< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
بعد از آن، داوود از خداوند سؤال کرد: «آیا به یکی از شهرهای یهودا برگردم؟» خداوند در پاسخ او فرمود: «بله.» داوود پرسید: «به کدام شهر بروم؟» خداوند جواب داد: «به حِبرون برو.»
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
پس داوود با دو زن خود اخینوعم یزرعیلی و ابیجایل، بیوهٔ نابال کرملی
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
و با همهٔ افرادش و خانواده‌های آنان به حبرون کوچ کرد.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
آنگاه رهبران یهودا نزد داوود آمده، او را در آنجا برای پادشاهی تدهین کردند تا بر سرزمین یهودا حکمرانی کند. داوود چون شنید که مردان یابیش جلعاد شائول را دفن کرده‌اند،
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
برای ایشان چنین پیغام فرستاد: «خداوند شما را برکت دهد زیرا نسبت به پادشاه خود شائول وفاداری خود را ثابت کرده، او را دفن نمودید.
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
خداوند برای این کارتان به شما پاداش بدهد. من نیز به نوبهٔ خود این خوبی شما را جبران خواهم کرد.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
حالا که شائول مرده است، قبیلهٔ یهودا مرا به عنوان پادشاه جدید خود قبول کرده‌اند. پس نترسید و شجاع باشید!»
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
اما ابنیر، پسر نیر، فرماندهٔ سپاه شائول به اتفاق ایشبوشت پسر شائول از رود اردن گذشته، به محنایم فرار کرده بودند.
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
در آنجا ابنیر ایشبوشت را بر جلعاد، اشیر، یزرعیل، افرایم، بنیامین و بقیهٔ اسرائیل پادشاه ساخت.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
ایشبوشت چهل ساله بود که پادشاه اسرائیل شد و دو سال سلطنت کرد. اما قبیلهٔ یهودا داوود را رهبر خود ساختند و داوود در حبرون هفت سال و شش ماه در سرزمین یهودا سلطنت کرد.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
روزی سپاهیان ایشبوشت به فرماندهی ابنیر، پسر نیر، از محنایم به جبعون آمدند.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
سپاهیان داوود نیز به فرماندهی یوآب (پسر صرویه) به مقابلهٔ آنها برآمدند. نیروها در کنار برکهٔ جبعون در مقابل هم قرار گرفتند.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
ابنیر به یوآب گفت: «چطور است چند نفر را از دو طرف به میدان بفرستیم تا با هم بجنگند؟» یوآب موافقت نمود.
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
پس از هر طرف دوازده نفر انتخاب شدند.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
هر یک از آنها با یک دست سر حریف خود را گرفته، با دست دیگر شمشیر را به پهلویش می‌زد، تا اینکه همه مردند. از آن به بعد آن مکان که در جبعون است به «میدان شمشیرها» معروف شد.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
به دنبال این کشتار، جنگ سختی بین دو طرف درگرفت و یوآب و نیروهای داوود، ابنیر و مردان اسرائیل را شکست دادند.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
ابیشای و عسائیل، برادران یوآب نیز در این جنگ شرکت داشتند. عسائیل مثل آهو می‌دوید.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
او به تعقیب ابنیر پرداخت و لحظه‌ای از او چشم برنمی‌داشت.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
ابنیر وقتی سرش را برگرداند و به عقب نگاه کرد، دید عسائیل او را تعقیب می‌کند. او را صدا زده، گفت: «آیا تو عسائیل هستی؟» عسائیل جواب داد: «بله، خودمم.»
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
ابنیر به او گفت: «برو با کسی دیگر بجنگ! سراغ یکی از جوانان برو و خلع سلاحش کن!» اما عسائیل همچنان به تعقیب ابنیر ادامه داد.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
ابنیر بار دیگر فریاد زد: «از تعقیب من دست بردار. اگر تو را بکشم دیگر نمی‌توانم به صورت برادرت یوآب نگاه کنم.»
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
ولی عسائیل دست بردار نبود. پس ابنیر با سر نیزه‌اش چنان به شکم او زد که سر نیزه از پشتش درآمد. عسائیل جابه‌جا نقش بر زمین شد و جان سپرد. هر کس به مکانی که نعش او افتاده بود می‌رسید، می‌ایستاد.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
ولی یوآب و ابیشای به تعقیب ابنیر پرداختند. وقتی به تپهٔ امه نزدیک جیح که سر راه بیابان جبعون است رسیدند، آفتاب غروب کرده بود.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
سپاهیان ابنیر که از قبیلهٔ بنیامین بودند، بر فراز تپهٔ امه گرد آمدند.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
ابنیر، یوآب را صدا زده، گفت: «تا کی می‌خواهی این کشت و کشتار ادامه یابد؟ این کار عاقبت خوشی ندارد. چرا دستور نمی‌دهی افرادت از تعقیب برادران خود دست بکشند؟»
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
یوآب در جواب او گفت: «به خدای زنده قسم، اگر این حرف را نمی‌زدی تا فردا صبح شما را تعقیب می‌کردیم.»
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
آنگاه یوآب شیپورش را زد و مردانش از تعقیب سربازان اسرائیلی دست کشیدند.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
همان شب ابنیر و افرادش برگشته، از رود اردن عبور کردند. آنها تمام صبح روز بعد نیز در راه بودند تا سرانجام به محنایم رسیدند.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
یوآب و همراهانش نیز به خانه برگشتند. تلفات افراد داوود غیر از عسائیل فقط نوزده نفر بود.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
ولی از افراد ابنیر (که همه از قبیلهٔ بنیامین بودند) سیصد و شصت نفر کشته شده بودند.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
یوآب و افرادش، جنازهٔ عسائیل را به بیت‌لحم برده، او را در کنار قبر پدرش به خاک سپردند. بعد، تمام شب به راه خود ادامه داده، سپیدهٔ صبح به حبرون رسیدند.

< 2 Samweli 2 >