< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
I stało się potem, że pytał Dawid Pana, mówiąc: Mamże iść do któregokolwiek miasta Judzkiego? Któremu Pan odpowiedział: Idź. I rzekł Dawid: Dokądże pójdę? I odpowiedział: Do Hebronu.
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
Tedy tam jechał Dawid, także i dwie żony jego, Achinoam Jezreelitka, i Abigail żona przedtem Nabalowa z Karmelu.
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
Także męże swe, którzy z nim byli, zabrał Dawid, każdego z domem jego, i mieszkali w miastach Hebrońskich.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
Przyszli potem mężowie Juda, i pomazali tam Dawida za króla nad domem Juda; tedy opowiadano Dawidowi, mówiąc: Mężowie z Jabes Galaad ci pogrzebli Saula.
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
Tedy wyprawił Dawid posły do mężów z Jabes Galaad, i rzekł do nich: Błogosławieniście wy od Pana, którzyście ucznili to miłosierdzie nad Panem waszym Saulem, żeście go pogrzebli.
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
Przetoż teraz niech uczyni Pan z wami miłosierdzie, i prawdę, a ja też oddam wam to dobrodziejstwo, żeście uczynili tę rzecz.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
Teraz tedy niech się zmacniają ręce wasze, a bądźcie mężnymi; bo choć umarł Saul, pan wasz, wszakże mnie pomazał dom Juda za króla nad sobą.
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
A Abner, syn Nera, hetman nad wojskiem Saulowem, wziął Izboseta syna Saulowego, i przyprowadził go do Machanaim,
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
I uczynił go królem nad Gaaladem, i nad Assury, i nad Jezreelem, i nad Efraimem, i nad Benjaminem, i nad wszystkim Izraelem.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
Czterdzieści lat miał Izboset, syn Saula, gdy począł królować nad Izraelem, a dwa lata królował; tylko dom Juda stał przy Dawidzie.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
I była liczba dni, których był Dawid królem w Hebronie nad domem Judzkim, siedm lat i sześć miesięcy.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
Potem wyszedł Abner, syn Nera, i słudzy Izboseta, syna Saulowego, z Machanaim do Gabaonu.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
Joab także, syn Sarwii, z sługami Dawidowymi wyszli, i spotkali się z sobą prawie u stawu Gabaońskiego, i zostali jedni na jednej stronie stawu, a drudzy na drugiej stronie stawu.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
Tedy rzekł Abner do Joaba: Niech teraz wstaną młodzieńcy, a poigrają przed nami. I rzekł Joab: Niech wstaną.
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
Wstali tedy; i wyszło w liczbie dwanaście z Benjamińczyków ze strony Izboseta, syna Saulowego, a dwanaście z sług Dawidowych.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
Którzy uchwyciwszy się, każdy za głowę przeciwnika swego, utopił miecz swój w boku jeden drugiego, i polegli pospołu. Przetoż nazwano miejsce ono Helkatassurym, które jest w Gabaonie.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
I była bitwa bardzo sroga dnia onego, a porażon jest Abner i mężowie Izraelscy od sług Dawidowych.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
I byli też tam trzej synowie Sarwii: Joab, Abisaj, i Asael; ale Asael był prędkich nóg, jako dzika koza.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
I gonił Asael Abnera, a nie ustąpił idąc ani na prawo ani na lewo, ścigając Abnera.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
A obejrzawszy się Abner nazad, rzekł: Tyżeś jest Asael? A on mu odpowiedział: Ja.
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
Tedy mu rzekł Abner: Uchyl się na prawą stronę twoję, albo na lewą stronę twoję, a pojmij sobie jednego z młodzieńców, i weźmij sobie łupy z niego; ale Asael nie chciał od niego ustąpić.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
Tedy po wtóre rzekł Abner do Asaela: Idź precz ode mnie, bym cię snać nie przebił ku ziemi; bo jakoże bym śmiał podnieść twarz moję na Joaba, brata twego?
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
A gdy nie chciał ustąpić, uderzył go Abner końcem włóczni pod piąte żebro, tak iż wyszła włócznia na drugą stronę. Tamże padł, i umarł na onemże miejscu, a wszyscy, którzy przychodzili do onego miejsca, gdzie poległ Asael i umarł, zastanawiali się.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
Wszakże gonili Joab i Abisaj Abnera; i zachodziło słońce, gdy przyszli do pagórka Amma, który jest przeciw Gia na drodze pustyni Gabaońskiej.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
Tedy się zebrali synowie Benjaminowi do Abnera, skupiwszy się w jeden huf, i stanęli na wierzchu jednego pagórka.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
I zawołał Abner na Joaba i rzekł: Izali się na wieki będzie srożył ten miecz? azaż nie wiesz, że na ostatku bywa gorzkość? i dokądże nie rzeczesz ludowi, aby się wrócił od pogoni braci swych?
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
Tedy rzekł Joab: Jako żywy Bóg, byś ty był nie wyzywał, zarazby się był z poranku lud wrócił, każdy od pogoni braci swych.
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
A tak zatrąbił Joab w trąbę i zastanowił się wszystek lud, a nie gonili dalej Izraela, ani się więcej potykali.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
Ale Abner i mężowie jego szli polem całą onę noc, a przeprawiwszy się przez Jordan, przeszli przez wszystko Betoron, aż przyszli do Mahanaim.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
A Joab wróciwszy się z pogoni za Abnerem, zebrał wszystek lud, i nie dostawało mu sług Dawidowych dziewiętnastu mężów, i Asaela.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
Ale słudzy Dawidowi pobili z Benjamińczyków, i z mężów Abnerowych trzy sta i sześćdziesiąt mężów, którzy tam pomarli.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
A wziąwszy Asaela, pogrzebli go w grobie ojca jego, który był w Betlehem; potem szli całą noc Joab i mężowie jego, a na świtaniu przyszli do Hebronu.

< 2 Samweli 2 >