< 2 Samweli 18 >

1 Daudi akakusanya watu aliokuwa nao na kuweka majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
Therfor Dauid, whanne the puple `was biholdun, ordeynede tribunes and centuriouns on hem.
2 Daudi akatuma vikosi vya askari: theluthi moja ilikuwa chini ya amri ya Yoabu, theluthi ya pili chini ya Abishai mwana wa Seruya nduguye Yoabu, na theluthi ya tatu chini ya Itai, Mgiti. Mfalme akaviambia vikosi, “Hakika mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nanyi.”
And he yaf the thridde part of the puple vndur the hond of Joab; and the thridde part vndur the hond of Abisai, sone of Saruye, brother of Joab; and the thridde part vndur the hond of Ethai, that was of Geth. And the kyng seide to the puple, Also Y schal go out with you.
3 Lakini watu wakasema, “Haikupasi kwenda, ikiwa sisi tutalazimika kukimbia, wao hawatatujali. Hata kama nusu yetu tukifa hawatajali, lakini wewe una thamani ya watu kama sisi kumi elfu. Ingekuwa bora zaidi kwako basi kutupatia msaada kutoka mjini.”
And the puple answeride, Thou schalt not go out; for whether we fleen, it schal not perteyne to hem bi greet werk of vs; whether half the part fallith doun of vs, thei schulen not recke ynow, for thou art rekynyd for ten thousynde; therfor it is betere, that thou be to vs in the citee in stronge hold.
4 Mfalme akajibu, “Nitafanya lolote linaloonekana jema zaidi kwenu.” Kwa hiyo mfalme akasimama kando ya lango wakati watu wote wakitoka nje kwa makundi ya mamia na maelfu.
`To whiche the kyng seide, Y schal do this, that semeth riytful to you. Therfor the kyng stood bisidis the yate, and the puple yede out bi her cumpenyes, bi hundridis and bi thousyndis.
5 Mfalme akawaamuru Yoabu, Abishai na Itai, “Kuweni wapole kwa kijana Absalomu kwa ajili yangu.” Vikosi vyote vikasikia mfalme akitoa amri kwa kila jemadari kumhusu Absalomu.
And the king comaundide to Joab, and to Abisai, and Ethai, and seyde, Kepe ye to me the child Absolon. And al the puple herde the kyng comaundinge to alle the princes for Absolon.
6 Jeshi likatoka kwenda kwenye uwanja wa vita kupigana na Israeli, hivyo vita vikapiganwa katika msitu wa Efraimu.
Therfor the puple yede out in to the feeld ayens Israel; and the batel was maad in the forest of Effraym.
7 Huko jeshi la Israeli likashindwa na watu wa Daudi, siku hiyo majeruhi walikuwa wengi kiasi cha watu ishirini elfu.
And the puple of Israel was slayn there of the oost of Dauid, and a greet sleyng of twenti thousynde was maad in that dai.
8 Vita vikaenea nchi nzima, watu wengi zaidi wakifia msituni siku hiyo kuliko waliouawa kwa upanga.
Forsothe the batel was scaterid there on the face of al erthe, and many mo weren of the puple whiche the forest wastide, than thei whiche the swerd deuourid in that dai.
9 Basi ikawa Absalomu alikutana na watu wa Daudi. Yeye alikuwa amepanda nyumbu wake, naye nyumbu alipopita chini ya matawi yaliyosongana ya mwaloni mkubwa, kichwa cha Absalomu kilinaswa kwenye mti. Akaachwa akiningʼinia hewani, wakati nyumbu aliyekuwa amempanda aliendelea kwenda.
Sotheli it bifeld, that Absalon sittinge on a mule, cam ayens the seruauntis of Dauid; and whanne the mule hadde entrid vndur a thicke ook, and greet, the heed of Absolon cleuyde to the ook; and whanne he was hangid bitwixe heuene and erthe, the mule, on which he sat, passide.
10 Mmojawapo wa wale watu alipoona, akamwambia Yoabu, “Nimemwona Absalomu akiningʼinia kwenye mti wa mwaloni.”
Sotheli `sum man siy this, and telde to Joab, and seide, Y siy Absolon hange on an ook.
11 Yoabu akamwambia huyo mtu, “Nini! Ulimwona Absalomu? Kwa nini hukumpiga papo hapo mpaka chini? Ndipo ningekupa shekeli kumi za fedha na mkanda wa askari shujaa.”
And Joab seide to the man that `hadde telde to hym, If thou siyest, whi persidist thou not hym to the erthe, and Y schulde haue youe `to thee ten siclis of siluer, and a girdil?
