< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
Tukun ma inge, David el lolngok nu sin LEUM GOD, “Ku nga ac som sruokya sie siti in acn Judah?” LEUM GOD El topuk, “Aok.” David el siyuk, “Acn ya se?” LEUM GOD El fahk, “Hebron.”
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
Ouinge David el som nu Hebron, ac el us mutan luo kial: Ahinoam sie mutan Jezreel, ac Abigail sie mutan Carmel su katinmas kial Nabal.
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
El oayapa us mwet lal wi sou lalos, ac elos muta ke siti srisrik raunela acn Hebron.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
Na mwet Judah elos tuku nu Hebron ac mosrwella David elan tokosra lun Judah. Ke David el lohng lah mwet Jabesh in Gilead elos piknilya Saul,
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
el supwala kutu mwet nu we wi kas inge: “Lela LEUM GOD Elan akinsewowoye kowos ke kowos akkalemye nunak pwaye lowos nu sin tokosra lowos ac piknilya.
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
Ac inge lela LEUM GOD Elan kulang ac oaru in liyekowosyang. Nga pac, nga fah oru wo nu suwos ke sripen ma kowos oru inge.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
Kowos in ku ac pulaik! Saul, tokosra lowos, el misa, ac mwet Judah elos mosrweyula in tokosra lalos.”
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
Abner wen natul Ner, su captain lun un mwet mweun lal Saul, el eisal Ishbosheth wen natul Saul, ac kaingla tupalla Infacl Jordan nu Mahanaim.
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
In acn se inge Abner el orala Ishbosheth elan tokosra lun acn Gilead, Asher, Jezreel, Ephraim, ac Benjamin — aok lun Israel nufon.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
Ishbosheth el yac angngaul ke pacl se el tokosrala lun Israel, ac el leum faclos ke yac luo. A sruf lun Judah srakna orekma nu sel David,
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
ac el leum in acn Hebron fin mwet Judah ke yac itkosr tafu.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
Abner ac mwet pwapa lal Ishbosheth elos som liki Mahanaim nu in siti Gibeon.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
Joab, su nina kial ah pa Zeruiah, ac mwet pwapa saya lal David elos osun nu selos ke lulu in kof in acn Gibeon. Elos nukewa muta in acn sac — sie u ah muta ke la lulu sac, ac u se ngia muta ke layen ngia.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
Na Abner el fahk nu sel Joab, “Kut srukak kutu mwet fusr ke u luo inge elos in akutun anwuk.” Joab el fahk, “Wona.”
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
Ouinge mwet singoul luo sin mwet lal Ishbosheth ac sruf lal Benjamin, elos lain mwet singoul luo sin mwet lal David.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
Kais sie mwet sruokya mwet se lainul ke sifal, ac kaskeang cutlass natul ah nu in pupal. Ouinge mwet longoul akosr ah nufon putatla misa. Na pa pangpang acn se inge in acn Gibeon “Ima in Cutlass.”
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
Na mweun na upa se srola, ac David ac mwet lal elos kutangulla Abner ac mwet Israel.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
Wen tolu natul Zeruiah oasr kac: Joab, Abishai, ac Asahel. Asahel, su kasrusr mui oana deer inima soko,
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
el ukwal Abner suwosyang tokol.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
Abner el tapulla siyuk, “Asahel, ya kom pa ingan?” El topuk, “Aok, nga.”
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
Na Abner el fahk, “Nimet ukweyu! Ukwe na sie mwet mweun saya an ac eisla ma el us an.” A Asahel el ukwal na.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
Na Abner el sifil fahk nu sel, “Tui! Nimet ukweyu! Kom ku oru ngan unikomi? Nga ac ngetnget fuka nu sel Joab, ma lim?”
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
Tuh Asahel el tiana tui. Na Abner el fakfuk nu tok ac fakisya insial Asahel, ac osra soko ah sasla fintokol. Asahel el putatla nu infohk uh ac misa. Ac mwet nukewa su tuku nu yen se el oan we ah elos tui in acn sac.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
Na Joab ac Abishai eltal mutawauk ukwal Abner, ac ke faht uh tili eltal sun fineol srisrik Ammah, su oan nu kutulap in acn Giah ke inkanek nu yen mwesis lun Gibeon.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
Mwet in sruf lal Benjamin sifilpa fahsreni in welul Abner, ac elos tu na akola fin eol soko.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
Na Abner el pangla nu yorol Joab ac fahk, “Ku kut ac kollana mweun lasr uh nwe ngac? Mea, kom tia akilen lah saflaiya uh kut ac arulana asrungai? Kut mutunfacl sefanna. Kut ac soano nwe ngac kom in sap mwet lom an in tui tila ukwe kut?”
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
Ac Joab el fahk, “Nga fulahk Inen God moul, lah kom funu tia kasla, mwet luk uh lukun ukwe kowos na nwe lututang.”
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
Na Joab el ukya mwe ukuk tuh mwet lal ah in tui ac tila ukwe mwet Israel ah. Ouinge mweun sac tui.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
Abner ac mwet lal elos fahsr sasla Infahlfal Jordan in fong fon sac. Elos tupalla Infacl Jordan, ac tukun fahsr lalos in lotu se tok ah nufon, elos sun acn Mahanaim.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
Ke Joab el tulokinya mwet lal ah, el konauk tuh na mwet singoul eu wanginla, sayal Asahel.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
Mwet lal David uniya mwet tolfoko onngoul sin mwet lal Abner ke sruf lal Benjamin.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
Joab ac mwet lal elos us manol Asahel ac pikinya inkulyuk lun sou lal ah in acn Bethlehem. Na elos fahsr in fong sac nufon nwe sun acn Hebron in lotu tok ah.

< 2 Samweli 2 >