< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
E succedeu depois d'isto que David consultou ao Senhor, dizendo: Subirei a alguma das cidades de Judah? E disse-lhe o Senhor: Sobe. E disse David: Para onde subirei? E disse: Para Hebron.
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
E subiu David para lá, e tambem as suas duas mulheres, Achinoam. a jizreelita, e Abigail, a mulher de Nabal, o carmelita.
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
Fez tambem David subir os homens que estavam com elle, cada um com a sua familia: e habitaram nas cidades de Hebron.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
Então vieram os homens de Judah, e ungiram ali a David rei sobre a casa de Judah. E deram avisos a David, dizendo: Os homens de Jabez-gilead são os que sepultaram a Saul.
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
Então enviou David mensageiros aos homens de Jabez-gilead, e disse-lhes: Bemditos sejaes vós do Senhor, que fizestes tal beneficencia a vosso senhor, a Saul, e o sepultastes!
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
Agora, pois, o Senhor use comvosco de beneficencia e fidelidade: e tambem eu vos farei este bem, porquanto fizestes isto.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
Esforcem-se pois agora as vossas mãos, e sêde homens valentes, pois Saul, vosso senhor, é morto, mas tambem os da casa de Judah já me ungiram a mim rei sobre si.
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
Porém Abner, filho de Ner, capitão do exercito de Saul, tomou a Isboseth, filho de Saul, e o fez passar a Mahanaim,
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
E o constituiu rei sobre Gilead, e sobre os assuritas, e sobre Jizreel, e sobre Ephraim, e sobre Benjamin, e sobre todo o Israel.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
Da edade de quarenta annos era Isboseth, filho de Saul, quando começou a reinar sobre Israel, e reinou dois annos: mas os da casa de Judah seguiam a David.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
E foi o numero dos dias que David reinou em Hebron, sobre a casa de Judah, sete annos e seis mezes.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
Então saiu Abner, filho de Ner, com os servos de Isboseth, filho de Saul, de Mahanaim a Gibeon.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
Sairam tambem Joab, filho de Zeruia, e os servos de David, e se encontraram uns com os outros perto do tanque de Gibeon: e pararam estes d'esta banda do tanque, e os outros d'aquella banda do tanque.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
E disse Abner a Joab: Deixa levantar os mancebos, e joguem diante de nós. E disse Joab: Levantem-se.
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
Então se levantaram, e passaram, por conta, doze de Benjamin, da parte d'Isboseth, filho de Saul, e doze dos servos de David.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
E cada um lançou mão da cabeça do outro, metteu-lhe a espada pela ilharga, e cairam juntamente: d'onde se chamou áquelle logar Helkath-hazzurim, que está junto a Gibeon.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
E seguiu-se n'aquelle dia uma crua peleja: porém Abner e os homens de Israel foram feridos diante dos servos de David.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
E estavam ali os tres filhos de Zeruia, Joab, Abisai, e Asael: e Asael era ligeiro de pés, como uma das cabras montezes que ha no campo.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
E Asael perseguiu a Abner: e não declinou de detraz de Abner, nem para a direita nem para a esquerda.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
E Abner, olhando para traz, disse: És tu este Asael? E disse elle: Eu sou.
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
Então lhe disse Abner: Desvia-te para a direita, ou para a esquerda, e lança mão d'um dos mancebos, e toma os seus despojos. Porém Asael não quiz desviar-se de detraz d'elle.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
Então Abner tornou a dizer a Asael: Desvia-te de detraz de mim: porque hei de eu ferir-te e dar comtigo em terra? e como levantaria eu o meu rosto diante de Joab teu irmão?
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
Porém, não se querendo elle desviar, Abner o feriu com o couto da lança pela quinta costella, e a lança lhe saiu por detraz, e caiu ali, e morreu n'aquelle mesmo logar; e succedeu que todos os que chegavam ao logar onde Asael caiu e morreu paravam.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
Porém Joab e Abisai perseguiram a Abner: e poz-se o sol, chegando elles ao outeiro de Amma, que está diante de Giah, junto ao caminho do deserto de Gibeon.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
E os filhos de Benjamin se ajuntaram detraz d'Abner, e fizeram um batalhão, e pozeram-se no cume d'um outeiro.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
Então Abner gritou a Joab, e disse: Consumirá a espada para sempre? não sabes tu que por fim haverá amargura? e até quando não has de dizer ao povo que se torne de detraz de seus irmãos?
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
E disse Joab: Vive Deus, que, se não tivesses fallado, já desde pela manhã o povo teria cessado cada um de perseguir a seu irmão.
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
Então Joab tocou a bozina, e todo o povo parou, e não perseguiram mais a Israel: e tão pouco pelejaram mais.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
E caminharam Abner e os seus homens toda aquella noite pela planicie: e, passando o Jordão, caminharam por todo o Bithron, e vieram a Mahanaim.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
Tambem Joab se tornou de detraz d'Abner, e ajuntou todo o povo: e dos servos de David faltaram dezenove homens, e Asael.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
Porém os servos de David feriram d'entre os de Benjamin, e d'entre os homens d'Abner, a trezentos e sessenta homens, que ali ficaram mortos.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
E levantaram a Asael, e sepultaram-n'o na sepultura de seu pae, que estava em Beth-lehem: e Joab e seus homens caminharam toda aquella noite, e amanheceu-lhes em Hebron.

< 2 Samweli 2 >