< 2 Samweli 21 >
1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
Et du temps de David, il y eut une famine qui dura trois années consécutives. David questionna le Seigneur, et le Seigneur dit: Sur Saül et sur sa maison pèse une iniquité qui demande encore de son sang, parce qu'il a mis à mort les Gabaonites.
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
Le roi David appela les Gabaonites, et il s'entretint avec eux. Or, les Gabaonites ne sont point fils d'Israël, mais un débris des Amorrhéens, et les fils d'Israël leur avaient prêté serment; malgré cela, Saül entreprit de les exterminer, dans son zèle pour les fils d'Israël et de Juda.
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
David dit donc aux Gabaonites: Que puis-je faire pour vous? comment pourrai-je vous apaiser afin que vous bénissiez l'héritage du Seigneur?
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Et les Gabaonites répondirent: Entre nous et entre Saül et sa famille, il n'est question ni d'argent, ni d'or, et nul en Israël ne doit, à cause de nous, mourir. Et David reprit: Que voulez-vous dire? Parlez, je le ferai pour vous.
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
Et ils dirent au roi: L'homme qui a tourné contre nous ses forces, qui nous a traqués, qui a conçu le vain projet de nous exterminer, nous voulons l'effacer de sorte qu'il ne reste rien de lui, sur tout le territoire d'Israël.
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
Livre-nous sept de ses fils, afin qu'en Gabaon, ville de Saül, nous les exposions au soleil pour le Seigneur; sept fils de Saül, choisis pour le Seigneur. Et le roi dit: Je vous les livrerai.
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
Le roi épargna Miphiboseth, fils de Jonathan, fils de Saül, à cause du serment du Seigneur que s'étaient mutuellement prêté Jonathan et David.
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
Mais il prit les deux fils de Respha, fille d'Ais, qu'elle avait eus de Saül: Hermoni et Miphiboseth, et les cinq fils de Michol, fille de Saül, qu'elle avait eus d'Esdriel, fils de Berzelli, le Moülathite.
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
Et il les remit aux Gabaonites, qui les exposèrent au soleil, sur la montagne, devant le Seigneur, et tous les sept succombèrent ensemble. Ils moururent dans les premiers jours de la moisson, comme on commençait à couper les orges.
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
Et Respha, fille d'Aïa, prit un cilice, et, au commencement de la moisson des orges, elle se plaça près de la roche; elle y demeura jusqu'à ce que l'eau du ciel tombât sur les morts, et elle ne laissa pas les oiseaux du ciel se poser sur eux, pendant le jour, ni les bêtes fauves des champs les atteindre, pendant la nuit.
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
On alla dire à David ce que faisait Respha, fille d'Aïa, concubine de Saül; puis, on détacha les cadavres; et Dan, fils de Joa, de la race des géants, les prit.
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
Après cela, David partit, et il reprit les ossements de Saül et ceux de Jonathan, aux hommes de Jabès-Galaad qui les avaient dérobés dans les rues de Bethsam, où les Philistins les avaient cloués, le jour de leur victoire sur Saül en Gelboé.
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
Et il rapporta de cette ville les ossements de Saül et ceux de Jonathan, et il recueillit les ossements des sept exposés au soleil.
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
Et l'on ensevelit tous ces ossements, en Benjamin, sur les flancs de la montagne, dans le sépulcre de Cis, père de Saül; on exécuta tout ce que David avait prescrit, et après cela Dieu exauça les vœux de la terre.
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
Ensuite, la guerre s'alluma encore entre les Philistins et Israël. David se mit en campagne avec ses serviteurs; dans une bataille contre les Philistins, lui-même sortit des rangs, et de l'autre côté,
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
Jesbi, de la race des géants. Celui-ci portait une javeline dont la pointe pesait trois cents sicles d'airain; à sa ceinture pendait une massue, et il pensait tuer David.
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
Mais Abessa vint au secours du roi; il frappa le Philistin et il le tua. Alors, les hommes de David jurèrent et dirent: Tu ne viendras plus à la guerre avec nous, de peur que tu n'éteignes la lampe d'Israël.
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
Après cela, il y eut encore un combat près de Geth avec les Philistins. Alors, Sebocha, d'Astaroth, tua Seph, de la race des géants.
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Puis, il y eut une bataille à Rhom avec les Philistins, et Eléanan, fils d'Ariorgim de Bethléem, tua Goliath le Géthéen, qui portait une javeline dont le bois ressemblait au mât d'un tisserand.
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Il y eut encore un combat à Geth. Et il y avait un homme de grande taille, ayant six doigts à chaque main et six doigts à chaque pied, en tout vingt-quatre doigts. Et il était aussi de la race des géants.
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Et il défiait Israël; il fut tué par Jonathan, fils de Sémeï, frère de David.
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Tous les quatre étaient issus des géants, et ils étaient nés à Geth dans la famille de Rhapha, et ils tombèrent sous les coups de David ou de ses serviteurs.