< 2 Samweli 18 >

1 Daudi akakusanya watu aliokuwa nao na kuweka majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
Davut kendini destekleyen askerleri bir araya topladı. Onlara binbaşılar ve yüzbaşılar atadı.
2 Daudi akatuma vikosi vya askari: theluthi moja ilikuwa chini ya amri ya Yoabu, theluthi ya pili chini ya Abishai mwana wa Seruya nduguye Yoabu, na theluthi ya tatu chini ya Itai, Mgiti. Mfalme akaviambia vikosi, “Hakika mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nanyi.”
Sonra orduyu Seruya oğlu Yoav'ın, kardeşi Avişay'ın ve Gatlı İttay'ın denetiminde üç kol halinde gönderdi. Kral askerlere, “Ben de sizinle birlikte gideceğim” dedi.
3 Lakini watu wakasema, “Haikupasi kwenda, ikiwa sisi tutalazimika kukimbia, wao hawatatujali. Hata kama nusu yetu tukifa hawatajali, lakini wewe una thamani ya watu kama sisi kumi elfu. Ingekuwa bora zaidi kwako basi kutupatia msaada kutoka mjini.”
Ancak askerler, “Bizimle gelmemelisin” diye karşılık verdiler, “Çünkü kaçmak zorunda kalırsak düşmanlarımız bizi umursamaz; yarımız ölse bile umursamazlar. Sen bizim gibi on bin adama değersin. Sen kentten bize yardım et, daha iyi.”
4 Mfalme akajibu, “Nitafanya lolote linaloonekana jema zaidi kwenu.” Kwa hiyo mfalme akasimama kando ya lango wakati watu wote wakitoka nje kwa makundi ya mamia na maelfu.
Kral, “Gözünüzde iyi olanı yapacağım” dedi. Adamları yüzer ve biner kişilik birlikler halinde kentten çıkarken kral kapının yanında duruyordu.
5 Mfalme akawaamuru Yoabu, Abishai na Itai, “Kuweni wapole kwa kijana Absalomu kwa ajili yangu.” Vikosi vyote vikasikia mfalme akitoa amri kwa kila jemadari kumhusu Absalomu.
Kral, Yoav'a, Avişay'a ve İttay'a, “Benim hatırım için genç Avşalom'a sert davranmayın” diye buyurdu. Bütün askerler kralın komutanlara Avşalom'a ilişkin buyruk verdiğini duydular.
6 Jeshi likatoka kwenda kwenye uwanja wa vita kupigana na Israeli, hivyo vita vikapiganwa katika msitu wa Efraimu.
Davut'un ordusu İsrailliler'le savaşmak üzere tarlalara çıktı. Savaş Efrayim Ormanı'nda başladı.
7 Huko jeshi la Israeli likashindwa na watu wa Daudi, siku hiyo majeruhi walikuwa wengi kiasi cha watu ishirini elfu.
İsrail ordusu Davut'un adamları önünde yenilgiye uğradı. Büyük bir kırım oldu. O gün yirmi bin kişi öldü.
8 Vita vikaenea nchi nzima, watu wengi zaidi wakifia msituni siku hiyo kuliko waliouawa kwa upanga.
Savaş her yana yayıldı. O gün ormanda yok olanların sayısı kılıçtan geçirilenlerin sayısından daha çoktu.
9 Basi ikawa Absalomu alikutana na watu wa Daudi. Yeye alikuwa amepanda nyumbu wake, naye nyumbu alipopita chini ya matawi yaliyosongana ya mwaloni mkubwa, kichwa cha Absalomu kilinaswa kwenye mti. Akaachwa akiningʼinia hewani, wakati nyumbu aliyekuwa amempanda aliendelea kwenda.
Avşalom ansızın Davut'un adamlarıyla karşılaştı. Avşalom katıra binmişti. Katır büyük bir yabanıl fıstık ağacının sık dalları altından geçerken, Avşalom'un başı dallara takıldı. Katır yoluna devam edince, Avşalom havada asılı kaldı.
10 Mmojawapo wa wale watu alipoona, akamwambia Yoabu, “Nimemwona Absalomu akiningʼinia kwenye mti wa mwaloni.”
Adamlardan biri bunu gördü. Yoav'a, “Avşalom'u bir yabanıl fıstık ağacına asılı gördüm” diye bildirdi.
11 Yoabu akamwambia huyo mtu, “Nini! Ulimwona Absalomu? Kwa nini hukumpiga papo hapo mpaka chini? Ndipo ningekupa shekeli kumi za fedha na mkanda wa askari shujaa.”
Yoav, haberi verene, “Onu gördün mü? Neden onu orada öldürmedin? Sana on parça gümüşle bir kemer verirdim” dedi.
12 Lakini huyo mtu akamjibu Yoabu, “Hata kama ningepimiwa shekeli 1,000 mikononi mwangu, nisingeinua mkono wangu dhidi ya mwana wa mfalme. Tukiwa tunasikia, mfalme alikuagiza wewe na Abishai pamoja na Itai, akisema, ‘Mlindeni kijana Absalomu kwa ajili yangu.’