12 Lakini huyo mtu akamjibu Yoabu, “Hata kama ningepimiwa shekeli 1,000 mikononi mwangu, nisingeinua mkono wangu dhidi ya mwana wa mfalme. Tukiwa tunasikia, mfalme alikuagiza wewe na Abishai pamoja na Itai, akisema, ‘Mlindeni kijana Absalomu kwa ajili yangu.’
And he seide to Joab, Thouy thou paiedist in myn hondis a thousynde platis of siluer, Y nolde sende myn hond in to the sone of the king; for the while we herden, the kyng comaundide to thee, and to Abisai, and to Ethai, and seide, Kepe ye to me the child Absolon.
13 Nami kama ningekuwa nimemtendea kwa hila, na hakuna lolote linalofichika kwa mfalme, wewe mwenyewe ungejitenga nami.”
But and if Y hadde do ayens my lijf hardili, this myyte not be hid fro the kyng, and thou woldist stonde on the contrarye side.
14 Yoabu akasema, “Mimi sitapoteza muda hapa pamoja nawe.” Hivyo akachukua mikuki mitatu mkononi mwake, akamchoma Absalomu nayo moyoni alipokuwa angali hai akiningʼinia katika ule mwaloni.
And Joab seide, Not as thou wolt, `Absolon schal be kept, but Y schal asaile hym bifor thee. Therfore Joab took thre speris in his hond, and fitchide tho in the herte of Absolon. And whanne he spraulide, yit cleuynge in the ook,
15 Nao wabeba silaha kumi wa Yoabu wakamzunguka Absalomu, wakampiga na kumuua.
ten yonge squieris of Joab runnen, and smytiden, and killiden hym.
16 Kisha Yoabu akapiga tarumbeta, navyo vikosi vikaacha kuwafuata Israeli, kwa maana Yoabu aliwasimamisha.
Sotheli Joab sownede with a clarioun, and withhelde the puple, lest it pursuede Israel fleynge, and he wolde spare the multitude.
17 Wakamchukua Absalomu, wakamtupa katika shimo kubwa huko msituni na kulundika lundo kubwa la mawe juu yake. Huko nyuma, Waisraeli wote wakakimbilia nyumbani kwao.
And thei token Absolon, and castiden forth him in to a greet dich in the forest, and baren togidere a ful greet heep of stoonys on hym; forsothe al Israel fledde in to his tabernaclis.
18 Wakati wa uhai wa Absalomu alikuwa amechukua nguzo na kuisimamisha katika Bonde la Mfalme, kwa maana alifikiri, “Sina mwana atakayeendeleza kumbukumbu ya jina langu.” Akaita nguzo hiyo kwa jina lake mwenyewe. Nayo inaitwa Mnara wa Ukumbusho wa Absalomu mpaka leo.
Forsothe Absolon, while he lyuyde yit, hadde reisid to hym a memorial, which is in the valey of the kyng; for he seide, Y haue no sone, and this schal be the mynde of my name; and he clepide `the memorial bi his name, and it is clepid the Hond, `that is, werk, of Absolon `til to this dai.
19 Basi Ahimaasi mwana wa Sadoki akasema, “Niruhusu mimi nikimbie na kumpelekea mfalme habari kwamba Bwana amemwokoa mfalme kutoka mikononi mwa adui zake.”
Forsothe Achymaas, sone of Sadoch, seide, Y schal renne, and Y schal telle to the kyng, that the Lord hath maad doom to hym of the hond of hise enemyes.
20 Yoabu akamwambia Ahimaasi, “Leo si wewe utakayepeleka habari. Unaweza kupeleka habari wakati mwingine, lakini leo haikupasi kupeleka, kwa sababu mwana wa mfalme amekufa.”
To whom Joab seide, Thou schalt not be messanger in this dai, but thou schalt telle in another dai; I nyle that thou telle to dai, for the sone of the kyng is deed.
21 Ndipo Yoabu akamwambia mtu mmoja Mkushi, “Nenda, ukamwambie mfalme kile ulichoona.” Mkushi akasujudu mbele ya Yoabu akaondoka mbio.
And Joab seide to Chusi, Go thou, and telle to the kyng tho thingis that thou hast seyn. Chusi worschypide Joab, and ran.
22 Ahimaasi mwana wa Sadoki akamwambia tena Yoabu, “Liwalo na liwe, tafadhali niruhusu nikimbie nyuma ya huyo Mkushi.” Lakini Yoabu akajibu, “Mwanangu, mbona wataka kwenda? Wewe huna habari yoyote itakayokupa tuzo.”
Eft Achymaas, sone of Sadoch, seide to Joab, What lettith, if also Y renne aftir Chusi? And Joab seide to hym, What wolt thou renne, my sone? Come thou hidur, thou schalt not be a berere of good message.
