< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Forsothe Dauid spak to the Lord the wordis of this song, in the dai in which the Lord delyuerede hym fro the hond of alle hise enemyes, and fro the hond of Saul.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
And Dauid seide, The Lord is my stoon, and my strengthe, and my sauyour;
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
my God, my stronge, I schal hope in to hym; my scheeld, and the horn of myn helthe, `my reisere, and my refuyt; my sauyour, thou schalt delyuere me fro wickidnesse.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Y schal inwardly clepe the Lord worthi to be preisid; and Y schal be saaf fro myn enemyes.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
For the sorewis of deeth cumpasside me; the strondis of Belial maden me aferd.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
The coordis of helle cumpassiden me; the snaris of deeth camen bifor me. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
In tribulacioun Y schal clepe, `that is, Y clepide thee, Lord, and Y schal crie to my God; and he herd fro his holi temple my vois, and my crye schal come to hise eeris.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
The erthe was mouyd, and tremblide; the foundementis of hillis weren smytun and schakun togidere, for the Lord was wrooth to hem.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Smoke stiede fro hise nosethirlis, and fier of his mouth schal deuoure; colis weren kyndlid of it.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
And he bowide heuenes, and cam doun; and myist vndur hise feet.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
And he stiede on cherubyn, and fliy; and he slood on the pennys of wynd.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
He puttide derknessis hidyng place in his cumpas, and riddlide watris fro the cloudis of heuenes;
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
for briytnesse in his siyt colis of fier weren kyndelid.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
The Lord schal thundur fro heuene; and hiy God schal yyue his vois.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
He sente hise arowis, and scateride hem; he sente leitis, and wastide hem.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
And the schedyngis out of the see apperiden, and the foundementis of the world weren schewid; fro the blamyng of the Lord, fro the brething of the spirit of his strong veniaunce.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He sente fro heuene, and took me; and drow me out of manye watris.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He delyuerede me fro my myytiest enemy, and fro hem that hatiden me; for thei weren strongere than Y.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Thei camen bifore me in the dai of my turmentyng; and the Lord was maad my stidfastnesse.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
And he ledde me out in to largenesse, and he delyuerede me; for Y pleside hym.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
The Lord schal yelde to me vp my riytfulnesse; and he schal yelde to me vp, `ethir aftir, the clennesse of myn hondis.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For Y kepte the weies of the Lord; and Y dide not wickidli fro my God.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For alle hise domes weren in my siyt; and Y dide not awei fro me hise heestis.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
And Y schal be perfit with hym; and Y schal kepe me fro my wickidnesse.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
And the Lord schal restore to me vpe my riytfulnesse; and vp the clennesse of myn hondis in the siyt of hise iyen.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
With the hooli thou schalt be hooli, and with the stronge, `that is, to suffre aduersitees pacientli, thou schalt be perfit;
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
and with a chosun man `to blis thou schalt be chosun, and with a weiward man thou schalt be maad weiward, `that is, in yeldynge iustli peyne to hym vpe his weiwardnesse.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
And thou schalt make saaf a pore puple; and with thin iyen thou schalt make lowe hem that ben hiye.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For thou, Lord, art my lanterne, and thou, Lord, schalt liytne my derknessis.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For Y gird, `that is, maad redi to batel, schal renne in thee, `that is, in thi vertu; and in my God Y schal `scippe ouer the wal.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
`God his weie is `with out wem; the speche of the Lord is examynyd bi fier, `that is, is pure and clene as metal preuyd in the furneys; he is a scheeld of alle men hopynge in hym.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who is God, outakun the Lord; and who is strong, outakun oure God?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
God, that hath gird me with strengthe, and hath maad pleyn my perfit weie;
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
and he made euene my feet with hertis, and settide me on myn hiye thingis;
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
and he tauyte myn hondis to batel, and made myn armes as a brasun bouwe.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Thou hast youe to me the sheeld of thin heelthe; and my myldenesse multipliede me.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Thou schalt alarge my steppis vndur me; and myn heelis schulen not faile.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Y schal pursue myn enemyes, and Y schal al to-breke hem; and Y schal not turne ayen, til Y waste hem.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Y schal waste hem, and Y schal breke, that thei rise not; thei schulen falle vndur my feet.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Thou hast gird me with strengthe to batel; thou hast bowid vnder me hem that ayenstoden me.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Thou hast youe myn enemyes abac to me, men hatynge me; and Y schal distrie hem.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Thei schulen crye, `that is, to ydols ether to mennus help, and noon schal be that schal saue; `thei schulen crie to the Lord, and he schal not here hem.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Y schal do awei hem as the dust of erthe; Y schal `powne hem, and Y schal do awei as the clei of stretis.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Thou schalt saue me fro ayenseiyngis of my puple; thou schalt kepe me in to the heed of folkis; the puple, whom Y knowe not, schal serue me.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Alien sones schulen ayenstonde me; bi heryng of eere thei schulen obeie to me.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Alien sones fletiden awei; and thei schulen be drawun togidere in her angwischis.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
The Lord lyueth, and my God is blessid; and the stronge God of myn helthe schal be enhaunsid.
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
God, that yyuest veniauncis to me; and hast cast doun puplis vndur me.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Which ledist me out fro myn enemyes, and reisist me fro men ayenstondinge me; thou schalt deliuere me fro the wickid man.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Therfor, Lord, Y schal knowleche to thee in hethene men; and Y schal synge to thi name.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
And he magnyfieth the helthis of his kyng; and doith mercyes to his crist Dauid, and to his seed til in to withouten ende.

< 2 Samweli 22 >