< 2 Samweli 21 >

1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
and to be famine in/on/with day David three year year after year and to seek David [obj] face LORD and to say LORD to(wards) Saul and to(wards) house: household [the] blood upon which to die [obj] [the] Gibeonite
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
and to call: call to [the] king to/for Gibeonite and to say to(wards) them and [the] Gibeonite not from son: descendant/people Israel they(masc.) that if: except if: except from remainder [the] Amorite and son: descendant/people Israel to swear to/for them and to seek Saul to/for to smite them in/on/with be jealous he to/for son: descendant/people Israel and Judah
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
and to say David to(wards) [the] Gibeonite what? to make: do to/for you and in/on/with what? to atone and to bless [obj] inheritance LORD
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
and to say to/for him [the] Gibeonite nothing (to/for us *Q(K)*) silver: money and gold with Saul and with house: household his and nothing to/for us man to/for to die in/on/with Israel and to say what? you(m. p.) to say to make: do to/for you
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
and to say to(wards) [the] king [the] man which to end: destroy us and which to resemble to/for us to destroy from to stand in/on/with all border: area Israel
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
(to give: give *Q(K)*) to/for us seven human from son: descendant/people his and to dislocate/hang them to/for LORD in/on/with Gibeah Saul chosen LORD and to say [the] king I to give: give
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
and to spare [the] king upon Mephibosheth Mephibosheth son: child Jonathan son: child Saul upon oath LORD which between them between David and between Jonathan son: child Saul
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
and to take: take [the] king [obj] two son: child Rizpah daughter Aiah which to beget to/for Saul [obj] Armoni and [obj] Mephibosheth and [obj] five son: child Merab daughter Saul which to beget to/for Adriel son: child Barzillai [the] Meholathite
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
and to give: give them in/on/with hand: power [the] Gibeonite and to dislocate/hang them in/on/with mountain: mount to/for face: before LORD and to fall: kill (seven their *Q(K)*) unitedness (and they(masc.) *Q(k)*) to die in/on/with day harvest in/on/with first (in/on/with beginning *Q(K)*) harvest barley
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
and to take: take Rizpah daughter Aiah [obj] [the] sackcloth and to stretch him to/for her to(wards) [the] rock from beginning harvest till to pour water upon them from [the] heaven and not to give: allow bird [the] heaven to/for to rest upon them by day and [obj] living thing [the] land: country night
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
and to tell to/for David [obj] which to make: do Rizpah daughter Aiah concubine Saul
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
and to go: went David and to take: take [obj] bone Saul and [obj] bone Jonathan son: child his from with master: men Jabesh (Jabesh)-gilead which to steal [obj] them from street/plaza Beth-shean Beth-shean which (to hang them there [to] Philistine *Q(K)*) in/on/with day to smite Philistine [obj] Saul in/on/with Gilboa
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
and to ascend: establish from there [obj] bone Saul and [obj] bone Jonathan son: child his and to gather [obj] bone [the] to dislocate/hang
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
and to bury [obj] bone Saul and Jonathan son: child his in/on/with land: country/planet Benjamin in/on/with Zela in/on/with grave Kish father his and to make: do all which to command [the] king and to pray God to/for land: country/planet after so
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
and to be still battle to/for Philistine with Israel and to go down David and servant/slave his with him and to fight with Philistine and be faint David
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
(and Ishbi-benob *Q(K)*) Ishbi-benob which in/on/with born [the] Rapha and weight spear his three hundred weight bronze and he/she/it to gird new and to say to/for to smite [obj] David
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
and to help to/for him Abishai son: child Zeruiah and to smite [obj] [the] Philistine and to die him then to swear human David to/for him to/for to say not to come out: come still with us to/for battle and not to quench [obj] lamp Israel
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
and to be after so and to be still [the] battle in/on/with Gob with Philistine then to smite Sibbecai [the] Hushathite [obj] Saph which in/on/with born [the] Rapha
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
and to be still [the] battle in/on/with Gob with Philistine and to smite Elhanan son: child Jaare-oregim Jaare-oregim Bethlehemite [the] Bethlehemite [obj] Goliath [the] Gittite and tree: stake spear his like/as loom-beam to weave
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
and to be still battle in/on/with Gath and to be man (stature *Q(K)*) and finger hand his and finger foot his six and six twenty and four number and also he/she/it to beget to/for [the] Rapha
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
and to taunt [obj] Israel and to smite him Jonathan son: child (Shimeah *Q(K)*) brother: male-sibling David
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
[obj] four these to beget to/for [the] Rapha in/on/with Gath and to fall: kill in/on/with hand: power David and in/on/with hand: power servant/slave his

< 2 Samweli 21 >