< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
David adressa à Yahweh les paroles de ce cantique, au jour où Yahweh l'eut délivré de la main de tous ses ennemis et de la main de Saül.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
Il dit: Yahweh est mon rocher, ma forteresse, mon libérateur,
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Dieu est mon roc où je trouve un asile, mon bouclier, la corne de mon salut, ma haute retraite et mon refuge. Mon Sauveur, tu m'as sauvé de la violence.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
J'invoquai celui qui est digne de louange, Yahweh, et je fus délivré de mes ennemis.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Car les vagues de la mort m'environnaient, les torrents de Bélial m'épouvantaient.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Les liens du schéol m'enlaçaient, les filets de la mort étaient tombés devant moi. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Dans ma détresse, j'invoquai Yahweh, et je criai vers mon Dieu; de son temple il entendit ma voix, et mon cri parvint à ses oreilles.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
La terre fut ébranlée et trembla, les fondements du ciel s'agitèrent; ils furent ébranlés, parce qu'il était courroucé;
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
une fumée montait de ses narines, et un feu dévorant sortait de sa bouche; il en jaillissait des charbons embrasés.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Il abaissa les cieux, et descendit; une sombre nuée était sous ses pieds.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Il monta sur un Chérubin, et il volait, il apparut sur les ailes du vent.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Il s'entoura des ténèbres comme d'une tente, d'amas d'eaux et de sombres nuages.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
De l'éclat qui le précédait jaillissaient des charbons de feu.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Yahweh tonna des cieux, le Très-Haut fit retentir sa voix.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Il lança des flèches et les dispersa, la foudre, et il les confondit.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Alors le lit de la mer apparut, les fondements de la terre furent mis à nu; à la menace de Yahweh, au souffle du vent de ses narines.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Il étendit sa main d'en haut et me saisit, il me retira des grandes eaux;
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
il me délivra de mon ennemi puissant, de ceux qui me haïssaient, alors qu'ils étaient plus forts que moi.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Ils m'avaient surpris au jour de mon malheur, mais Yahweh fut mon appui.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Il m'a mis au large, il m'a sauvé, parce qu'il s'est complu en moi.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Yahweh m'a récompensé selon ma justice, il m'a rendu selon la pureté de mes mains.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Car j'ai gardé les voies de Yahweh, et je n'ai pas péché, pour m'éloigner de mon Dieu.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Tous ses jugements étaient devant moi, et je ne m'écartais pas de ses lois.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
J'étais sans reproche envers lui, et je me tenais en garde contre mon iniquité.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Yahweh m'a rendu selon ma justice, selon ma pureté devant ses yeux.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Avec celui qui est bon, tu te montres bon, avec l'homme droit, tu te montres droit;
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
avec celui qui est pur, tu te montres pur, et avec le fourbe, tu agis perfidement.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Tu sauves le peuple humilié, et de ton regard tu abaisses les orgueilleux.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Car tu es ma lumière, ô Yahweh; Yahweh éclaire mes ténèbres.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Avec toi je me précipite sur les bataillons armés. Avec mon Dieu je franchis les murailles.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Dieu!... Ses voies sont parfaites, la parole de Yahweh est éprouvée; il est un bouclier pour tous ceux qui se confient en lui.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Car qui est Dieu, si ce n'est Yahweh, et qui est un rocher, si ce n'est notre Dieu?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Dieu est ma forte citadelle, il conduit l'homme intègre dans sa voie,
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Il rend mes pieds semblables à ceux des biches, et il me fait tenir debout sur mes hauteurs.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Il forme mes mains au combat, et mes bras tendent l'arc d'airain.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Tu m'as donné le bouclier de ton salut, et ta douleur me fait grandir.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Tu élargis mon pas au-dessous de moi, et mes pieds ne chancellent point.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Je poursuis mes ennemis et je les détruis; je ne reviens pas sans les avoir anéantis.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Je les anéantis, je les brise, ils ne se relèvent pas; ils tombent sous mes pieds.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Tu me ceins de force pour le combat, tu fais plier sous moi mes adversaires.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Mes ennemis, tu leur fais tourner le dos devant moi, comme à ceux qui me haïssent, pour que je les extermine.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ils regardent, et personne qui les sauve! Ils crient vers Yahweh, et il ne leur répond pas!
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Je les broie comme la poussière de la terre; comme la boue des rues, je les écrase, je les foule.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Tu me délivres des révoltes de mon peuple; tu me conserves pour chef des nations; un peuple que je ne connaissais pas m'est asservi.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Les fils de l'étranger me flattent, dès qu'ils ont entendu, ils m'obéissent.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Les fils de l'étranger sont défaillants, ils sortent tremblants de leurs forteresses.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Vive Yahweh et béni soit mon rocher! Dieu, mon rocher de refuge, qu'il soit exalté!
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Dieu, qui m'accorde des vengeances, qui fait descendre les peuples sous mes pieds,
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
qui me fait échapper à mes ennemis; toi qui m'élèves au-dessus de mes adversaires, qui me délivres de l'homme de violence.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
C'est pourquoi je te louerai parmi les nations, ô Yahweh, et je chanterai à la gloire de ton nom.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Il accorde de glorieuses délivrances à son roi, il fait miséricorde à son oint, à David et à sa postérité pour toujours.

< 2 Samweli 22 >