< 2 Samweli 20 >

1 Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
Then there was come thither a wicked man (named Sheba the sonne of Bichri, a man of Iemini) and hee blew the trumpet, and saide, Wee haue no part in Dauid, neither haue we inheritance in the sonne of Ishai: euery man to his tents, O Israel.
2 Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
So euery man of Israel went from Dauid and followed Sheba the sonne of Bichri: but the men of Iudah claue fast vnto their King, from Iorden euen to Ierusalem.
3 Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
When Dauid then came to his house to Ierusalem, the King tooke the ten women his concubines, that hee had left behinde him to keepe the house, and put them in warde, and fed them, but lay no more with them: but they were enclosed vnto the day of their death, liuing in widowhode.
4 Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
Then sayde the King to Amasa, Assemble me the men of Iudah within three dayes, and be thou here present.
5 Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
So Amasa went to assemble Iudah, but hee taried longer then the time which he had appoynted him.
6 Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
Then Dauid sayd to Abishai, Now shall Sheba the sonne of Bichri doe vs more harme then did Absalom: take thou therefore thy lords seruants and follow after him, lest he get him walled cities, and escape vs.
7 Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
And there went out after him Ioabs men, and the Cherethites and the Pelethites, and all the mightie men: and they departed out of Ierusalem, to follow after Sheba the sonne of Bichri.
8 Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
When they were at the great stone, which is in Gibeon, Amasa went before them, and Ioabs garment, that hee had put on, was girded vnto him, and vpon it was a sword girded, which hanged on his loynes in the sheath, and as hee went, it vsed to fall out.
9 Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
And Ioab sayde to Amasa, Art thou in health, my brother? and Ioab tooke Amasa by the beard with the right hand to kisse him.
10 Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
But Amasa tooke no heede to the sworde that was in Ioabs hande: for therewith he smote him in the fift rib, and shed out his bowels to the ground, and smote him not the second time: so he dyed. then Ioab and Abishai his brother followed after Sheba the sonne of Bichri.
11 Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
And one of Ioabs men stoode by him, and saide, He that fauoureth Ioab, and hee that is of Dauids part, let him go after Ioab.
12 Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
And Amasa wallowed in blood in the mids of the way: and when the man sawe that all the people stood still, he remooued Amasa out of the way into the fielde, and cast a cloth vpon him, because he saw that euery one that came by him, stoode still.
13 Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
When hee was remoued out of the way, euerie man went after Ioab, to follow after Sheba the sonne of Bichri.
14 Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
And he went through all the tribes of Israel vnto Abel, and Bethmaachah and all places of Berim: and they gathered together, and went also after him.
15 Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
So they came, and besieged him in Abel, neere to Bethmaachah: and they cast vp a mount against the citie, and the people thereof stood on the ramper, and al the people that was with Ioab, destroyed and cast downe the wall.
16 mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
Then cried a wise woman out of the citie, Heare, heare, I pray you, say vnto Ioab, Come thou hither, that I may speake with thee.
17 Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
And when hee came neere vnto her, the woman said, Art thou Ioab? And he answered, Yea. And she said to him, Heare the wordes of thine handmaid. And he answered, I do heare.
18 Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
Then shee spake thus, They spake in the olde time, saying, They shoulde aske of Abel. and so haue they continued.
19 Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
I am one of them, that are peaceable and faithful in Israel: and thou goest about to destroy a citie, and a mother in Israel: why wilt thou deuoure the inheritance of the Lord?
20 Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
And Ioab answered, and said, God forbid, God forbid it me, that I should deuoure, or destroy it.
21 Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
The matter is not so, but a man of mout Ephraim (Sheba ye sonne of Bichri by name) hath lift vp his had against ye King, euen against Dauid: deliuer vs him onely, and I will depart from the citie. And the woman saide vnto Ioab, Beholde, his head shalbe throwen to thee ouer the wall.
22 Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
Then the woman went vnto all the people with her wisedome, and they cut off the head of Sheba the sonne of Bichri, and cast it to Ioab: the he blewe the trumpet, and they retired from the citie, euery man to his tent: and Ioab returned to Ierusalem vnto the King.
23 Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
Then Ioab was ouer all the hoste of Israel, and Benaiah the sonne of Iehoiada ouer the Cherethites and ouer the Pelethies,
24 Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
And Adoram ouer the tribute, and Ioshaphat the sonne of Ahilud the recorder,
25 Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
And Sheia was Scribe, and Zadok and Abiathar the Priests,
26 na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.
And also Ira the Iairite was chiefe about Dauid.

< 2 Samweli 20 >