< 2 Samweli 17 >
1 Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Nipe ruhusa niwachague watu kumi na mbili elfu na waanze safari usiku huu huu kumfuatia Daudi.
Achitophel donc dit à Absalom: Je me choisirai douze mille hommes, et me levant, je poursuivrai David en cette nuit.
2 Nitamshambulia wakati akiwa amechoka na ni dhaifu. Nitampiga na hofu, na kisha watu wote walio pamoja naye watakimbia. Nitampiga mfalme peke yake
Et, fondant sur lui (car il est las et de mains défaillantes), je le frapperai; et lorsqu’aura fui tout le peuple qui est avec lui, je frapperai le roi désolé.
3 na kuwarudisha watu wote kwako. Kifo cha mtu yule unayemtafuta kitamaanisha kurudi kwa wote, hakuna hata mtu mmoja atakayeumizwa.”
Et je ramènerai tout le peuple, comme un seul homme a coutume de revenir; car c’est un seul homme que vous cherchez vous-même; et tout le peuple sera en paix.
4 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Absalomu na kwa wazee wote wa Israeli.
Et sa parole plut à Absalom et à tous les anciens d’Israël.
5 Lakini Absalomu akasema, “Pia mwiteni Hushai, Mwariki, ili tuweze kusikia anachokisema.”
Mais Absalom dit: Appelez Chusaï, l’Arachite, et écoutons ce que lui aussi dira.
6 Hushai alipokuja, Absalomu akasema, “Ahithofeli ametoa shauri hili. Je, tufanye anavyosema? Kama sivyo, tupe maoni yako.”
Et lorsque Chusaï fut venu vers Absalom, Absalom lui dit: Achitophel a dit cette parole; devons-nous l’exécuter ou non? quel conseil donnes-tu?
7 Hushai akamjibu Absalomu, “Shauri la Ahithofeli alilotoa halifai kwa wakati huu.
Et Chusaï répondit à Absalom: Ce n’est pas un bon conseil qu’a donné Achitophel cette fois.
8 Unamfahamu baba yako na watu wake, ni wapiganaji hodari, nao ni wakali kama dubu mwitu aliyepokonywa watoto wake. Zaidi ya hayo, baba yako ni mpiganaji jasiri, usiku hatalala pamoja na vikosi.
Et Chusaï ajouta encore: Vous savez que votre père et les hommes qui sont avec lui sont très vaillants, et d’un cœur outré, comme si une ourse était furieuse, ses petits lui ayant été ravis dans la forêt; et votre père aussi, homme de guerre, ne restera point avec le peuple.
9 Hata sasa, amefichwa ndani ya pango au mahali pengine. Kama atatangulia kushambulia vikosi vyako, yeyote asikiaye habari hii atasema, ‘Kuna machinjo makubwa miongoni mwa vikosi vinavyomfuata Absalomu.’
Peut-être est-il maintenant caché dans les cavernes, ou en un autre lieu qu’il aura voulu; et si quelqu’un, quel qu’il soit, tombe au commencement, on l’apprendra, et quiconque l’apprendra, dira: Il a été fait une grande plaie sur le peuple qui suivait Absalom.
10 Basi hata yule askari hodari kuliko wengine wote, ambaye moyo wake ni kama wa simba, atayeyuka kwa hofu, kwa maana Israeli yote wanajua kwamba baba yako ni mpiganaji na kwamba wale walio pamoja naye ni watu hodari.
Et tous les plus vaillants, dont le cœur est comme celui du lion, seront saisis d’effroi; car tout le peuple d’Israël sait que votre père est vaillant, et que tous ceux qui sont avec lui sont vigoureux.
11 “Kwa hiyo nakushauri: Israeli wote na wakusanyikie kwako, kuanzia Dani hadi Beer-Sheba, katika wingi wao jinsi walivyo kama mchanga wa ufuoni mwa bahari, wewe mwenyewe ukiwaongoza vitani.
