< 2 Samweli 20 >
1 Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
And there happened to be a worthless man, whose name was Sheba', the son of Bichri, a Benjamite; and he blew the cornet, and said, We have no part in David, nor have we any inheritance in the son of Jesse: every man to his tents, O Israel!
2 Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
So every man of Israel went off from David, following Sheba' the son of Bichri; but the men of Judah adhered unto their king, from the Jordan even to Jerusalem.
3 Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
And David came to his house at Jerusalem; and the king took the ten women, the concubines, whom he had left to guard the house, and put them in a guard-house, and provided for them, but went not in unto them. So they were confined until the day of their death, living in widowhood.
4 Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
Then said the king to 'Amassa, Call together for me the men of Judah within three days, and thou present thyself here [then].
5 Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
So 'Amassa went to call Judah together; but he remained out longer than the set time which he had appointed him.
6 Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
And David said to Abishai, Now will Sheba' the son of Bichri do us more harm than [did] Abshalom: take thou the servants of thy Lord, and pursue after him, lest he succeed in reaching fortified cities, and withdraw himself from our eyes.
7 Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
And there went out after him Joab's men, and the Kerethites, and the Pelethites, and all the mighty men: and they went forth out of Jerusalem, to pursue after Sheba' the son of Bichri.
8 Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
They were close by the great stone which is at Gib'on, as 'Amassa came before them. And Joab was girded with his coat, his [usual] garment, and upon it the girdle of the sword which was fastened upon his loins in its sheath; and as he went forth it fell out.
9 Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
And Joab said to 'Amassa, Art thou in health, my brother? And Joab's right hand took hold of 'Amassa's beard to kiss him.
10 Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
And 'Amassa did not guard himself against the sword that was in Joab's hand: so he smote him therewith in the fifth rib and shed out his bowels to the ground, and struck him not again; and he died. But Joab and Abishai his brother pursued after Sheba' the son of Bichri.
11 Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
And one man of Joab's people remained standing by him, and said, He that favoreth Joab, and he that is for David, follow Joab.
12 Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
And 'Amassa was wallowing in his blood in the midst of the highway. And when the man saw that all the people stood still, he put 'Amassa aside out of the highway into the field, and threw a garment over him, when he saw that every one that came by him stood still.
13 Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
When he was removed out of the highway, every man passed on after Joab, to pursue after Sheba' the son of Bichri.
14 Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
And this one passed through all the tribes of Israel unto Abel, which is of Beth-ma'achah, and all the Berim: and they assembled themselves together, and went also after him.
15 Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
And they came and besieged him in Abel of Beth-ma'achah, and they cast up a trench against the city, and it stood enclosed by the troops: and all the people that were with Joab were battering to throw down the wall.
16 mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
Then called a wise woman out of the city, Hear, hear: say, I pray you, unto Joab, Come near as far as hither, that I may speak with thee.
17 Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
And when he was come near unto her, the woman said, Art thou Joab? And he said, I am. Then said she unto him, Hear the words of thy hand-maid. And he said, I do hear.
18 Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
Then said she, thus, They ought surely first to have spoken, saying, “Let them ask at least in Abel:” and so would they have come to an end.
19 Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
I am one of the peaceful and faithful [cities] in Israel; thou seekest to overthrow a city and a metropolis in Israel: why wilt thou destroy the inheritance of the Lord?
20 Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
And Joab answered and said, Far be it, far be it from me, that I should destroy or ruin.
21 Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
The matter is not so; but a man from the mountains of Ephraim, Sheba' the son of Bichri is his name, hath lifted up his hand against the king, against David: give him up alone, and I will withdraw from the city. And the woman said unto Joab, Behold, his head shall be cast down to thee over the wall.
22 Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
And the woman came unto all the people with her wisdom; and they cut off the head of Sheba' the son of Bichri, and cast it down to Joab: and he blew the cornet, and they scattered themselves from the city, every man to his tents. And Joab returned to Jerusalem unto the king.
23 Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
Now Joab was over all the army of Israel; and Benayah the son of Yehoyada' was over the Kerethites and over the Pelethites;
24 Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
And Adoram was over the tribute; and Jehoshaphat the son of Achilud was recorder;
25 Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
And Sheva was scribe; and Zadok and Ebyathar were priests;
26 na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.
And 'Ira also the Yairite was an officer of state unto David.