< 2 Samweli 17 >

1 Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Nipe ruhusa niwachague watu kumi na mbili elfu na waanze safari usiku huu huu kumfuatia Daudi.
Achitophel dit à Absalom: « Laisse-moi choisir douze mille hommes; je me lèverai et je poursuivrai David cette nuit même et,
2 Nitamshambulia wakati akiwa amechoka na ni dhaifu. Nitampiga na hofu, na kisha watu wote walio pamoja naye watakimbia. Nitampiga mfalme peke yake
tombant sur lui à l'improviste pendant qu'il est fatigué et que ses mains sont affaiblies, je l'épouvanterai, et tout le peuple qui est avec lui s'enfuira; je frapperai alors le roi seul,
3 na kuwarudisha watu wote kwako. Kifo cha mtu yule unayemtafuta kitamaanisha kurudi kwa wote, hakuna hata mtu mmoja atakayeumizwa.”
et je ramènerai à toi tout le peuple: l'homme à qui tu en veux vaut le retour de tous; et tout le peuple sera en paix. »
4 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Absalomu na kwa wazee wote wa Israeli.
Ce discours plut à Absalom et à tous les anciens d'Israël.
5 Lakini Absalomu akasema, “Pia mwiteni Hushai, Mwariki, ili tuweze kusikia anachokisema.”
Cependant Absalom dit: « Appelez encore Chusaï l'Arachite et que nous entendions ce que lui aussi a dans la bouche. »
6 Hushai alipokuja, Absalomu akasema, “Ahithofeli ametoa shauri hili. Je, tufanye anavyosema? Kama sivyo, tupe maoni yako.”
Chusaï vint auprès d'Absalom, et Absalom lui dit: « Voici comment a parlé Achitophel; devons-nous faire ce qu'il a dit? Sinon, parle à ton tour. »
7 Hushai akamjibu Absalomu, “Shauri la Ahithofeli alilotoa halifai kwa wakati huu.
Chusaï répondit à Absalom: « Pour cette fois, le conseil qu'a donné Achitophel n'est pas bon. »
8 Unamfahamu baba yako na watu wake, ni wapiganaji hodari, nao ni wakali kama dubu mwitu aliyepokonywa watoto wake. Zaidi ya hayo, baba yako ni mpiganaji jasiri, usiku hatalala pamoja na vikosi.
Et Chusaï ajouta: « Tu sais que ton père et ses gens sont des braves; ils sont exaspérés comme le serait dans la campagne une ourse privée de ses petits. Ton père est un homme de guerre, et il ne passe pas la nuit avec le peuple.
9 Hata sasa, amefichwa ndani ya pango au mahali pengine. Kama atatangulia kushambulia vikosi vyako, yeyote asikiaye habari hii atasema, ‘Kuna machinjo makubwa miongoni mwa vikosi vinavyomfuata Absalomu.’
Voici que maintenant il est caché dans quelque ravin ou dans quelque autre lieu. Et si, dès le commencement, il tombe quelques-uns des vôtres, on l'apprendra et l'on dira: Il y a eu une déroute dans le peuple qui suit Absalom.
10 Basi hata yule askari hodari kuliko wengine wote, ambaye moyo wake ni kama wa simba, atayeyuka kwa hofu, kwa maana Israeli yote wanajua kwamba baba yako ni mpiganaji na kwamba wale walio pamoja naye ni watu hodari.
Alors, même le plus vaillant, son cœur fût-il comme un cœur de lion, sera découragé; car tout Israël sait que ton père est un héros, et que ceux qui l'accompagnent sont des braves.
11 “Kwa hiyo nakushauri: Israeli wote na wakusanyikie kwako, kuanzia Dani hadi Beer-Sheba, katika wingi wao jinsi walivyo kama mchanga wa ufuoni mwa bahari, wewe mwenyewe ukiwaongoza vitani.
Je conseille donc que tout Israël se rassemble auprès de toi, depuis Dan jusqu'à Bersabée, multitude pareille au sable qui est sur le bord de la mer; et tu marcheras en personne au combat.
12 Ndipo tutakapomshambulia popote atakapoonekana, nasi tutamwangukia kama umande unavyoshuka juu ya ardhi. Yeye mwenyewe wala watu wake hakuna atakayeachwa hai.
Nous l'atteindrons en quelque lieu qu'il se trouve, et nous tomberons sur lui comme la rosée tombe sur le sol, et nous ne laisserons échapper ni lui, ni aucun de tous les hommes qui sont avec lui.
13 Kama atakimbilia katika mji wowote, basi Israeli wote watazungushia mji ule kamba, nasi tutauburuta mji huo mpaka bondeni hadi isionekane hata changarawe ya huo mji.”
