< 2 Samweli 21 >

1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
در دوران سلطنت داوود، قحطی شد و این قحطی سه سال طول کشید. داوود به درگاه خداوند دعا کرد و خداوند فرمود: «این قحطی به سبب خطای شائول و خاندان اوست، زیرا آنها جبعونی‌ها را کشتند.»
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
پس داوود جبعونی‌ها را احضار نمود. (آنها جزو قوم اسرائیل نبودند، بلکه گروه کوچکی از اموری‌ها بودند. بنی‌اسرائیل قسم خورده بودند که آنها را نکشند؛ اما شائول به دلیل غیرتی که برای اسرائیل و یهودا داشت سعی کرد آنها را نابود کند.)
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
داوود از ایشان پرسید: «چطور می‌توانم ظلمی را که در حق شما شده، جبران کنم تا شما قوم خداوند را برکت دهید؟»
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
آنها جواب دادند: «ما از خاندان شائول طلا و نقره نمی‌خواهیم. در ضمن راضی هم نیستیم که به خاطر ما کسی از اسرائیلی‌ها کشته شود.» داوود گفت: «شما هر چه بخواهید برایتان انجام می‌دهم.»
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
آنها گفتند: «هفت نفر از پسران شائول را به دست ما بدهید، یعنی پسران مردی را که می‌کوشید ما را از بین ببرد تا از ما کسی در اسرائیل باقی نماند. ما آنها را در حضور خداوند در جِبعه، شهر شائول که پادشاه برگزیدهٔ خداوند بود، به دار می‌آویزیم.» پادشاه گفت: «بسیار خوب، این کار را می‌کنم.»
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
داوود به خاطر عهد و پیمانی که در حضور خداوند با یوناتان بسته بود، پسر او مفیبوشت را که نوهٔ شائول بود به دست ایشان نداد.
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
ولی دو پسر شائول یعنی ارمونی و مفیبوشت را که مادرشان رصفه، دختر اَیه بود، به ایشان داد. همچنین پنج پسر میرب را هم که از دختر شائول، زن عدریئیل پسر برزلای محولاتی به دنیا آمده بودند، به دست آنها سپرد.
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
جبعونی‌ها آنها را روی کوه در حضور خداوند به دار آویختند. بدین ترتیب، این هفت نفر در آغاز فصل درو جو مردند.
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
سپس رصفه، کنیز شائول، پلاسی گرفت و آن را روی یک تخته سنگ نزدیک اجساد انداخت و تمام فصل درو در آنجا ماند تا نگذارد پرندگان در روز و درندگان در شب اجساد را بخورند.
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
وقتی داوود شنید که رصفه، دختر آیَه، مُتعۀ شائول چه کرده است،
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
ترتیبی داد که استخوانهای مردگان را دفن کنند. در ضمن از مردان یابیش جلعاد خواهش کرد استخوانهای شائول و پسرش یوناتان را برایش بیاورند. (وقتی شائول و یوناتان در جنگی که در کوه جلبوع واقع شد مردند، فلسطینی‌ها جنازه‌های آنها را در میدان شهر بیتْ‌شان به دار آویختند، ولی مردان یابیش جلعاد شبانه رفتند و جنازه‌های آنها را دزدیدند.) پس استخوانهای شائول و یوناتان را نزد داوود آورده، آنها را در قبر قیس، پدر شائول، واقع در صیلع در ملک بنیامین دفن کردند. سرانجام خداوند دعای داوود را مستجاب نمود و قحطی تمام شد.
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
یک بار وقتی فلسطینی‌ها با اسرائیلی‌ها می‌جنگیدند، داوود و افرادش در بحبوحهٔ جنگ خسته و درمانده شدند.
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
یک غول فلسطینی به نام یشبی بنوب که وزن نیزهٔ مفرغین او در حدود سه کیلو و نیم بود و زره‌ای نو بر تن داشت، به داوود حمله کرد و نزدیک بود او را بکشد.
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
ولی ابیشای پسر صرویه به کمک داوود شتافت و آن فلسطینی را کشت. بنابراین افراد داوود به تأکید به او گفتند: «تو امید اسرائیل هستی و دیگر نباید به میدان جنگ بیایی. ما نمی‌خواهیم تو را از دست بدهیم.»
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
در جنگی که بعد در جُب با فلسطینی‌ها درگرفت، سبکای حوشاتی یک غول فلسطینی دیگر به نام ساف را کشت.
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
بار دیگر در همان محل، الحانان برادر جلیات جتی را که چوب نیزه‌اش به کلفتی چوب نساجها بود، کشت.
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
یک بار هم وقتی فلسطینی‌ها در جت با اسرائیلی‌ها می‌جنگیدند، یک غول فلسطینی که در هر دست و پایش شش انگشت داشت، نیروهای اسرائیلی را به ستوه آورد. آنگاه یوناتان، برادرزادهٔ داوود که پسر شمعا بود، او را کشت.
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
این چهار مرد که به دست داوود و سربازان او کشته شدند از نسل غول‌پیکران جت بودند.

< 2 Samweli 21 >