Mais ceci me semble être un bon conseil: que tout Israël s’assemble près de vous, depuis Dan jusqu’à Bersabée, comme le sable innombrable de la mer, et vous, vous serez au milieu d’eux.
12 Ndipo tutakapomshambulia popote atakapoonekana, nasi tutamwangukia kama umande unavyoshuka juu ya ardhi. Yeye mwenyewe wala watu wake hakuna atakayeachwa hai.
Et nous fondrons sur David, en quelque lieu que nous le trouvions, et nous le couvrirons comme la rosée a coutume de tomber sur la terre; quant aux hommes qui sont avec lui, nous n’en laisserons pas même un seul.
13 Kama atakimbilia katika mji wowote, basi Israeli wote watazungushia mji ule kamba, nasi tutauburuta mji huo mpaka bondeni hadi isionekane hata changarawe ya huo mji.”
Que s’il entre en quelque ville, tout Israël environnera cette ville de cordes; et nous l’entraînerons dans le torrent, afin qu’on n’en trouve pas même une petite pierre.
14 Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai, Mwariki, ni jema zaidi kuliko lile la Ahithofeli.” Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kupinga shauri nzuri la Ahithofeli, ili kuleta maafa juu ya Absalomu.
Alors Absalom dit et tous les hommes d’Israël: Le conseil de Chusaï, l’Arachite, est meilleur que le conseil d’Achitophel. Ainsi par la volonté du Seigneur fut dissipé le conseil utile d’Achitophel, afin que le Seigneur amenât le malheur sur Absalom.
15 Hushai akawaambia makuhani Sadoki na Abiathari, “Ahithofeli amemshauri Absalomu na wazee wa Israeli kufanya kadha wa kadha, lakini mimi nimewashauri wao kufanya kadha wa kadha.
Et Chusaï dit à Sadoc et à Abiathar, prêtres: C’est de cette manière qu’Achitophel a donné conseil à Absalom et aux anciens d’Israël, et moi j’ai donné tel et tel conseil.
16 Sasa tumeni ujumbe haraka na kumwambia Daudi, ‘Usiku huu usilale kwenye vivuko katika jangwa; vuka bila kukosa, la sivyo, mfalme pamoja na watu wote waliofuatana naye watamezwa.’”
Maintenant donc, envoyez vite, et annoncez à David, disant: Ne demeurez point cette nuit dans les plaines du désert; mais passez au-delà sans délai, de peur que le roi ne soit englouti, et tout le peuple qui est avec lui.
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwa wakingoja huko En-Rogeli, naye mtumishi mmoja wa kike akawa anakwenda kuwapasha habari nao wakawa wanakwenda kumwambia Mfalme Daudi, kwa maana wasingetaka kujihatarisha kuonekana wakiingia mjini.
Or Jonathas et Achimaas étaient près de la fontaine de Rogel: la servante vint, et les avertit; et ils partirent pour rapporter au roi David le message; car ils ne pouvaient être vus, ou entrer dans la ville.
18 Lakini kijana mmoja mwanaume akawaona, naye akamwambia Absalomu. Basi wote wawili wakaondoka haraka, wakaenda mpaka kwenye nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu. Mtu huyo alikuwa na kisima katika ua wa nyumba yake, nao Yonathani na Ahimaasi wakateremka ndani ya kisima hicho.
Mais un certain enfant les vit, et en donna avis à Absalom: or, eux, d’un pas précipité, entrèrent dans la maison d’un certain homme de Bahurim, lequel avait un puits dans sa cour, et ils y descendirent.
19 Mkewe akachukua kifuniko, akakiweka kwenye mdomo wa kile kisima na kuanika nafaka juu yake. Hakuna mtu yeyote aliyefahamu chochote kuhusu jambo hilo.
Cependant la femme prit sa couverture, et retendit sur le puits, comme pour faire sécher de l’orge mondé; et ainsi fut cachée la chose.
20 Watu wa Absalomu walipofika kwa huyo mwanamke, wakamuuliza, “Wako wapi Ahimaasi na Yonathani?” Huyo mwanamke akawajibu, “Walivuka kijito.” Watu wa Absalomu wakapekua lakini hawakuwaona hata mmoja, hivyo wakarudi Yerusalemu.
