< 2 Samweli 2 >
1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
And it was after thus and he enquired David by Yahweh - saying ¿ will I go up in one of [the] cities of Judah and he said Yahweh to him go up and he said David where? will I go up and he said Hebron towards.
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
And he went up there David and also [the] two wives his Ahinoam the Jezreelite [woman] and Abigail [the] wife of Nabal the Carmelite.
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
And men his who [were] with him he brought up David each man and household his and they dwelt in [the] cities of Hebron.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
And they came [the] people of Judah and they anointed there David to king over [the] house of Judah and people told to David saying [the] men of Jabesh Gilead who they buried Saul.
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
And he sent David messengers to [the] people of Jabesh Gilead and he said to them [be] blessed you by Yahweh that you have done the loyalty this with lord your with Saul and you have buried him.
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
And now may he do Yahweh with you covenant loyalty and faithfulness and also I I will do with you the good this that you have done the thing this.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
And now - let them be strong hands your and become sons of strength for he has died lord your Saul and also me they have anointed [the] house of Judah to king over them.
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
And Abner [the] son of Ner [the] commander of [the] army which [belonged] to Saul he had taken Ish-bosheth [the] son of Saul and he had brought over him Mahanaim.
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
And he made king him to Gilead and to the Ashurite[s] and to Jezreel and over Ephraim and over Benjamin and over Israel all of it.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
[was] a son of Forty year[s] Ish-bosheth [the] son of Saul when became king he over Israel and two years he reigned only [the] house of Judah they were after David.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
And it was [the] number of the days which he was David king in Hebron over [the] house of Judah seven years and six months.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
And he went out Abner [the] son of Ner and [the] servants of Ish-bosheth [the] son of Saul from Mahanaim Gibeon towards.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
And Joab [the] son of Zeruiah and [the] servants of David they went out and they met them at [the] pool of Gibeon together and they sat down these [men] at the pool from this and these [men] at the pool from this.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
And he said Abner to Joab let them arise please the young men and let them play before us and he said Joab let them arise.
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
And they arose and they passed by by number two [plus] ten for Benjamin and for Ish-bosheth [the] son of Saul and two [plus] ten from [the] servants of David.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
And they took hold each - on [the] head of neighbor his and sword his [was] in [the] side of neighbor his and they fell together and someone called the place that Helkath Hazzurim which [is] in Gibeon.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
And it was the battle severe up to muchness on the day that and he was defeated Abner and [the] men of Israel before [the] servants of David.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
And they were there three [the] sons of Zeruiah Joab and Abishai and Asahel and Asahel [was] swift on feet his like one of the gazelles which [are] in the open country.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
And he pursued Asahel after Abner and not he turned aside to go to the right and to the left from after Abner.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
And he turned Abner behind him and he said ¿ you [is] this O Asahel and he said I.
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
And he said to him Abner turn aside for yourself to right your or to left your and seize for yourself one from the young men and take for yourself spoils his and not he was willing Asahel to turn aside from after him.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
And he repeated again Abner to say to Asahel turn aside for yourself from after me why? will I strike you [the] ground towards and how? will I lift up face my to Joab brother your.
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
And he refused to turn aside and he struck him Abner with [the] back end of the spear into the belly and it went out the spear from behind him and he fell there and he died (in place his *Q(K)*) and it was every [one] who came to the place where he fell there Asahel and he died and they stood still.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
And they pursued Joab and Abishai after Abner and the sun it set and they they came to [the] hill of Ammah which [is] on [the] face of Giah [the] way of [the] wilderness of Gibeon.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
And they gathered together [the] descendants of Benjamin behind Abner and they became a band one and they stood on [the] top of a hill one.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
And he called out Abner to Joab and he said ¿ to perpetuity will it devour [the] sword ¿ not do you know? that bitter it will be at the last and until when? not will you say to the people to turn back from after brothers their.
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
And he said Joab [by] [the] life of God if if not you had spoken for then from the morning it had abandoned pursuit the people each from after brother his.
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
And he gave a blast Joab on the trumpet and they stood all the people and not they pursued again after Israel and not they repeated again to wage war.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
And Abner and men his they went in the Arabah all the night that and they passed over the Jordan and they went all Bitron and they came Mahanaim.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
And Joab he returned from after Abner and he gathered all the people and they were missed of [the] servants of David nine-teen man and Asah-el.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
And [the] servants of David they had struck down of Benjamin and among [the] men of Abner three hundred and sixty man they had died.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
And people lifted up Asahel and they buried him in [the] tomb of father his which [was] Beth-lehem and they went all the night Joab and men his and it became light for them at Hebron.