< 2 Samweli 22 >
1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
And David spake unto Yahweh, the words of this song, in the day when Yahweh had rescued him, out of the hand of all his enemies, and out of the hand of Saul;
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
and he said, —Yahweh, was my mountain crag and my stronghold, and my deliverer—mine;
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
My God, was my rock, I sought refuge in him, —My shield, and my horn of salvation, my high tower, and my refuge, My Saviour! from violence, thou didst save me.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
As one worthy to be praised, called I on Yahweh, —And, from my foes, was I saved.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
When the breakers of death had encompassed me, —the torrents of perdition, made me afraid, —
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
the meshes of hades, had surrounded me, —the snares of death had confronted me, (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
In my distress, called I on Yahweh, Yea, unto my God, did I call, —and he hearkened, out of his temple, unto my voice, and, my cry for help, was in his ears!
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Then did the earth shake and quake, the foundations of the heavens, were deeply moved, —yea they did shake, because he was angry,
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
There went up a smoke in his nostrils, and, a fire out of his mouth, devoured, —live coals, were kindled from it:
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Then he stretched out the heavens, and came down, —and, thick gloom, was under his feet;
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Then he rode on a cherub, and flew, —and was seen on the wings of the wind;
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
And made of the darkness around him, pavilions, —gathering of waters, clouds of vapours.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Out of the brightness before him, were kindled live coals of fire;
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Thunder from the heavens, did Yahweh give forth, —yea, the Highest, uttered his voice;
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
And he sent forth arrows, and scattered them, —lightning, and confused them;
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Then appeared the channels of the sea, were uncovered the foundations of the world, —at the rebuke of Yahweh, the blast of the breath of his nostrils;
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He sent from on high, he took me, —he drew me out of many waters;
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He rescued me from my foe, in his might, —from them who hated me, because they were too strong for me:
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They confronted me, in the day of my necessity, —then became Yahweh my stay:
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
And brought out, into a large place, even me, —he delivered me, because he delighted in me:
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Yahweh rewarded me, according to my righteousness—according to the cleanness of my hands, he repaid me:
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For I had kept the ways of Yahweh, —and not broken away from my God;
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For, all his regulations, were before me, —and, as for his statutes, I turned not from them.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
So became I blameless towards him, —and kept myself from mine iniquity:
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Yahweh therefore repaid me, according to my righteousness, —according to my pureness before his eyes.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
With the loving, thou didst show thyself loving, —with the blameless hero, thou didst show thyself blameless;
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
With the pure, thou didst show thyself pure, —but, with the perverse, thou didst shew thyself ready to contend:
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
And, a patient people, thou didst save, —but, thine eyes, were on the lofty—thou layedst them low;
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For, thou, wast my lamp, O Yahweh, —and, Yahweh, enlightened my darkness;
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For, by thee, I ran through a troop, —by my God, I leapt over a wall.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
As for God, blameless is his way, —the speech of Yahweh, hath been proved, a shield, he is to all who seek refuge in him.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who is a GOD, save Yahweh? and who a Rock, save our God?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
GOD, is my fortress of strength, —and shewed to the blameless his way;
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Planting my feet like the hinds’, —yea, on my high places, he caused me to stand;
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Teaching my hands, to war, —so that a bow of bronze was bent by mine arms;
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Thus didst thou grant me, as a shield, thy salvation, —and, thy condescension, made me great.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Thou didst widen my stepping-places, under me, —so that mine ankles faltered not:
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
I pursued my foes, and destroyed them, —and returned not, till they were consumed;
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
So I consumed them, and crushed them, and they rose not again, —thus fell they under my feet:
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Thus didst thou gird me with strength, for the battle, —thou subduedst mine assailants under me:
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
And, as for my foes, thou didst give me their neck, —yea, them who hated me, that I might destroy them:
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They cried out, but there was none to save, —unto Yahweh, but he answered them not.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Then did I beat them in pieces, like the dust of the earth, —like the clay of the lanes, did I crush them, stamp them down.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Thus didst thou rescue me from the contentions of my people, didst keep me to be the head of nations: —a people whom I had not known, served me;
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
The sons of the foreigner, came cringing unto me, —at the hearing of the ear, they submitted to me, —
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
The sons of the foreigner, were disheartened, and came quaking, out of their fortresses.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Yahweh liveth, and blessed be my rock, —and exalted be the God (of the rock) of my salvation: —
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
The GOD who hath avenged me, and brought down peoples under me;
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
And brought me forth from among my foes, —yea, from mine assailants, hast thou set me on high, from the man of violence, hast thou delivered me.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
For this cause, will I praise thee, O Yahweh, among the nations, —and, to thy name, will I touch the strings: —
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Who hath made great the victories of his King, —and shown lovingkindness to his Anointed One, to David and to his Seed, unto times age-abiding.