< 2 Samweli 22 >
1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
and to speak: speak David to/for LORD [obj] word [the] song [the] this in/on/with day to rescue LORD [obj] him from palm all enemy his and from palm Saul
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
and to say LORD crag my and fortress my and to escape me to/for me
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
God rock my to seek refuge in/on/with him shield my and horn salvation my high refuge my and refuge my to save me from violence to save me
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
to boast: praise to call: call to LORD and from enemy my to save
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
for to surround me wave death torrent: river Belial: destruction to terrify me
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
cord hell: Sheol to turn: surround me to meet me snare death (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
in/on/with distress to/for me to call: call to LORD and to(wards) God my to call: call to and to hear: hear from temple his voice my and cry my in/on/with ear his
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
(and to shake *Q(K)*) and to shake [the] land: country/planet foundation [the] heaven to tremble and to shake for to be incensed to/for him
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
to ascend: rise smoke in/on/with face: nose his and fire from lip his to eat coal to burn: burn from him
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
and to stretch heaven and to go down and cloud underneath: under foot his
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
and to ride upon cherub and to fly and to see: see upon wing spirit: breath
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
and to set: make darkness around him booth collection water cloud cloud
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
from brightness before him to burn: burn coal fire
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
to thunder from heaven LORD and Most High to give: cry out voice his
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
and to send: depart arrow and to scatter them lightning (and to confuse *Q(K)*)
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
and to see: see channel sea to reveal: uncover foundation world in/on/with rebuke LORD from breath spirit: breath face: nose his
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
to send: depart from height to take: take me to draw me from water many
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
to rescue me from enemy my strong from to hate me for to strengthen from me
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
to meet me in/on/with day calamity my and to be LORD support to/for me
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
and to come out: send to/for broad [obj] me to rescue me for to delight in in/on/with me
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
to wean me LORD like/as righteousness my like/as cleanness hand my to return: pay to/for me
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
for to keep: obey way: conduct LORD and not be wicked from God my
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
for all (justice: judgement his *Q(K)*) to/for before me and statute his not to turn aside: turn aside from her
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
and to be unblemished: blameless to/for him and to keep: guard [emph?] from iniquity: crime my
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
and to return: pay LORD to/for me like/as righteousness my like/as cleanness my to/for before eye his
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
with pious be kind with mighty man unblemished: blameless to finish
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
with to purify to purify and with twisted to twist
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
and [obj] people afflicted to save and eye your upon to exalt to abase
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
for you(m. s.) lamp my LORD and LORD to shine darkness my
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
for in/on/with you to run: run band in/on/with God my to leap wall
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
[the] God unblemished way: conduct his word LORD to refine shield he/she/it to/for all [the] to seek refuge in/on/with him
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
for who? God from beside LORD and who? rock from beside God our
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
[the] God security my strength and to free unblemished: blameless (way: conduct my *Q(K)*)
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
to set (foot my *Q(K)*) like/as doe and upon high place my to stand: stand me
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
to learn: teach hand my to/for battle and to descend bow bronze arm my
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
and to give: give to/for me shield salvation your and humility your to multiply me
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
to enlarge step my underneath: under me and not to slip ankle my
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
to pursue enemy my and to destroy them and not to return: return till to end: destroy them
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
and to end: destroy them and to wound them and not to arise: rise [emph?] and to fall: fall underneath: under foot my
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
and to gird me strength to/for battle to bow to arise: attack me underneath: under me
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
and enemy my to give: make to/for me neck to hate me and to destroy them
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
to gaze and nothing to save to(wards) LORD and not to answer them
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
and to beat them like/as dust land: soil like/as mud outside to crush them to beat them
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
and to escape me from strife people my to keep: guard me to/for head: leader nation people not to know to serve: minister me
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
son: type of foreign to deceive to/for me to/for to hear: hear ear: hearing to hear: obey to/for me
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
son: type of foreign to wither and to gird from perimeter their
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
alive LORD and to bless rock my and to exalt God rock salvation my
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
[the] God [the] to give: give vengeance to/for me and to go down people underneath: under me
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
and to come out: send me from enemy my and from to arise: rise me to exalt me from man violence to rescue me
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
upon so to give thanks you LORD in/on/with nation and to/for name your to sing
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
(tower *Q(K)*) salvation king his and to make: do kindness to/for anointed his to/for David and to/for seed: children his till forever: enduring