< 2 Samweli 2 >

1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
Some time after that, David asked Yahweh, “Should I go back to [live in] one of the towns in Judah?” Yahweh replied, “Yes, go up there.” Then David asked, “To which town should I go?” Yahweh replied, “To Hebron.”
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
So David went up there, taking his two wives, Ahinoam who was from Jezreel [city], and Abigail, the widow of Nabal from Carmel [city].
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
He also took the men who had been with him, and their families. They all started to live in villages near Hebron.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
Then the men of Judah came to Hebron, and [one of] them poured olive oil on David’s head [to show they were appointing him to be] [MTY] the king of the tribe [MTY] of Judah. When David found out that the people of Jabesh [town] in [the] Gilead [region] had buried Saul’s body,
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
he sent messengers to the men of Jabesh to tell them this: “I desire/hope that Yahweh will bless you for having shown, by burying the body of Saul your king, that you were loyal to him.
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
Now I also desire/hope that Yahweh will faithfully love you and be loyal to you. And I will do good things for you because of what you have done [for Saul].
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
Now, although Saul your king is dead, be strong and courageous, like the people of Judah, who have appointed me to be their king.”
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
[While this was happening], Ner’s son Abner, the commander of Saul’s army, took Saul’s son Ishbosheth and went across [the Jordan River] to Mahanaim [town].
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
There Abner proclaimed that Ishbosheth was now the king of [the] Gilead [region] and of the tribe of Asher and the region of Jezreel and the tribes of Ephraim and Benjamin. That meant that he was the king of all of the people of Israel.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
Ishbosheth was 40 years old when he started to rule over the people of Israel. He ruled them for two years. But the tribe of Judah (was loyal to David/wanted David to be their king),
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
and he ruled them for seven and a half years while he was living in Hebron.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
[One day] Abner and the officials of Isbosheth went from Mahanaim [across the Jordan River] to Gibeon [city].
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
Joab, whose mother was Zeruiah, and some of David’s officials [went from Hebron to Gibeon, and] met at the pool there. They all sat down, the one group on one side of the pool and the other group on the other side.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
Abner said to Joab, “Let’s tell some of our young men to fight each other!” Joab replied, “Okay!”
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
So twelve men from the tribe of Benjamin fought for Ishbosheth, against twelve of David’s soldiers.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
Each of them grabbed the head of the man against whom he was fighting, and thrust his sword into that man’s side. The result was that all 24 of them fell down dead. So that area in Gibeon is now called ‘Field of Swords’.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
Then [the others started to fight]. It was a very fierce battle. Abner and the men of Israel were defeated by David’s soldiers.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
Zeruiah’s three sons were there [on that day]: Joab, Abishai, and Asahel. Asahel was able to run very fast; he could run as fast as a wild gazelle/antelope.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
Asahel started to pursue Abner. He ran straight toward Abner, without stopping.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
Abner looked behind him, and said “Is that you, Asahel?” Asahel replied, “Yes!”
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
Abner yelled at him, “Turn to one side or the other, [and pursue someone else]!” But Asahel would not stop pursuing Abner.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
So Abner yelled at him again, “Stop (chasing after/pursuing) me! (Why should I kill you?/It would not be good for me to kill you!) [RHQ] If I did that, (how could I (face/be reconciled with) your brother Joab?/it would be very difficult for me to (face/be reconciled with) your brother Joab.) [RHQ]”
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
But Asahel refused to stop pursuing Abner. So Abner [suddenly turned and] thrust the butt end of his spear into Asahel’s stomach. Because he thrust it very strongly, that end of the spear [went though Asahel’s body and] came out at his back, and he fell to the ground, dead. All the other soldiers who came to the place where his body was lying stopped and stood there, [stunned].
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
But Joab and Abishai continued to pursue Abner. At sunset they came to Ammah Hill, which is east of Giah, along the road to the desert near Gibeon.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
The men from the tribe of Benjamin gathered around Abner in one group, and stood at the top of a hill.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
Then Abner called out to Joab, saying “Are we going to continue to fight forever [RHQ]? Do you not realize that [if we continue fighting], the result will be very bad [RHQ]? We are all descendants of Jacob. [So we should stop fighting each other] (How long will it be until you tell your soldiers to stop pursuing us?/Tell your soldiers to stop pursuing us.)” [RHQ]
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
Joab replied, “Just as surely as God lives, if you had not said that, my soldiers would have continued pursuing your men until tomorrow morning!”
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
So Joab blew a trumpet [to signal that they should stop fighting]. So all his men did that. They did not pursue the soldiers of Israel any more, and they stopped fighting.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
That night Abner and his soldiers went through the Jordan [River] Valley. They crossed the Jordan [River] and marched all the next morning, and they finally arrived at Mahanaim.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
Joab [and his soldiers] stopped pursuing Abner. And when he gathered all his soldiers together, he found out that in addition to Asahel, only 19 of them had been killed in the battle.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
But David’s soldiers had killed 360 of Abner’s men, all from the tribe of Benjamin.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
[Some of Joab’s soldiers] took Asahel’s body and buried it in the tomb where his father had been buried, in Bethlehem. Then they marched all during the night, and at dawn they arrived [back home] at Hebron.

< 2 Samweli 2 >