< 2 Samweli 2 >
1 Ikawa baada ya mambo haya, Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nipande kwenda katika mojawapo ya miji ya Yuda?” Bwana akasema, “Panda.” Daudi akauliza, “Je, niende wapi?” Bwana akajibu, “Nenda Hebroni.”
And so, after these things, David consulted the Lord, saying, “Shall I ascend to one of the cities of Judah?” And the Lord said to him, “Ascend.” And David said, “To where shall I ascend?” And he responded to him, “To Hebron.”
2 Basi Daudi akakwea kwenda huko pamoja na wake zake wawili, Ahinoamu wa Yezreeli na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
Therefore, David ascended with his two wives, Ahinoam, the Jezreelite, and Abigail, the wife of Nabal of Carmel.
3 Pia Daudi akawachukua watu waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na jamaa yake, nao wakaishi huko Hebroni na miji yake.
And as for the men who were with him, David led forth each man with his household. And they stayed in the towns of Hebron.
4 Ndipo watu wa Yuda wakaja Hebroni, huko wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda. Daudi alipoambiwa kuwa ni watu wa Yabeshi-Gileadi waliomzika Sauli,
And the men of Judah went and anointed David there, so that he would reign over the house of Judah. And it was reported to David that the men of Jabesh Gilead had buried Saul.
5 akatuma wajumbe kwa watu wa Yabeshi-Gileadi kuwaambia, “Bwana awabariki kwa kuonyesha wema huu kwa kumzika Sauli bwana wenu.
Therefore, David sent messengers to the men of Jabesh Gilead, and he said to them: “Blessed are you to the Lord, who has accomplished this mercy with your lord Saul, so that you would bury him.
6 Sasa Bwana na awaonyeshe wema na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema ule ule kwa kuwa mmefanya jambo hili.
And now, certainly, the Lord will repay to you mercy and truth. But I also will act with favor, because you have accomplished this word.
7 Sasa basi, kuweni hodari na mashujaa, kwa maana bwana wenu Sauli amekufa, nayo nyumba ya Yuda imenitia mafuta niwe mfalme juu yao.”
Let your hands be strengthened, and be sons of fortitude. For even though your lord Saul has died, still the house of Judah has anointed me as king over them.”
8 Wakati huo Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi la Sauli, alikuwa amemchukua Ish-Boshethi mwana wa Sauli na kumleta hadi Mahanaimu.
Then Abner, the son of Ner, the leader of the army of Saul, took Ishbosheth, the son of Saul, and he led him around, throughout the camp.
9 Akamweka awe mfalme juu ya nchi ya Gileadi, Waasheri, Yezreeli, Efraimu, Benyamini na Israeli yote.
And he appointed him as king over Gilead, and over Geshuri, and over Jezreel, and over Ephraim, and over Benjamin, and over all of Israel.
10 Ish-Boshethi mwana wa Sauli alikuwa na umri wa miaka arobaini alipoanza kutawala Israeli, naye akatawala miaka miwili. Hata hivyo, nyumba ya Yuda ikamfuata Daudi.
Ishbosheth, the son of Saul, was forty years old when he had begun to rule over Israel. And he reigned for two years. For only the house of Judah followed David.
11 Muda ambao Daudi alikuwa mfalme juu ya nyumba ya Yuda huko Hebroni ilikuwa miaka saba na miezi sita.
And the number of the days, during which David was staying and ruling in Hebron over the house of Judah, was seven years and six months.
12 Abneri mwana wa Neri, pamoja na watu wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu kwenda Gibeoni.
And Abner, the son of Ner, and the youths of Ishbosheth, the son of Saul, went out from the camp to Gibeon.
13 Yoabu mwana wa Seruya na watu wa Daudi wakatoka na kukutana nao kwenye bwawa la Gibeoni. Kikundi kimoja kiliketi upande mmoja wa bwawa, na kikundi kingine upande wa pili.
Therefore, Joab, the son of Zeruiah, and the youths of David, went out and met them beside the pool of Gibeon. And when they had convened together, they sat down opposite one another: these on one side of the pool, and those on the other side.
14 Ndipo Abneri akamwambia Yoabu, “Tuwaweke baadhi ya vijana wasimame na wapigane ana kwa ana mbele yetu.” Yoabu akasema, “Sawa, na wafanye hivyo.”
And Abner said to Joab, “Let the youths rise up and play before us.” And Joab answered, “Let them rise up.”
15 Kwa hiyo vijana wakasimama, wakahesabiwa: watu wa Benyamini na wa Ish-Boshethi mwana wa Sauli kumi na wawili, na upande wa Daudi kumi na wawili.
Therefore, they rose up and crossed over, twelve in number of Benjamin, from the side of Ishbosheth, the son of Saul, and twelve of the youths of David.
16 Kisha kila mtu akakamatana na mpinzani wake kichwani na kuchomana kwa upanga, nao wakaanguka chini pamoja. Kwa hiyo mahali pale katika Gibeoni pakaitwa Helkath-Hasurimu.
And each one, taking hold of his peer by the head, fixed a sword into the side of his adversary, and they fell down together. And the name of that place was called: The Field of the Valiant in Gibeon.
17 Siku hiyo vita vilikuwa vikali sana, naye Abneri na watu wa Israeli wakashindwa na watu wa Daudi.
And a very harsh war rose up on that day. And Abner, with the men of Israel, was put to flight by the youths of David.