Ama adam, “Elime bin parça gümüş saysan bile, kralın oğluna elimi kaldırmam” diye yanıtladı, “Çünkü kralın sana, Avişay'a ve İttay'a, ‘Benim hatırım için genç Avşalom'u koruyun’ diye buyruk verdiğini duyduk.
13 Nami kama ningekuwa nimemtendea kwa hila, na hakuna lolote linalofichika kwa mfalme, wewe mwenyewe ungejitenga nami.”
Oysa Avşalom'u öldürseydim –hiçbir şey kraldan gizli kalmaz– o zaman sen de beni savunmazdın.”
14 Yoabu akasema, “Mimi sitapoteza muda hapa pamoja nawe.” Hivyo akachukua mikuki mitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu nayo moyoni alipokuwa angali hai akiningʼinia katika ule mwaloni.
Yoav, “Seninle böyle vakit kaybedemem” dedi. Üç kargı aldı, yabanıl fıstık ağacında asılı duran ve hâlâ sağ olan Avşalom'un yüreğine sapladı.
15 Nao wabeba silaha kumi wa Yoabu wakamzunguka Absalomu, wakampiga na kumuua.
Bunun üzerine Yoav'ın silahlarını taşıyan on genç Avşalom'un çevresini sarıp onu öldürdüler.
16 Kisha Yoabu akapiga tarumbeta, navyo vikosi vikaacha kuwafuata Israeli, kwa maana Yoabu aliwasimamisha.
Yoav boru çaldırınca, askerler İsrailliler'i kovalamayı bırakıp geri döndüler. Yoav onların savaşı sürdürmelerine engel oldu.
17 Wakamchukua Absalomu, wakamtupa katika shimo kubwa huko msituni na kulundika lundo kubwa la mawe juu yake. Huko nyuma, Waisraeli wote wakakimbilia nyumbani kwao.
Yoav'ın askerleri Avşalom'u alıp ormanda derin bir çukura attılar; üzerine büyük bir taş yığını yaptılar. Bütün İsrailliler evlerine kaçtılar.
18 Wakati wa uhai wa Absalomu alikuwa amechukua nguzo na kuisimamisha katika Bonde la Mfalme, kwa maana alifikiri, “Sina mwana atakayeendeleza kumbukumbu ya jina langu.” Akaita nguzo hiyo kwa jina lake mwenyewe. Nayo inaitwa Mnara wa Ukumbusho wa Absalomu mpaka leo.
Avşalom daha sağken bir direk alıp kendisi için Kral Vadisi'ne dikmişti. Çünkü, “Adımı anımsatacak bir oğlum yok” diye düşünmüştü. Direğe kendi adını vermişti. Bu direk bugün de Avşalom Anıtı diye bilinir.
19 Basi Ahimaasi mwana wa Sadoki akasema, “Niruhusu mimi nikimbie na kumpelekea mfalme habari kwamba Bwana amemwokoa mfalme kutoka mikononi mwa adui zake.”
Sadok oğlu Ahimaas Yoav'a, “İzin ver de koşup krala RAB'bin onu düşmanlarının elinden kurtardığını haber vereyim” dedi.
20 Yoabu akamwambia Ahimaasi, “Leo si wewe utakayepeleka habari. Unaweza kupeleka habari wakati mwingine, lakini leo haikupasi kupeleka, kwa sababu mwana wa mfalme amekufa.”
Yoav, “Olmaz, bugün haberi götüren sen olmayacaksın” dedi, “Başka bir zaman haber götürürsün, ama bugün değil. Çünkü kralın oğlu öldü.”
21 Ndipo Yoabu akamwambia mtu mmoja Mkushi, “Nenda, ukamwambie mfalme kile ulichoona.” Mkushi akasujudu mbele ya Yoabu akaondoka mbio.
Sonra bir Kûşlu'ya, “Sen git, gördüklerini krala bildir” dedi. Kûşlu Yoav'ın önünde yere kapandı, sonra koşmaya başladı.
22 Ahimaasi mwana wa Sadoki akamwambia tena Yoabu, “Liwalo na liwe, tafadhali niruhusu nikimbie nyuma ya huyo Mkushi.” Lakini Yoabu akajibu, “Mwanangu, mbona wataka kwenda? Wewe huna habari yoyote itakayokupa tuzo.”
Ama Sadok oğlu Ahimaas yine, “Ne olursa olsun, izin ver, ben de Kûşlu'nun ardısıra koşayım” dedi. Yoav, “Oğlum, neden koşmak istiyorsun?” dedi, “Sana ödül kazandıracak bir haberin yok ki!”
23 Ahimaasi akasema, “Liwalo na liwe, nataka kukimbia.” Kwa hiyo Yoabu akamwambia, “Haya, kimbia!” Ndipo Ahimaasi akakimbia kufuata njia ya kupitia tambarare, akafika kabla ya huyo Mkushi.
