< 2 Samweli 22 >
1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
And Dauid spake the woordes of this song vnto the Lord, what time the Lord had deliuered him out of the handes of all his enemies, and out of the hand of Saul.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
And he sayd, The Lord is my rocke and my fortresse, and he that deliuereth mee.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
God is my strength, in him will I trust: my shielde, and the horne of my saluation, my hie tower and my refuge: my Sauiour, thou hast saued me from violence.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
I will call on the Lord, who is worthy to be praysed: so shall I be safe from mine enemies.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
For the pangs of death haue compassed me: the floods of vngodlinesse haue made mee afrayd.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
The sorowes of the graue compassed mee about: the snares of death ouertooke mee. (Sheol )
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
But in my tribulation did I call vpon the Lord, and crie to my God, and he did heare my voyce out of his temple, and my crie did enter into his eares.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Then the earth trembled and quaked: the foundations of the heauens mooued and shooke, because he was angrie.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Smoke went out at his nostrels, and consuming fire out of his mouth: coles were kindled thereat.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
He bowed the heauens also, and came downe, and darkenes was vnder his feete.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
And he rode vpon Cherub and did flie, and hee was seene vpon the winges of the winde.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
And hee made darkenesse a Tabernacle round about him, euen the gatherings of waters, and the cloudes of the ayre.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
At the brightnesse of his presence the coles of fire were kindled.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
The Lord thundred from heauen, and the most hie gaue his voyce.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
He shot arrowes also, and scattered them: to wit, lightning, and destroyed them.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
The chanels also of the sea appeared, euen the foundations of the worlde were discouered by the rebuking of the Lord, and at the blast of the breath of his nostrels.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He sent from aboue, and tooke me: hee drewe me out of many waters.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He deliuered me from my strong enemie, and from them that hated me: for they were too strong for me.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They preuented me in the day of my calamitie, but the Lord was my stay,
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
And brought me foorth into a large place: he deliuered me, because he fauoured me.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
The Lord rewarded me according to my righteousnesse: according to the purenesse of mine handes he recompensed me.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For I kept the wayes of the Lord, and did not wickedly against my God.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For all his lawes were before me, and his statutes: I did not depart therefrom.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
I was vpright also towarde him, and haue kept me from my wickednesse.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Therefore the Lord did reward me according to my righteousnesse, according to my purenesse before his eyes.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
With the godly thou wilt shewe thy selfe godly: with the vpright man thou wilt shew thy selfe vpright.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
With the pure thou wilt shewe thy selfe pure, and with the frowarde thou wilt shew thy selfe frowarde.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Thus thou wilt saue the poore people: but thine eyes are vpon the hautie to humble them.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Surely thou art my light, O Lord: and the Lord will lighten my darkenes.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For by thee haue I broken through an hoste, and by my God haue I leaped ouer a wall.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
The way of God is vncorrupt: the word of the Lord is tryed in the fire: he is a shield to all that trust in him.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who is God besides the Lord? and who is mightie, saue our God?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
God is my strength in battel, and maketh my way vpright.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
He maketh my feete like hindes feete, and hath set me vpon mine hie places.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
He teacheth mine handes to fight, so that a bowe of brasse is broken with mine armes.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Thou hast also giuen me the shield of thy saluation, and thy louing kindnesse hath caused me to increase.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Thou hast inlarged my steppes vnder me, and mine heeles haue not slid.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
I haue pursued mine enemies and destroyed them, and haue not turned againe vntill I had consumed them.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Yea, I haue consumed them and thrust them through, and they shall not arise, but shall fall vnder my feete.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
For thou hast girded me with power to battell, and them that arose against me, hast thou subdued vnder me.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
And thou hast giuen me the neckes of mine enemies, that I might destroy them that hate me.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They looked about, but there was none to saue them, euen vnto the Lord, but he answered them not.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Then did I beate them as small as the dust of the earth: I did treade them flat as the clay of the streete, and did spread them abroad.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Thou hast also deliuered me from the contentions of my people: thou hast preserued me to be the head ouer nations: the people which I knewe not, doe serue me.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Strangers shalbe in subiection to me: assoone as they heare, they shall obey me.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Strangers shall shrinke away, and feare in their priuie chambers.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Let the Lord liue, and blessed be my strength: and God, euen the force of my saluation be exalted.
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
It is God that giueth me power to reuenge me, and subdue the people vnder me,
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
And rescueth me from mine enemies: (thou also hast lift me vp from them that rose against me, thou hast deliuered me from the cruell man.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Therefore I will praise thee, O Lord amog the nations, and will sing vnto thy Name)
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
He is the tower of saluation for his King, and sheweth mercie to his anointed, euen to Dauid, and to his seede for euer.