Et lorsque les serviteurs d’Absalom furent venus dans la maison, ils dirent à cette femme: Où sont Achimaas et Jonathas? Et la femme leur répondit: Ils ont passé à la hâte, après avoir goûté un peu d’eau. Mais ceux qui les cherchaient, ne les trouvant point, retournèrent à Jérusalem.
21 Baada ya watu hao kuondoka, wale watu wawili yaani Yonathani na Ahimaasi wakapanda kutoka mle kisimani na kwenda kumpasha Mfalme Daudi habari. Wakamwambia, “Ondoka, uvuke haya maji haraka. Ahithofeli ameshauri kadha wa kadha dhidi yako.”
Et lorsqu’ils s’en furent allés, Achimaas et Jonathas montèrent hors du puits, et, cheminant, ils l’annoncèrent au roi David, et dirent: Levez-vous, et passez le fleuve; car Achitophel a donné tel conseil contre vous.
22 Kwa hiyo Daudi na watu wote aliokuwa nao waliondoka na kuvuka Yordani. Kufika wakati wa mapambazuko, hapakuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa hajavuka Mto Yordani.
David donc se leva, et tout le peuple qui était avec lui, et ils passèrent le Jourdain jusqu’à ce que le jour parût, et il n’en demeura pas même un seul qui ne passât le fleuve.
23 Ahithofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka kwenda nyumbani kwake kwenye mji wake. Akaiweka nyumba yake katika utaratibu, kisha akajinyonga mwenyewe. Hivyo akafa na akazikwa katika kaburi la baba yake.
Mais Achitophel, voyant que son conseil n’avait pas été suivi, sella son âne et se leva, et s’en alla en sa maison et en sa ville; et, sa maison réglée, il se pendit, et il fut enseveli dans le sépulcre de son père.
24 Daudi akaenda Mahanaimu, naye Absalomu akavuka Yordani pamoja na watu wote wa Israeli.
Ensuite David vint dans le camp, et Absalom passa le Jourdain, lui et tous les hommes d’Israël avec lui.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Amasa alikuwa mwana wa mtu mmoja aliyeitwa Yetheri, Mwisraeli, ambaye alikuwa amemwoa Abigaili binti Nahashi, dada yake Seruya mamaye Yoabu.
Et Absalom établit Amasa sur l’armée au lieu de Joab. Or Amasa était fils d’un homme qui s’appelait Jétra, de Jezraël, qui avait été avec Abigaïl, fille de Naas, sœur de Sarvia, laquelle fut mère de Joab.
26 Waisraeli na Absalomu wakapiga kambi huko nchi ya Gileadi.
Et Israël campa avec Absalom dans la terre de Galaad.
27 Daudi alipofika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni, Makiri mwana wa Amieli kutoka Lo-Debari, na Barzilai Mgileadi kutoka Rogelimu
Et lorsque David fut venu dans le camp, Sobi, fils de Naas, de Rabbath des enfants d’Ammon, et Machir, fils d’Ammihel de Lodabar, et Berzellaï, le Galaadite, de Rogelim,
28 wakaleta matandiko ya kitandani, mabakuli na vyombo vya mfinyanzi. Walileta pia ngano na shayiri, unga na bisi, maharagwe na kunde,
Lui offrirent des lits, des tapis, des vases de terre, du blé, de l’orge, de la farine, des grains rôtis, des fèves, des lentilles, des pois grillés.
29 asali na maziwa yaliyoganda, kondoo na jibini kutoka kwenye maziwa ya ngʼombe kwa ajili ya Daudi na watu wake ili wale. Kwa maana walisema, “Watu wameona njaa, tena wamechoka na wamepata kiu huko jangwani.”
Du miel, du beurre, des brebis, et des veaux gras; et ils les donnèrent à David et au peuple qui était avec lui pour manger: car ils supposèrent que le peuple était abattu par la faim et par la soif dans le désert.