< 2 Samweli 20 >
1 Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
Nakapasamak iti isu met laeng a lugar nga adda iti maysa a manangriribok a managan iti Siba a putot ni Bikri, a Benjaminita. Pinuyotanna ti trumpeta ket kinunana, “Awan ti bingaytayo kenni David, kasta met nga awan ti tawidtayo iti putot ni Jesse. Agawid ketdin ti tunggal maysa iti pagtaenganna diay Israel.”
2 Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
Isu a pinanawan amin dagiti Israelita ni David ket sinurotda ni Siba a putot ni Bikri. Ngem sinurot dagiti tattao ti Juda ti ari, manipud iti Jordan agingga idiay Jerusalem.
3 Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
Idi dimteng ni David iti palasiona idiay Jerusalem, innalana dagiti sangapulo nga adipen nga assawana nga imbatina a mangtaripato iti palasio, ket pinagnaedna ida iti balay a nainget ti pannakabantayna. Impaayna dagiti masapsapulda, ngem saannan a kinaidda pay ida. Isu a naiserraanda agingga iti aldaw nga ipapatayda, nagbibiagda a kasda la balo.
4 Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
Ket kinuna ti ari kenni Amasa, “Ummongem dagiti amin a tattao ti Juda iti unos ti tallo nga aldaw; masapul nga addaka met ditoy.”
5 Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
Isu a napan inayaban ni Amasa dagiti amin a tattao ti Juda, ngem nagtalinaed isuna iti nabaybayag ngem iti ingkeddeng ti ari a tiempo nga imbilinna kenkuana.
6 Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
Isu a kinuna ni David kenni Abisai, “Ita, nakarkaronto pay a kinaranggas ti aramiden ni Siba a putot ni Bikri kadatayo ngem ti inaramid ni Absalom. Ikuyogmo dagiti adipen ti apom, dagiti soldadok, ket kamatenyo isuna, ta di ket mangbirok kadagiti natalged a siudad ket makalibas isuna iti panagkitatayo.”
7 Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
Simmaruno ngarud kenkuana dagiti tattao ni Joab, a kaduada dagiti Cheretita ken dagiti Peletita ken dagiti amin a maingel a mannakigubat. Pinanawanda ti Jerusalem tapno kamatenda ni Siba a putot ni Bikri.
8 Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
Idi addadan idiay ayan ti dakkel a bato idiay Gabaon, dimteng ni Amasa a sumabat kadakuada. Nakaaruat ni Joab ti kalasag a pakigubat, a pakaibilangan ti barikes iti siketna nga addaan iti nakakaluban a kampilan a nakagalot iti daytoy. Iti panpannagnana nga agpasango, natnag ti kampilan.
9 Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
Isu a kinuna ni Joab kenni Amasa, “Naimbag kadi ti amin kenka, kasinsinko?” Siaayat nga iniggaman ni Joab ti barbas ni Amasa babaen iti kannawan nga imana tapno agkanna isuna.
10 Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Saan a nadlaw ni Amasa ti imuko nga adda iti kannigid nga ima ni Joab. Dinuyok ni Joab ti buksit ni Amasa ket natnag dagiti bagisna iti daga. Saanen nga inulit pay a dinuyok ni Joab isuna, ket natay ni Amasa. Isu a kinamat ni Joab ken ni Abisai a kabsatna ni Siba a putot ni Bikri.
11 Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
Ket nagtakder iti abay ni Amasa ti maysa kadagiti tattao ni Joab, ken kinuna ti lalaki, “Siasinoman nga umanamong kenni Joab, ken siasinoman a para kenni David, surotenna ni Joab.”
12 Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
Naidasay ni Amasa a nadigos iti darana iti tengnga ti dalan. Idi nakita ti lalaki a nagtalinaed a nakatakder dagiti tattao, binagkatna ni Amasa manipud iti dalan ket impanna iti tay-ak. Inabbonganna ti lupot isuna gapu ta nakitana a ti tunggal tao a lumabas ket agtakder.
13 Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
Kalpasan a naibagkat ni Amasa manipud iti dalan, simmurot amin dagiti tattao kenni Joab a mangkamat kenni Siba a putot ni Bikri.
14 Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
Linabsan ni Siba dagiti amin a tribu ti Israel a nagturong iti Abel, iti Bet Maaca, ken kadagiti amin a daga ti Berites, a naguummong ken kimmamat met kenni Siba.
15 Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
Nakamatanda isuna ket pinalawlawanda isuna idiay Abel ti Bet Maaca. Pinalawlawanda iti nabunton a daga ti igid ti pader ti siudad. Minaso dagiti amin nga armada a kadua ni Joab ti pader tapno marba daytoy. Ket nagpukkaw ti maysa a masirib a babai iti siudad,
16 mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
“Dumngegka, pangaasim ta dumngegka, Joab! Umasidegka kaniak tapno makatungtongka.”
17 Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
Isu nga immasideg ni Joab kenkuana, ket kinuna ti babai, “Sika kadi ni Joab?” Simmungbat isuna, “Siak,” Ket kinuna ti babai kenkuana, “Denggem ti sao daytoy adipenmo.” Insungbatna, “Dumdumngegak.”
18 Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
Ket nagsao ti babai, “Masansan a maibaga idi un-unana a tiempo, 'Pudno a no dumawatka ti pammagbaga idiay Abel,' ket sulbaren dayta a pammagbaga ti parikutmo.
19 Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
Dakami ti siudad a maysa kadagiti katatalnaan ken kapupudnoan iti Israel. Padpadasenyo a dadaelen ti siudad nga ina iti Israel. Apay a kayatyo nga alun-onen ti tawid ni Yahweh?”
20 Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
Isu a simmungbat ni Joab ket kinunana, “Saan a kasta, saan a kasta kaniak, a rumbeng nga alun-onek wenno dadaelek.
21 Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
Saan a pudno dayta. Ngem adda ti lalaki a naggapu iti turod ti pagilian ti Efraim, a managan ti Siba a putot ni Bikri, ket intag-ayna ti imana a maibusor iti ari, maibusor kenni David. Isukoyo isuna, ket pumanawak iti siudad.” Kinuna ti babai kenni Joab, “Maipuruak ti ulona kenka iti ngatoen ti pader.”
22 Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
Ket napan ti babai kadagiti amin a tattao nga ammona. Pinutedda ti ulo ni Siba a putot ni Bikri, ket impurwakda daytoy kenni Joab. Kalpasanna, pinuyotanna ti trumpeta ket pinanawan dagiti tattao ni Joab ti siudad, nagawid ti tunggal maysa iti pagtaenganna. Ket nagsubli ni Joab idiay Jerusalem iti ayan ti ari.
23 Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
Ita, ni Joab ti nangidadaulo kadagiti amin nga armada ti Israel, ken ni Benaias a putot ni Jehoyada ti nangidaulo kadagiti Cheretites ken kadagiti Peletites.
24 Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Ni Adoram ti nangidaulo kadagiti tattao nga agtrabaho nga ingkapilitan, ket ni Jehosafat a putot ni Ahilut ti tagailista.
25 Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
Ni Siva ti sekretario ken da Zadok ken Abiatar dagiti papadi.
26 na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.
Ni Ira a Jairita ti panguloen a ministro ni David.