< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Et David adressa à l'Éternel les paroles de ce cantique, lorsque l'Éternel l'eut délivré de la main de tous ses ennemis et de la main de Saül
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
et il dit: Éternel, mon rocher, mon asile et mon libérateur,
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
ô Dieu, mon rocher, où je vais m'abriter! mon bouclier, corne de mon salut, mon boulevard et mon refuge, mon Sauveur, de la violence tu me sauves!
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Loué soit l'Éternel, me suis-je écrié, et de mes ennemis j'ai été délivré.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Car les vagues de la mort m'enserraient, et les torrents de l'adversité m'épouvantaient,
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
les chaînes des Enfers m'enlaçaient et j'étais pris dans les rêts de la mort. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Dans mon angoisse j'invoquai l'Éternel et à mon Dieu j'adressai mon appel, et de son palais Il entendit ma voix, et mes cris [vinrent] à ses oreilles.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Alors la terre oscilla et trembla, les fondements des Cieux s'ébranlèrent et tremblèrent, parce qu'il était courroucé.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Une fumée sortit de ses narines, et de sa bouche, un feu dévorant, et Il fit jaillir des charbons ardents,
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
et Il inclina le Ciel et Il descendit, et l'obscurité était sous ses pieds.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Et Il était monté sur le Chérubin et volait Et Il se montra sur les ailes du vent,
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
et autour de Lui Il fit sa tente des ténèbres, des amas d'eau et des sombres nuées.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
De la splendeur qui le précède, jaillirent les charbons ardents.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
L'Éternel tonna du ciel et le Très-Haut émit sa voix,
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
et Il lança ses flèches et Il les dissipa, la foudre, et Il les défit.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Et l'on vit paraître les vallées de la mer, et les fondements du monde furent mis à nu au grondement de l'Éternel, au souffle du vent de ses narines.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Il tendit [sa main] d'en haut et me prit et Il me retira des grandes eaux.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Il me sauva de mes puissants ennemis, de mes adversaires qui l'emportaient sur moi.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Ils m'attaquaient au jour du malheur, mais l'Éternel fut un soutien pour moi.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Il m'amena au large, Il me dégagea parce qu'il m'était propice.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
L'Éternel me traita selon ma justice, et me rendit selon la pureté de mes mains;
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
car je gardais les voies de l'Éternel, et n'étais point rebelle à mon Dieu.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Car j'avais toutes ses lois sous les yeux, et ne m'écartais pas de ses commandements;
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
j'étais sans reproche envers Lui, et je prenais garde de me rendre coupable.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Aussi l'Éternel me rendit selon ma justice, selon ma pureté dont Il était témoin.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
A celui qui t'aime, tu donnes ton amour, tu te montres juste pour l'homme juste,
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
tu es pur envers celui qui est pur, et tu trahis celui qui est perfide.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Et tu es en aide au peuple qui souffre, et tes yeux sont sur les superbes pour les humilier.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Oui, tu as été mon flambeau, Éternel, et l'Éternel éclaira mes ténèbres.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Avec toi j'affrontai des bataillons, et avec mon Dieu je franchis des murailles.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Les voies de Dieu ne sont point trompeuses, et la parole de l'Éternel est sans alliage. Il est un bouclier pour quiconque le réclame.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Car qui est-ce qui est Dieu hors l'Éternel? et qui est un rocher sinon notre Dieu,
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
ce Dieu qui fut ma forte citadelle et guida le juste dans Sa voie?
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Il assimila mes pieds à ceux de la biche, et Il m'établit sur mes hauteurs.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Il forma mes mains au combat, et mon bras sut bander l'arc d'airain.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Tu me donnas le bouclier de ton secours, et en m'exauçant tu m'agrandis.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Sous mes pieds tu donnas de l'espace à mes pas, et mes talons ne furent point vacillants.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Je poursuivis mes ennemis et les anéantis, et je ne revins pas qu'ils ne fussent détruits;
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
je les achevai, et les écrasai, et ils n'ont pu se relever, ils tombèrent sous mes pieds.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Tu me ceignis de force pour la bataille, et tu fis plier mes adversaires sous moi.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Tu me fis voir le dos de mes ennemis, et j'anéantis ceux qui me haïssaient.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ils regardèrent autour d'eux; il n'y eut point de sauveur, vers l'Éternel, Il ne leur répondit pas.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Je les pulvérisai comme la poudre de la terre, comme la boue des rues les foulai, les broyai.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Tu me délivras des attaques de mon peuple, et me gardas pour chef des nations; des peuples à moi inconnus me sont asservis;
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
les enfants de l'étranger devinrent mes flatteurs; sur ma renommée ils se soumirent.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Les enfants de l'étranger sont en décadence, et quittent alarmés leurs châteaux.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Vive l'Éternel! béni soit mon rocher! qu'il soit exalté le Dieu, mon rocher, mon sauveur,
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
le Dieu qui m'accorda la vengeance et m'assujettit les peuples,
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
qui me délivra de mes ennemis, m'éleva au-dessus de mes adversaires et me fit échapper à l'homme violent!
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Aussi je veux te chanter parmi les peuples, Éternel, et célébrer ton Nom,
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
ô toi, qui accordes un grand salut à ton Roi, et fais miséricorde à ton Oint, à David et à sa race éternellement.

< 2 Samweli 22 >