< 2 Samweli 20 >
1 Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
Mane yiğbışil Benyaminaaşina Bikriyna dix Şeva donana sa karaı'dəəna insan Gilgalee eyxhe. Mang'vee şeypur əlixı', eyhen: – Şaka Davuduka, Yesseyne duxayka, sacigeedın kar deşin! Yişda mang'uka avqas deş! İzrailybı, gırgınbı xaybışeeqa savk'le!
2 Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
Gırgıne İzrailybışe Davud g'alerçu, Bikriyne duxayqa Şevayqa qihna avayk'an. Yahudermee cone paççahıke Davuduke cureebaxhe deş. Manbı İordanne damaysse İyerusalimqamee Davuduqa qihna avayk'an.
3 Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
Davud cune İyerusalimeene sareeqa siyk'al. Mang'vee sarayqa ilyaakasva g'alyav'uyn caariyebı sa xaaqa akkyaa'a. Qiyğa mane xaane hiqiy-alla g'aravulyçer giviyxhe. Mang'vee manbışis gırgıncad helen. Mana saccu manbışika g'ılexha deş. Manbı sip'ırer xhinne vuxha. Manbı hapt'asmee mane xaançe qığeebaç'e deş.
4 Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
Paççahee Amasayk'le eyhen: – Xhebne yiğee Yahuder zasqa see'e, ğunar cone k'ane ixhe.
5 Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
Amasa, Yahuder sacigeeqa qoot'alasva ark'ıneeyir, cus gyuvxhuyne gahıl yı'q'əlqa siyk'al deş.
6 Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
Davudee Avişayk'le eyhen: – Həşde Bikriyne duxee, Şevayee, şas dekkanan Avşalomuled geed ha'as. Yizın insanarıb alyapt'ı, ğu mang'uqar qihna hoora. Deşxheene, sayıb mang'vee hiqiy-allançe cabırbışika it'um hı'iyn şaharbı t'abal hı'ı, yişde uleke aygval.
7 Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
Yoavın insanar, Keretbı, Peletbı, gırgın yugun cehiler Bikriyna dix Şeva t'abal ha'asva İyerusalimeençe mang'uqa qihna gyabak'a. Manbışil ooyur Avişay ıxha.
8 Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
Manbı Giveoneene xənne g'ayeyne k'anenang'a Amasa manbışde ögilqa arayle. Yoavıl dəv'əyn tanalinbı ıxha, yıq'eeqab ts'ira qav'u vuxha. Mane ts'iraylid g'ılınc givatxın ıxha. Mana ögilqava əlyhəəme, g'ılınc givatxınne cigeençe qakkitxhu, g'e'exhxhan.
9 Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
Yoavee Amasayk'le eyhen: – Yizda çoc, ğu yugrane vor? Qiyğa Yoavee Amaseys ubba ha'asva, mana sağne xıleka muç'ruyke aqqaqqa.
10 Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Amasee, Yoavne solne xılene g'ılıncılqa fıkır hoole deş. Yoavee xılen g'ılınc Amasayne vuxhnyaqa hı'xı' mang'un iç'alatbı ç'iyelqa ehekka'a. Q'öd'es g'ılınc hı'xəsda iş aaxva deş, mana mankecar qek'ana. Yoaviy cuna çoc Avişayıb Bikriyne duxayqa, Şevayqa, qihna avayk'an.
11 Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
Yoavne insanaaşine sang'vee Amasayne k'ane ulyorzul, eyhen: – Şavusiy Yoav ıkkan, vuşuyiy Davudne sural Yoavıqa qihna qoracen.
12 Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
Amasa yəqqı'ne yı'q'nee eban alyart'u ıxha. Mane insanık'le g'ecen, Amasayne mayıtısqa qarına-qarına maa'ar ulyoyzarır. Millet mang'usne ulyoyzar g'ecemee, mang'vee Amasayn mayıt yəqqı'ne yı'q'neençe alyaat'u, çoleeqa qıkkı, ooqad tanalin kar adaççe.
13 Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Amasa yəqqı'le alyart'uyle qiyğa, gırgınbı Bikriyna dix Şeva aqqasva Yoavne qihna avayk'an.
14 Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
Yoav Avel-Bet-Maaka eyhene şaharılqasse gırgıne İzrailyne nasılbışde yı'q'neençe ılğeç'e. Maane cigabışeençeb g'oşun sabı, mang'uqab qihna avayk'an. Sayib mang'uqab qihna Berim eyhene cigeençenbı avayk'an.
15 Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
Yoavna g'oşun k'yoptul, Avel-Bet-Maaka hiqiy-allançe avqaaqqana. Manbışe şaharne cabırbışde hiqiy-alla nyuq'vneke sa axtın ciga hı'ı, cabırbı qukkyok'al ha'as havayk'an.
16 mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
Mane gahil sa ək'elikane zəiyfee şahareençe ts'ir hav'u, eyhen: – K'ırıbı alixhxhe! K'ırıbı alixhxhe! Hucoona ixhes, Yoavık'le inyaqana qoracen, cuk'le eyhesın cuvab vodun.
17 Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
Yoav məng'ısqana qarımee, məng'ee qiyghanan: – Yoav ğune vor? Mang'vee, «Ho'o, zı vornava» eyhe. Zəiyfee meed eyhen: – K'ırı alixhxhe, zı, yiğne nukaree, vak'le hucooyiy eyhes. Mang'vee «Yizın k'ırı val vodva» alidghıniy qele.
18 Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
Zəiyfee eyhen: – Şenke «Mı'sləhət Avel eyhene şahareençe hevqevaniyxhe» eyhen. İş manbışe məxüb g'ooce vuxha.
19 Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
Mana İzrailyna yugvalla vukkanna qopkuna sa şahar vobna. Vas İzrailyne xəbne şaharbışda sane hı'ğəəkar haa'as vukkan? Nişil-allane vas Rəbbis vukkanne şaharbışda sa hı'ğəəkar ha'as vukkan?
20 Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
Yoavee alidghıniy qelen: – Hı'ğəəkaraa'asdayiy avaak'an haa'asda fıkır zake əq'əna quvxhecen!
21 Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
Man ğu eyhen xhinne deş vod. Efrayimne suvabınane cigeençe Bikriyne dix Şeva paççah Davudılqa g'elil qıxha. Saccu mana şasqa qele, zınar ine şaharısse qığeç'u, əlyhəəsda. Zəiyfee Yoavık'le eyhen: – Mang'una vuk'ul şaharne cabırıle valqa dağepçes.
22 Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
Zəiyfa ək'elika ı'ğiykır milletne k'anyaqa iyeek'an. Milletınıb Bikriyne duxayna Şevayna vuk'ul gats'apk'ın, mang'usqa dağabaççe. Mançile qiyğa Yoavee şeypur ı'lyviyxə, g'oşunub şaharne hiqiy-allançe ts'ıts'ooxhena. Gırgınbı cone xaybışeeqa siviyk'al. Yoavır İyerusalimqa paççahne k'anyaqa siyk'al.
23 Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
Yoav gırgıne İzrailyne g'oşunna xərna ıxha. Yehoyadayna dix Benaya Keretbışdayiy Peletbışda xərna ıxha.
24 Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Adoram həmbalaaşina xərna ıxha. Axiludna dix Yehoşafat taarix oyk'anna ıxha.
25 Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
Şeva mirza ıxha, Tsadokiy Evyatarıb kaahinar vuxha.
26 na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.
Yair eyhene şahareençena İra Davudusne kaahin ıxha.