Ahimaas, “Ne olursa olsun koşacağım” diye karşılık verdi. Yoav, “Koş öyleyse” dedi. Böylece Ahimaas Şeria Ovası yolundan koşarak Kûşlu'yu geçti.
24 Wakati Daudi alipokuwa ameketi kati ya lango la ndani na la nje, mlinzi akapanda juu ya paa la lango kupitia ukutani. Alipotazama nje, akaona mtu mmoja akikimbia peke yake.
Davut kentin iç ve dış kapıları arasında oturuyordu. Nöbetçi surun yanındaki kapının tepesine çıktı. Çevreye göz gezdirince, tek başına koşan birini gördü.
25 Mlinzi akampazia mfalme sauti na kumpa taarifa. Mfalme akasema, “Ikiwa yuko peke yake, lazima atakuwa na habari njema.” Naye yule mtu akazidi kusogea karibu.
Krala seslenerek gördüğünü bildirdi. Kral, “Tek başına geliyorsa, iyi haber getiriyor demektir” dedi. Adam gitgide yaklaşıyordu.
26 Kisha mlinzi akaona mtu mwingine anakuja akikimbia, akamwita bawabu, “Tazama, mtu mwingine anakuja akikimbia peke yake!” Mfalme akasema, “Lazima atakuwa analeta habari njema pia.”
Nöbetçi koşan başka birini görünce, kapıcıya, “İşte tek başına koşan bir adam daha!” diye seslendi. Kral, “O da iyi haber getiriyor” dedi.
27 Mlinzi akasema, “Ninaona kuwa yule wa kwanza anakimbia kama Ahimaasi mwana wa Sadoki.” Mfalme akasema, “Yeye ni mtu mwema. Analeta habari njema.”
Nöbetçi, “Sanırım birinci adamın koşuşu Sadok oğlu Ahimaas'ın koşuşuna benziyor” dedi. Kral, “Ahimaas iyi adamdır” diye karşılık verdi, “İyi haberle gelir.”
28 Ndipo Ahimaasi akamwita mfalme, akasema, “Mambo yote ni mema!” Akasujudu mbele ya mfalme uso wake mpaka ardhini, akasema, “Ahimidiwe Bwana Mungu wako! Yeye aliyewatoa watu wale walioinua mikono yao dhidi ya mfalme bwana wangu.”
Ahimaas krala, “Her şey yolunda!” diye seslendi. Kralın önünde yüzüstü yere kapanarak, “Efendimiz krala el kaldıranları teslim eden Tanrın RAB'be övgüler olsun!” dedi.
29 Mfalme akauliza, “Je, huyo kijana Absalomu yuko salama?” Ahimaasi akajibu, “Kulikuwa na machafuko mengi mara tu Yoabu alipokuwa anataka kumtuma mtumishi wa mfalme pamoja nami mtumishi wako, lakini sijui ilikuwa nini?”
Kral, “Genç Avşalom güvenlikte mi?” diye sordu. Ahimaas şöyle yanıtladı: “Yoav kralın hizmetkârı Kûşlu'yla beni gönderdiği sırada büyük bir karışıklık gördüm, ama ne olduğunu anlamadım.”
30 Mfalme akasema, “Simama kando na usubiri hapa.” Basi akasogea kando na kusimama hapo.
Kral, “Bir yana çekilip burada bekle” dedi. Ahimaas da çekilip beklemeye başladı.
31 Ndipo huyo Mkushi akawasili na kusema, “Mfalme bwana wangu, sikia habari njema! Leo Bwana amekuokoa kutoka kwa wale wote walioinuka dhidi yako.”
Tam o sırada Kûşlu geldi. “Efendimiz krala müjde!” dedi, “Bugün RAB sana karşı bütün ayaklananların elinden seni kurtardı.”
32 Mfalme akamuuliza huyo Mkushi, “Je, kijana Absalomu yuko salama?” Huyo Mkushi akajibu, “Adui wa mfalme bwana wangu na wote wale walioinuka kukudhuru na wawe kama huyo kijana.”
Kral Kûşlu'ya, “Genç Avşalom güvenlikte mi?” diye sordu. Kûşlu, “Efendimiz kral!” diye yanıtladı, “Düşmanlarının ve kötü amaçla sana karşı ayaklananların hepsinin sonu bu gencin sonu gibi olsun.”
33 Mfalme akatetemeka. Akapanda chumbani juu kupitia langoni akilia. Alipokuwa akienda, akasema, “Ee mwanangu Absalomu! Mwanangu, mwanangu Absalomu! Laiti ningekufa badala yako: Ee Absalomu, mwanangu, mwanangu!”
Kral sarsıldı. Giriş kapısının üstündeki odaya çıkıp ağladı. Giderken, “Ah oğlum Avşalom! Ah oğlum, oğlum Avşalom!” diye inliyordu, “Keşke senin yerine ben ölseydim, oğlum! Ah oğlum Avşalom!”

< 2 Samweli 18 >