< 2 Samweli 21 >

1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
Au temps de David, il y eut une famine, et elle dura trois ans continus. David consulta la face de Yahweh, et Yahweh dit: « C'est à cause de Saül et de sa maison, parce qu'il y a du sang, parce qu'il a mis à mort des Gabaonites. »
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
Le roi appela les Gabaonites et leur dit: — Les Gabaonites n'étaient pas d'entre les enfants d'Israël, mais ils étaient du reste des Amorrhéens, et les enfants d'Israël s'étaient liés envers eux par serment. Et néanmoins, Saül avait voulu les frapper, par zèle pour les enfants d'Israël et de Juda. —
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
David dit aux Gabaonites: « Que ferai-je pour vous, et avec quoi ferai-je l'expiation, afin que vous bénissiez l'héritage de Yahweh? »
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Les Gabaonites lui dirent: « Ce n'est pas pour nous une question d'argent et d'or avec Saül et avec sa maison, et il n'est pas question pour nous de faire mourir personne en Israël. » Et le roi dit: « Que voulez-vous donc que je fasse pour vous? »
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
Ils répondirent au roi: « Cet homme nous a détruits et il avait formé le projet de nous exterminer, pour que nous ne subsistions pas dans tout le territoire d'Israël:
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
qu'on nous livre sept hommes d'entre ses fils, pour que nous les pendions devant Yahweh à Gabaa de Saül, l'élu de Yahweh. » Et le roi dit: « Je les livrerai. »
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
Le roi épargna Miphiboseth, fils de Jonathas, fils de Saül, à cause du serment par Yahweh qui était entre eux, entre David et Jonathas, fils de Saül.
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
Le roi prit les deux fils que Respha, fille d'Aia, avait enfantés à Saül, Armoni et Miphiboseth, et les cinq fils que Michol, fille de Saül, avait enfantés à Hadriel, fils de Bersellaï, de Molathi,
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
et il les livra entre les mains des Gabaonites, qui les pendirent sur la montagne, devant Yahweh. Tous les sept périrent ensemble; ils furent mis à mort dans les premiers jours de la moisson, au commencement de la moisson des orges.
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
Respha, fille d'Aia, ayant pris un sac, l'étendit pour elle sur le rocher, depuis le commencement de la moisson jusqu'à ce que la pluie se répandit du ciel sur eux; et elle empêcha les oiseaux du ciel de se poser sur eux pendant le jour, et les bêtes des champs pendant la nuit.
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
On apprit à David ce qu'avait fait Respha, fille d'Aia, concubine de Saül.
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
Et David alla prendre les os de Saül et les os de Jonathas, son fils, chez les habitants de Jabès en Galaad, qui les avaient enlevés de la place de Bethsan, où les Philistins les avaient suspendus, au jour où les Philistins avaient battu Saül à Gelboé.
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
Il emporta de là les os de Saül et les os de Jonathas, son fils, et l'on recueillit aussi les os de ceux qui avaient été pendus.
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
On enterra les os de Saül et de son fils Jonathas dans le pays de Benjamin, à Séla, dans le sépulcre de Cis, père de Saül, et l'on fit tout ce que le roi avait ordonné. Après cela, Dieu fut apaisé envers le pays.
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
Il y eut encore guerre entre les Philistins et Israël, et David descendit avec ses serviteurs, et ils combattirent les Philistins: David fut fatigué.
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
Et Jesbi-Benob, l'un des fils de Rapha, — le poids de sa lance était de trois cents sicles d'airain, et il était ceint d'une épée neuve, — parlait de frapper David.
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
Abisaï, fils de Sarvia, vint au secours de David; il frappa le Philistin et le tua. Alors les gens de David lui firent serment, en lui disant: « Tu ne sortiras plus avec nous pour combattre, et tu n'éteindras point le flambeau d'Israël. »
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
Après cela, il y eut encore une bataille à Gob avec les Philistins. Alors Sabochaï, le Husathite, tua Saph, qui était parmi les fils de Rapha.
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Il y eut encore une bataille à Gob avec les Philistins; et Elchanan, fils de Jaaré-Oreghim, de Bethléem, tua Goliath de Geth; le bois de sa lance était semblable à une ensouple de tisserand.
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Il y eut encore une bataille à Geth. Il s'y trouva un homme de haute taille, et les doigts de ses mains et les doigts de ses pieds étaient au nombre respectif de six, vingt-quatre en tout, et lui aussi descendait de Rapha.
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Il insulta Israël, et Jonathan, fils de Samaa, frère de David, le tua.
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Ces quatre hommes étaient des fils de Rapha, à Geth; ils périrent par la main de David et par la main de ses serviteurs.

< 2 Samweli 21 >