< 2 Samweli 22 >
1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
After Yahweh had rescued David from Saul and his other enemies, David sang a song to Yahweh.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
[This is what] he sang: Yahweh, you are like a [huge overhanging] rock [under which I can hide] [MET]; you are like my fortress, and you rescue me.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Yahweh, you protect me; you are like a shield; you are the powerful one [MET] who saves me; you are like a place where I (find refuge/am safe). You save me from those who act violently toward me.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
I call out to you, Yahweh; you deserve to be praised, and you rescue me from my enemies.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
“almost died [PRS]; it was like [MET] a huge wave had crashed over me, and almost destroyed me like a flood.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
I thought that I would die; it was as though death wrapped ropes around me; it was as though I was in a trap where I would surely die. [PRS, MET] (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
But when I was (very distressed/in great trouble), I called out to you, Yahweh; I cried out to you, my God. And from your temple you heard me; you listened when I called to you to help me.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
“Then [it was as though] the earth quaked and shook; [it was as though] the foundations that ([held up/supported]) the sky trembled, because you were angry.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
[It was as though] smoke poured out of your nostrils and burning coals and fire that burns everything came out of your mouth.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
You tore open the sky and came down; there was a thick dark [cloud] under your feet.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
You rode [through the sky] on a winged creature; the wind enabled you to travel [swiftly] [MET], like a bird.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
The darkness surrounded you, like a blanket; thick clouds that were full of water also surrounded you.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Out of the lightning in front of you fire from burning coals flamed.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Then, Yahweh, you spoke like thunder from the sky; it was your voice, God, you who are greater than all other gods, that was heard.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
When you sent flashes of lightning, [it was as though] [MET] you shot your arrows and scattered your enemies.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Then the bottom of the ocean was uncovered; the foundations of the world could be seen when you rebuked [your enemies] with a snort from your nostrils.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
“Yahweh, you reached down from heaven and lifted me up; you pulled me up from the deep water.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
You rescued me from my strong enemies, from those who hated me; [I could not defeat them because] they were very strong.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They attacked me when I was experiencing troubles/difficulties, but Yahweh, you protected me.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
You brought me to a place where I was safe; you rescued me because you were pleased with me.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
“Yahweh, you rewarded me because I do what is right; you did good things for me because I (was innocent/had not done things that are wrong).
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Yahweh, I have obeyed your laws; I have not turned away from you, my God.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
All of your regulations were in my mind, and I did not turn away from [obeying] all your statutes.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
You know that I have not done anything that is evil; I have kept myself from doing things for which I should be punished.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
So you have rewarded me in return for my doing what is right, because [you know that] I (am innocent of doing/have not done) wrong things.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
“Yahweh, you are faithful/loyal to those who always trust in you; you always do what is good to those whose behavior is always good.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
You act sincerely toward those whose inner beings are pure, but you are hostile to those who are perverse/wicked.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
You rescue those who are humble, but you watch [MTY] those who are proud and humiliate them.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Yahweh, you are [like] [MET] a lamp that causes it to become light when I am in the dark.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
With your strength/help I can run through a line of enemy soldiers and I can climb over the wall [that surrounds their city].
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
“My God whom I worship, everything that you do is perfect; you always do what you promise that you will do. You are like a shield [MET] to all those who request you to protect them.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Yahweh, you are [RHQ] the only one who is God; only you are like a huge rock [MET] [under which we are protected/safe].
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
God, you [whom I worship] are a strong refuge for me; you keep me safe on the roads that I [walk on].
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
[When I walk] in the mountains, you enable me to walk safely, without stumbling [MET] like a deer runs.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
You teach me [how to fight] in a battle in order that I can shoot arrows well from a very strong bow.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
[It is as though] [MET] you have given me a shield by which you have saved/rescued me, and you have answered my prayers and caused me to become famous/great.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
You have not allowed [my enemies] to capture me [IDM], and I have not fallen down [during battles].
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
“pursued my enemies and defeated them; I did not stop [fighting them] until they were all killed.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
I struck them down; I stabbed them with my sword; they fell down at my feet and did not stand up again.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
You have given me strength for fighting battles and caused those who were attacking me to fall down, and I trampled on them.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
You caused my enemies to turn and run away from me; I destroyed those who hated me.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They (looked for/wanted) someone to rescue them, but no one did. They cried out to you, Yahweh, [for help, ] but you did not answer them.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
I crushed them, and as a result they became like [SIM] tiny particles of dust. I trampled them, and they became like [SIM] mud in the streets.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
“You rescued me from those who tried to rebel [against me], and you appointed me to rule many nations; people whom I did not know previously are now (under my authority/my slaves).
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Foreigners humbly bowed down in front of me; as soon as they heard about me, they obeyed me.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
They became afraid, and they came to me, trembling, from the places where they were hiding.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
“Yahweh, you are alive! I praise you! You are like [MET] a [huge overhanging] rock under which I am safe/protected! You are the one who rescues me [MET]. Everyone should exalt/honor/praise you.
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
You enable me to conquer my enemies; you cause people of [other] nations to be (under my authority/my slaves).
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
You delivered me from my enemies; you caused me to be honored more than they were; you rescued me from men who [always] acted violently.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Because of all that, I exalt you among many people-groups and I sing to praise you.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
You enable me, whom you appointed to be king, to powerfully conquer [my enemies]; you faithfully love me, David, and you will love my descendants forever.