnes ont été agités et ébranlés, parce que le Seigneur s’est irrité contre elles.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Une fumée est montée de ses narines, et un feu sorti de sa bouche dévorera; des charbons en ont été allumés.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Il a incliné les cieux, et il est descendu, et un nuage obscur était sous ses pieds.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Il a monté sur des chérubins, et il a pris son vol, et il s’est élancé sur des ailes de vent.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Il a mis des ténèbres autour de lui pour se cacher; il a fait distiller des eaux des nuées des cieux.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
À la lumière qui éclate en sa présence, des charbons de feu se sont allumés.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Le Seigneur tonnera du ciel, et le Très-Haut élèvera sa voix.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Il a lancé des flèches, et il les a dissipés; la foudre, et il les a consumés.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Alors ont paru les abîmes de la mer, les fondements du monde ont été mis à nu, à la menace du Seigneur, au souffle du vent de sa colère.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Il a envoyé d’en haut, et il m’a pris, et il m’a retiré d’un gouffre d’eaux.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Il m’a délivré de mon ennemi très puissant, et de ceux qui me haïssaient, parce qu’ils étaient plus forts que moi.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Il m’a prévenu au jour de mon affliction, et le Seigneur s’est fait mon appui.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Et il m’a mis au large; il m’a délivré, parce que je lui ai plu.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Le Seigneur me rétribuera selon ma justice, et il me rendra selon la pureté de mes mains,
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Parce que j’ai gardé les voies du Seigneur, et que je n’ai pas agi avec impiété en m’éloignant de mon Dieu.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Tous ses jugements sont devant mes yeux, et je n’ai point éloigné ses préceptes de moi.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Et je serai parfait avec lui, et je me garderai de mon iniquité.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Et le Seigneur me rendra selon ma justice, et selon la pureté de mes mains devant ses yeux.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Avec un saint vous serez saint, et avec un fort, parfait.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Avec un homme excellent, vous serez excellent, et avec un pervers, vous agirez selon sa perversité.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Vous sauverez un peuple pauvre, et par vos yeux vous humilierez les superbes.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Parce que c’est vous, Seigneur, qui êtes ma lampe; vous, qui illuminez mes ténèbres.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Car avec vous je courrai tout prêt au combat; avec mon Dieu, je franchirai un mur.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Dieu, sa voie est sans tache, la parole du Seigneur est éprouvée par le feu; il est le bouclier de tous ceux qui espèrent en lui.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Qui est Dieu, excepté le Seigneur? et qui est le fort, excepté notre Dieu?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Le Dieu qui m’a revêtu de force, et qui m’a aplani ma voie parfaite;
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Egalant mes pieds aux cerfs, et m’établissant sur mes lieux élevés;
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Instruisant mes mains au combat, et rendant mes bras comme un arc d’airain.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Vous m avez donné le bouclier de votre salut, et votre bonté ma multiplié.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Vous agrandirez mes pas sous moi, et mes talons ne chancelleront point.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Je poursuivrai mes ennemis, et je les briserai; et je ne reviendrai point jusqu’à ce que je les détruise.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Je les détruirai et les briserai, de manière qu’ils ne se relèvent point; ils tomberont sous mes pieds.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Vous m’avez revêtu de force pour le combat, vous avez fait plier sous moi ceux qui me résistaient.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Vous m’avez livré mes ennemis par derrière; ceux qui me haïssaient, et je les exterminerai.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ils crieront, et il n’y aura personne qui les sauve; ils crieront vers le Seigneur, et il ne les exaucera pas.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Je les dissiperai comme de la poussière de la terre, et je les broierai comme de la boue de rues et les briserai.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Vous me sauverez des contradictions de mon peuple; vous me garderez pour chef de nations; un peuple que j’ignore me servira.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Des fils d’étranger me résisteront; en écoutant de leurs oreilles, ils m’obéiront.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Des fils d’étranger se sont dispersés, et ils seront resserrés dans leurs défilés.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Le Seigneur vit, et béni mon Dieu! et le Dieu fort de mon salut sera exalté;
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Vous, le Dieu qui me donnez des vengeances, et qui abattez des peuples sous moi;
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Qui m’arrachez à mes ennemis et qui m’élevez au-dessus de ceux qui me résistent: vous me délivrerez de l’homme inique.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
À cause de cela, je vous confesserai. Seigneur, parmi les nations, et je chanterai votre nom,
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Qui exalte les victoires de son roi, et qui fait miséricorde à son christ, David, et à sa postérité pour toujours.

< 2 Samweli 22 >