< 2 Samweli 22 >
1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
And he spoke David to Yahweh [the] words of the song this on [the] day [when] he delivered Yahweh him from [the] hand of all enemies his and from [the] hand of Saul.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
And he said Yahweh [is] rock my and stronghold my and deliverer my to me.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
O God of rock my [whom] I take refuge in him shield my and [the] horn of salvation my refuge my and place of escape my O deliverer my from violence you deliver me.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
[the one] to be praised I called out to Yahweh and from enemies my I am delivered.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
For they surrounded me [the] breakers of death torrents of worthlessness they overwhelmed me.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
[the] cords of Sheol they surrounded me they confronted me [the] snares of death. (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
When it was distress to me I called out to Yahweh and to God my I called out and he heard from temple his voice my and cry for help my [was] in ears his.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
(And it shook back and forth *Q(K)*) and it quaked the earth [the] foundations of the heavens they trembled and they shook back and forth for it burned to him.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
It went up smoke in nose his and fire from mouth his it consumed coals they burned from him.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
And he bowed [the] heavens and he came down and thick darkness [was] under feet his.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
And he rode on a cherub and he flew and he appeared on [the] wings of [the] wind.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
And he put darkness around him shelters a sieve of waters dark clouds of clouds.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
From [the] brightness before him they burned coals of fire.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
He thundered from heaven Yahweh and [the] Most High he gave voice his.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
And he sent arrows and he scattered them [with] lightning (and he routed [them]. *Q(K)*)
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
And they appeared [the] channels of [the] sea they were uncovered [the] foundations of [the] world at [the] rebuke of Yahweh from [the] breathing of [the] breath of nose his.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He stretched out from a high place he took hold of me he drew me from waters many.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He rescued me from enemy my mighty from [those who] hate me for they were [too] strong for me.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They confronted me in [the] day of calamity my and he was Yahweh a support of me.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
And he brought out to roomy place me he rescued me for he delighted in me.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
He dealt with me Yahweh according to righteousness my according to [the] cleanness of hands my he repaid to me.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For I have kept [the] ways of Yahweh and not I have acted wickedly from God my.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For all (judgments his *Q(K)*) [are] to before me and statutes his not I turn aside from it.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
And I was blameless to him and I kept myself! from iniquity my.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
And he repaid Yahweh to me according to righteousness my according to cleanness my to before eyes his.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
With a faithful [person] you show yourself faithful with a mighty [man] blameless you show yourself blameless.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
With [one who] purifies himself you show yourself pure and with a perverse [person] you show yourself twisted.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
And a people afflicted you save and eyes your [are] on haughty [people] you bring [them] low.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For you [are] lamp my O Yahweh and Yahweh he lightens darkness my.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For by you I run a marauding band by God my I leap over a wall.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
God [is] blameless way his [the] word of Yahweh [is] refined [is] a shield he for all those [who] seek refuge in him.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who? [is] God except Yahweh and who? [is] a rock except God our.
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
God [is] place of refuge my strength and he set free a blameless [person] (way my. *Q(K)*)
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
[he is] making (Feet my *Q(K)*) like does and on high places my he makes stand firm me.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
[he has] trained Hands my for battle and it will stretch a bow of bronze arms my.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
And you gave to me [the] shield of salvation your and answering your you make great me.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
You enlarge step[s] my under me and not they slip ankles my.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Let me pursue enemies my and I destroyed them and not I returned until brought to an end them.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
And I brought to an end them and I shattered them and not they will rise! and they fell under feet my.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
And you have girded me strength for battle you make bow down [those who] rise against me under me.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
And enemies my you have given to me a neck [those who] hate me and I destroyed them.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They looked and there not [was] a deliverer to Yahweh and not he answered them.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
And I beat fine them like [the] dust of [the] earth like [the] mud of [the] streets I pulverized them I beat out them.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
And you rescued me from [the] strifes of people my you kept me to [the] head of [the] nations a people [whom] not I knew they served me.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Sons of foreignness they cringed to me to hear an ear they became obedient to me.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Sons of foreignness they withered and they may girdethemselves from strongholds their.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
[is] living Yahweh and [be] blessed rock my and may he be exalted [the] God of [the] rock of salvation my.
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
God [is] the [one who] gives vengeance to me and [is] bringing down peoples under me.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
And [is] bringing out me from enemies my and from [those who] rise against me you lift up me from a man of violence you rescue me.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
There-fore I will give thanks you O Yahweh among the nations and to name your I will sing praise.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
([the] tower *Q(K)*) Of [the] salvation of king his and [who] does covenant loyalty to anointed his to David and to offspring his until perpetuity.