< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
Mluvil pak David Hospodinu slova písně této v ten den, když ho vysvobodil Hospodin z ruky všech nepřátel jeho, i z ruky Saulovy.
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
A řekl: Hospodin skála má a hrad můj, i vysvoboditel můj se mnou.
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Bůh skála má, doufati budu v něho; štít můj a roh spasení mého, vyvýšení mé a útočiště mé, spasitel můj, kterýž od násilí vysvobozuje mne.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Chvály hodného vzýval jsem Hospodina, a od nepřátel svých vysvobozen jsem.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Nebo obklíčily mne byly úzkosti smrti, a proudové bezbožných předěsili mne.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Bolesti smrtelné obstoupily mne, a osídla smrti zachvátila mne. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
V úzkosti své vzýval jsem Hospodina, a k Bohu svému volal jsem, i vyslyšel z chrámu svého hlas můj, a křik můj přišel v uši jeho.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Tedy pohnula se a zatřásla země, základové nebes pohnuli se, a třásli se pro rozhněvání jeho.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Dým vycházel z chřípí jeho, a oheň zžírající z úst jeho, od něhož se uhlí roznítilo.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Nakloniv nebes, sstoupil, a mrákota byla pod nohami jeho.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
I vsedl na cherubín a letěl, a spatřín jest na peří větrovém.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Položil temnosti vůkol sebe jako stany, shrnutí vod, oblaky husté.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Od blesku oblíčeje jeho rozpálilo se uhlí řeřavé.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Hřímal s nebes Hospodin, a Nejvyšší vydal zvuk svůj.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Vystřelil i střely, kterýmiž je rozptýlil, a blýskání, jímž je porazil.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
I ukázaly se hlubiny mořské, a odkryti jsou základové okršlku, pro zůřivé kárání Hospodinovo, pro dmýchání větru chřípí jeho.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Poslav s výsosti, přijal mne, vytáhl mne z vod velikých.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Vysvobodil mne od nepřítele mého silného, od těch, kteříž mne nenáviděli, ačkoli silnější mne byli.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Předstihli mne v den trápení mého, ale Hospodin byl mi podpora.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Kterýž vyvedl mne na prostranství, vysvobodil mne, nebo sobě oblíbil mne.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Odplatil mi Hospodin podlé spravedlnosti mé, podlé čistoty rukou mých odplatil mi.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Nebo jsem ostříhal cest Hospodinových, aniž jsem se bezbožně strhl Boha svého.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Všickni zajisté soudové jeho jsou před oblíčejem mým, aniž jsem od kterých ustanovení jeho odstoupil.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
A tak byv dokonalý před ním, šetřil jsem, abych se nedopustil nepravosti.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Protož odplatil mi Hospodin podlé spravedlnosti mé, vedlé čistoty mé před očima jeho.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Ty, Pane, s milosrdným milosrdně nakládáš, a k upřímému upřímě se máš.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
K sprostnému sprostně se ukazuješ, a s převráceným převráceně zacházíš.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Lid pak ssoužený vysvobozuješ, ale před vysokomyslnými oči své sklopuješ.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Ty zajisté jsi svíce má, ó Hospodine. Hospodin jistě osvěcuje temnosti mé.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Nebo v tobě proběhl jsem vojska, v Bohu svém přeskočil jsem zed.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Toho Boha silného cesta jest dokonalá, výmluvnosti Hospodinovy přečištěné; onť jest štít všech, kteříž doufají v něho.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Nebo kdo jest Bohem kromě Hospodina? A kdo jest skalou kromě Boha našeho?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Bůh jest síla má i vojska mého, onť působí volnou cestu mou.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Činí nohy mé jako laní, a na vysokých místech mých postavuje mne.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Cvičí ruce mé k boji, tak že lámi lučiště ocelivá rukama svýma.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Nebo dal mi štít spasení svého, a dobrotivost jeho zvelebila mne.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Rozšířil kroky mé pode mnou, aby se nepodvrtly nohy mé.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Honil jsem nepřátely své a zahladil jsem je, aniž jsem se navrátil, dokudž jsem jich nevyplénil.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Docela jsem je vyhubil a sprobodal jsem je, tak že nepovstanou; i padli pod nohy mé.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Ty zajisté, Bože, přepásals mne udatností k boji, porazils pode mne ty, kteříž povstávají proti mně.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Nýbrž dals mi šíji nepřátel mých, těch, kteříž v nenávisti měli mne, a vyplénil jsem je.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ohlédali se, ale nebyl, kdo by vysvobodil, k Hospodinu, ale nevyslyšel jich.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
I potřel jsem je jako prach země, jako bláto na ulicích potlačil a rozptýlil jsem je.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
Ty jsi mne vytrhl z různic lidu mého, zachovals mne, abych byl za hlavu národům; lid neznámý mně sloužil.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Cizozemci lhali mi, a jakž zaslechli, uposlechli mne.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Cizozemci svadli, a třásli se i v ohradách svých.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Živť jest Hospodin, a požehnaná skála má; protož ať jest vyvyšován Bůh, skála spasení mého,
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
Bůh silný, kterýž dává mi pomsty a podmaňuje mi lidi.
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Vyvodíš mne z prostřed nepřátel mých, a nad povstávajícími proti mně vyvyšuješ mne, člověka nepravého mne zbavuješ.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
Protož chváliti tě budu, Hospodine, mezi národy, a jménu tvému žalmy zpívati budu.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Onť jest hrad jistého spasení krále svého, a ten, kterýž činí milosrdenství pomazanému svému Davidovi, i semeni jeho až na věky.

< 2 Samweli 22 >