18 Wana watatu wa Seruya walikuwako huko: nao ni Yoabu, Abishai na Asaheli. Basi huyo Asaheli alikuwa na mbio kama paa.
Now the three sons of Zeruiah were in that place: Joab, and Abishai, and Asahel. And Asahel was a very swift runner, like one of the deer that lives in the forest.
19 Asaheli akamfukuza Abneri, pasipo kugeuka kulia wala kushoto wakati akimfuata.
And Asahel pursued Abner, and he did not turn aside to the right, nor to the left, to cease in the pursuit of Abner.
20 Abneri akaangalia nyuma na kumuuliza, “Ni wewe, Asaheli?” Akamjibu, “Ndiyo.”
And so, Abner looked behind his back, and he said, “Are you not Asahel?” And he responded, “I am.”
21 Ndipo Abneri akamwambia, “Geuka upande wa kulia au kushoto. Mchukue mmoja wa vijana wa kiume na umvue silaha zake.” Lakini Asaheli hakuacha kumfukuza.
And Abner said to him, “Go to the right, or to the left, and apprehend one of the youths, and take his spoils for yourself.” But Asahel was not willing to cease from pursuing him closely.
22 Abneri akamwonya tena Asaheli akimwambia, “Acha kunifukuza! Kwa nini nikuue? Je, nitawezaje kumtazama ndugu yako Yoabu usoni?”
And again, Abner said to Asahel: “Withdraw, and do not choose to follow me. Otherwise, I will be compelled to stab you to the ground, and I will not be able to lift up my face before your brother, Joab.”
23 Lakini Asaheli alikataa kuacha kumfuatia, kwa hiyo Abneri akamchoma Asaheli tumboni kwa ncha butu ya mkuki wake, mkuki ukamtoboa ukatokea mgongoni mwake. Akaanguka na kufa papo hapo. Ikawa kila mtu alisimama alipofika mahali pale Asaheli alipoanguka na kufa.
But he disdained to heed him, and he was not willing to turn aside. Therefore, turning, Abner struck him with his spear in the groin, and he pierced him through, and he died in the same place. And all those who would pass by the place, in which Asahel had fallen and died, would stand still.
24 Lakini Yoabu na Abishai walimfuata Abneri, na jua lilipokuwa linatua, wakafika kwenye kilima cha Ama, karibu na Gia kwenye njia ya kuelekea kwenye nyika ya Gibeoni.
Now while Joab and Abishai were pursuing Abner as he fled, the sun set. And they went as far as the Hill of the Aqueduct, which is opposite the valley on the way of the desert in Gibeon.
25 Ndipo watu wa kabila la Benyamini wakakusanyika tena nyuma ya Abneri. Wakaunda kikosi na kujiimarisha juu ya kilima.
And the sons of Benjamin gathered themselves to Abner. And being joined in one battle line, they stood at the summit of a hill.
26 Abneri akamwita Yoabu, akamwambia, “Je, ni lazima upanga uendelee kuangamiza milele? Hutambui kwamba jambo hili litaishia katika uchungu? Utaacha kuwaagiza watu wako waache kuwafuatilia ndugu zao hata lini?”
And Abner cried out to Joab, and he said: “Will your sword rage unto utter destruction? Are you ignorant that it is perilous to act in desperation? How long will you not tell the people to cease from the pursuit of their brothers?”
27 Yoabu akajibu, “Hakika kama aishivyo Mungu, kama hukusema, hawa watu wangeendelea kuwafuatia ndugu zao mpaka asubuhi.”
And Joab said: “As the Lord lives, if you had spoken in the morning, the people would have withdrawn from pursuing their brothers.”
28 Basi Yoabu akapiga tarumbeta, nao watu wote wakasimama, hawakuwafuata Israeli tena, wala hawakuwapiga tena.
Therefore, Joab sounded the trumpet, and the entire army stood still, and they did not pursue after Israel any more, and they did not engage in conflict.
29 Usiku ule wote Abneri na watu wake wakatembea kupitia Araba. Wakavuka Mto Yordani, wakaendelea wakipitia nchi yote ya Bithroni wakafika Mahanaimu.
Then Abner and his men went away, all that night, through the plains. And they crossed the Jordan, and having roamed throughout all of Beth-horon, they arrived in the camp.
30 Basi Yoabu akarudi kutoka kumfuatia Abneri, na kuwakusanya watu wake wote. Pamoja na Asaheli, watu kumi na tisa wa Daudi walikuwa wamepotea.
But Joab, returning after he had released Abner, gathered together all the people. And of David’s youths, they were missing nineteen men, aside from Asahel.
31 Lakini watu wa Daudi walikuwa wamewaua watu wa kabila la Benyamini 360 waliokuwa pamoja na Abneri.
But of Benjamin and of the men who were with Abner, the servants of David had struck three hundred and sixty, who also died.
32 Wakamchukua Asaheli, wakamzika katika kaburi la baba yake huko Bethlehemu. Kisha Yoabu na watu wake wakatembea usiku kucha na kufika huko Hebroni wakati wa mapambazuko.
And they took Asahel, and they buried him in the sepulcher of his father at Bethlehem. And Joab, and the men who were with him, walked throughout the night, and they arrived in Hebron at the very break of day.