23 Ahimaasi akasema, “Liwalo na liwe, nataka kukimbia.” Kwa hiyo Yoabu akamwambia, “Haya, kimbia!” Ndipo Ahimaasi akakimbia kufuata njia ya kupitia tambarare, akafika kabla ya huyo Mkushi.
Which answeride, `What sotheli if Y schal renne? And Joab seide to hym, Renn thou. Therfor Achymaas ran bi the weie of schortnesse, `and sped, and passide Chusi.
24 Wakati Daudi alipokuwa ameketi kati ya lango la ndani na la nje, mlinzi akapanda juu ya paa la lango kupitia ukutani. Alipotazama nje, akaona mtu mmoja akikimbia peke yake.
Forsothe Dauid sat bitwixe twei yatis; sotheli the spiere, that was in the hiynesse of the yate on the wal, reiside the iyen, and siy a man aloone rennynge;
25 Mlinzi akampazia mfalme sauti na kumpa taarifa. Mfalme akasema, “Ikiwa yuko peke yake, lazima atakuwa na habari njema.” Naye yule mtu akazidi kusogea karibu.
and the spiere criede, and schewide to the kyng. And the kyng seide to hym, If he is aloone, good message is in his mouth.
26 Kisha mlinzi akaona mtu mwingine anakuja akikimbia, akamwita bawabu, “Tazama, mtu mwingine anakuja akikimbia peke yake!” Mfalme akasema, “Lazima atakuwa analeta habari njema pia.”
Sotheli while he hastide, and neiyede neer, the spiere siy another man rennynge; and the spiere criede `in the hiynesse, and seide, Another man rennynge aloone apperith to me. And the kyng seide to hym, And this man is a good messanger.
27 Mlinzi akasema, “Ninaona kuwa yule wa kwanza anakimbia kama Ahimaasi mwana wa Sadoki.” Mfalme akasema, “Yeye ni mtu mwema. Analeta habari njema.”
Sotheli the spiere seide, Y biholde the rennyng of the formere, as the rennyng of Achymaas, sone of Sadoch. And the kyng seide, He is a good man, and he cometh bryngynge a good message.
28 Ndipo Ahimaasi akamwita mfalme, akasema, “Mambo yote ni mema!” Akasujudu mbele ya mfalme uso wake mpaka ardhini, akasema, “Ahimidiwe Bwana Mungu wako! Yeye aliyewatoa watu wale walioinua mikono yao dhidi ya mfalme bwana wangu.”
Forsothe Achymaas criede, and seide to the kyng, Heil kyng! And he worschipide the kyng lowli bifor hym to erthe, and seide, Blessid be thi Lord God, that closide togidere the men, that reisyden her hondis ayens my lord the kyng.
29 Mfalme akauliza, “Je, huyo kijana Absalomu yuko salama?” Ahimaasi akajibu, “Kulikuwa na machafuko mengi mara tu Yoabu alipokuwa anataka kumtuma mtumishi wa mfalme pamoja nami mtumishi wako, lakini sijui ilikuwa nini?”
And the kyng seide, Whether pees is to the child Absolon? And Achymaas seide, Y siy, `that is, Y herde, a great noise, whanne Joab, thi seruaunt, thou kyng, sente me thi seruaunt; Y kan noon othir thing.
30 Mfalme akasema, “Simama kando na usubiri hapa.” Basi akasogea kando na kusimama hapo.
To whom the kyng seide, Passe thou, and stonde here. And whanne he hadde passid, and stood, Chusi apperide;
31 Ndipo huyo Mkushi akawasili na kusema, “Mfalme bwana wangu, sikia habari njema! Leo Bwana amekuokoa kutoka kwa wale wote walioinuka dhidi yako.”
and he cam and seide, My lord the kyng, Y brynge good message; for the Lord hath demed to dai for thee of the hond of alle men that risiden ayens thee.
32 Mfalme akamuuliza huyo Mkushi, “Je, kijana Absalomu yuko salama?” Huyo Mkushi akajibu, “Adui wa mfalme bwana wangu na wote wale walioinuka kukudhuru na wawe kama huyo kijana.”
Forsothe the kyng seide to Chusi, Whether pees is to the child Absolon? To whom Chusi answeride, and seide, The enemyes of my lord the kyng, and alle men that risiden ayens hym in to yuel, be maad as the child.
33 Mfalme akatetemeka. Akapanda chumbani juu kupitia langoni akilia. Alipokuwa akienda, akasema, “Ee mwanangu Absalomu! Mwanangu, mwanangu Absalomu! Laiti ningekufa badala yako: Ee Absalomu, mwanangu, mwanangu!”
Therfor the kyng was sory, and stiede in to the soler of the yate, and wepte, and spak thus goynge, My sone, Absolon! Absolon, my sone! who yyueth to me, that Y die for thee? Absolon, my sone! my sone, Absolon!

< 2 Samweli 18 >