< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
And David spoke to Jehovah the words of this song in the day that Jehovah had delivered him out of the hand of all his enemies, and out of the hand of Saul.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
And he said, Jehovah is my rock, and my fortress, and my deliverer;
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
God is my rock, in him will I trust — My shield, and the horn of my salvation, My high tower, and my refuge, My saviour: thou wilt save me from violence.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
I will call upon Jehovah, who is to be praised; So shall I be saved from mine enemies.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
For the waves of death encompassed me, Torrents of Belial made me afraid.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
The bands of Sheol surrounded me; The cords of death encountered me; (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
In my distress I called upon Jehovah, And I cried to my God; And he heard my voice out of his temple, And my cry [came] into his ears.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Then the earth shook, and quaked; The foundations of the heavens trembled And shook because he was wroth.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
There went up a smoke out of his nostrils, And fire out of his mouth devoured: Coals burned forth from it.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
And he bowed the heavens, and came down; And darkness was under his feet.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
And he rode upon a cherub, and did fly; And he was seen upon the wings of the wind.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
And he made darkness round about him a tent, Gatherings of waters, thick clouds of the skies.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
From the brightness before him Burned forth coals of fire.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Jehovah thundered from the heavens, And the Most High uttered his voice.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
And he sent arrows, and scattered [mine enemies]; Lightning, and discomfited them.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
And the beds of the sea were seen, The foundations of the world were uncovered At the rebuke of Jehovah, At the blast of the breath of his nostrils.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He reached forth from above, he took me, He drew me out of great waters;
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He delivered me from my strong enemy, From them that hated me; For they were mightier than I.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They encountered me in the day of my calamity; But Jehovah was my stay.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
And he brought me forth into a large place; He delivered me, because he delighted in me.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Jehovah hath rewarded me according to my righteousness, According to the cleanness of my hands hath he recompensed me.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For I have kept the ways of Jehovah, And have not wickedly departed from my God.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For all his ordinances were before me, And his statutes, I did not depart from them,
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
And I was upright before him, And kept myself from mine iniquity.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
And Jehovah hath recompensed me according to my righteousness, According to my cleanness in his sight.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
With the gracious thou dost shew thyself gracious; With the upright man thou dost shew thyself upright;
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
With the pure thou dost shew thyself pure; And with the perverse thou dost shew thyself contrary.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
And the afflicted people thou dost save; And thine eyes are upon the haughty, [whom] thou bringest down.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For thou art my lamp, Jehovah; And Jehovah enlighteneth my darkness.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For by thee I have run through a troop; By my God have I leaped over a wall.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
As for God, his way is perfect; The word of Jehovah is tried: He is a shield to all that trust in him.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who is God, save Jehovah? And who is a rock, save our God?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
God is my strong fortress, And he maketh my way perfectly smooth.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
He maketh my feet like hinds' [feet], And setteth me upon my high places.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
He teacheth my hands to war, And mine arms bend a bow of brass.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
And thou didst give me the shield of thy salvation, And thy condescending gentleness hath made me great.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Thou enlargedst my steps under me; And mine ankles did not slip.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
I pursued mine enemies, and destroyed them, And I turned not again till they were consumed.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
And I have consumed them and have crushed them, and they rose not again; Yea, they fell under my feet.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
And thou girdedst me with strength to battle: Thou didst subdue under me those that rose up against me.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
And mine enemies didst thou make to turn their backs unto me, And those that hated me I destroyed.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They looked, and there was none to save — Unto Jehovah, and he answered them not.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
And I did beat them small as the dust of the earth, I trod them as the mire of the streets; I stamped upon them.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
And thou hast delivered me from the strivings of my people, Thou hast kept me to be head of the nations: A people I knew not doth serve me:
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Strangers come cringing unto me: At the hearing of the ear, they obey me.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Strangers have faded away, And they come trembling forth from their close places.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Jehovah liveth; and blessed be my rock; And exalted be the God, the rock of my salvation,
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
The God who hath avenged me, And hath brought the peoples under me.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
He brought me forth from mine enemies: Yea, thou hast lifted me up above them that rose up against me; From the man of violence hast thou delivered me.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Therefore will I give thanks to thee, Jehovah, among the nations, And will sing psalms to thy name.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
[It is he] who giveth great deliverances to his king, And sheweth loving-kindness to his anointed, To David, and to his seed for evermore.

< 2 Samweli 22 >