S'il se retire dans une ville, tout Israël apportera des cordes vers cette ville, et nous la traînerons jusqu'au torrent, jusqu'à ce qu'on n'y trouve plus même une pierre. »
14 Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai, Mwariki, ni jema zaidi kuliko lile la Ahithofeli.” Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kupinga shauri nzuri la Ahithofeli, ili kuleta maafa juu ya Absalomu.
Absalom et tous les gens d'Israël dirent: « Le conseil de Chusaï l'Arachite vaut mieux que le conseil d'Achitophel. » Yahweh avait décidé de rendre vain le bon conseil d'Achitophel, afin que Yahweh amenât le malheur sur Absalom.
15 Hushai akawaambia makuhani Sadoki na Abiathari, “Ahithofeli amemshauri Absalomu na wazee wa Israeli kufanya kadha wa kadha, lakini mimi nimewashauri wao kufanya kadha wa kadha.
Chusaï dit aux prêtres Sadoc et Abiathar: « Achitophel a donné tel et tel conseil à Absalom et aux anciens d'Israël, et moi j'ai donné tel et tel conseil.
16 Sasa tumeni ujumbe haraka na kumwambia Daudi, ‘Usiku huu usilale kwenye vivuko katika jangwa; vuka bila kukosa, la sivyo, mfalme pamoja na watu wote waliofuatana naye watamezwa.’”
Envoyez donc de suite informer David, et faites-lui dire: Ne passe pas la nuit dans les plaines du désert, mais hâte-toi de traverser, de peur qu'il n'y ait un suprême désastre pour le roi et pour tout le peuple qui est avec lui. »
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwa wakingoja huko En-Rogeli, naye mtumishi mmoja wa kike akawa anakwenda kuwapasha habari nao wakawa wanakwenda kumwambia Mfalme Daudi, kwa maana wasingetaka kujihatarisha kuonekana wakiingia mjini.
Jonathas et Achimaas se tenaient à En-Rogel; la servante allait les informer, et eux-mêmes allaient donner avis au roi David; car ils ne pouvaient se faire voir en entrant dans la ville.
18 Lakini kijana mmoja mwanaume akawaona, naye akamwambia Absalomu. Basi wote wawili wakaondoka haraka, wakaenda mpaka kwenye nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu. Mtu huyo alikuwa na kisima katika ua wa nyumba yake, nao Yonathani na Ahimaasi wakateremka ndani ya kisima hicho.
Un jeune homme les ayant aperçus, il le rapporta à Absalom. Mais ils se hâtèrent tous deux de partir, et ils arrivèrent à Bahurim, dans la maison d'un homme qui avait une citerne dans sa cour, et ils y descendirent.
19 Mkewe akachukua kifuniko, akakiweka kwenye mdomo wa kile kisima na kuanika nafaka juu yake. Hakuna mtu yeyote aliyefahamu chochote kuhusu jambo hilo.
La femme prit une couverture, qu'elle étendit au dessus de la citerne, et elle y répandit du grain pilé, en sorte qu'on ne remarquait rien.
20 Watu wa Absalomu walipofika kwa huyo mwanamke, wakamuuliza, “Wako wapi Ahimaasi na Yonathani?” Huyo mwanamke akawajibu, “Walivuka kijito.” Watu wa Absalomu wakapekua lakini hawakuwaona hata mmoja, hivyo wakarudi Yerusalemu.
Les serviteurs d'Absalom entrèrent chez la femme dans la maison, et dirent: « Où sont Achimaas et Jonathas? » La femme leur répondit: « Ils ont passé le ruisseau. » Ils cherchèrent et, ne les trouvant pas, ils retournèrent à Jérusalem.
21 Baada ya watu hao kuondoka, wale watu wawili yaani Yonathani na Ahimaasi wakapanda kutoka mle kisimani na kwenda kumpasha Mfalme Daudi habari. Wakamwambia, “Ondoka, uvuke haya maji haraka. Ahithofeli ameshauri kadha wa kadha dhidi yako.”
Après leur départ, Achimaas et Jonathas remontèrent de la citerne, et allèrent informer le roi David. Ils dirent à David: « Levez-vous et hâtez-vous de passer l'eau, car Achitophel a donné tel conseil contre vous. »
22 Kwa hiyo Daudi na watu wote aliokuwa nao waliondoka na kuvuka Yordani. Kufika wakati wa mapambazuko, hapakuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa hajavuka Mto Yordani.
David et tout le peuple qui était avec lui, s'étant levés, passèrent le Jourdain; au point du jour, il n'en restait pas un seul qui n'eût passé le Jourdain.
23 Ahithofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka kwenda nyumbani kwake kwenye mji wake. Akaiweka nyumba yake katika utaratibu, kisha akajinyonga mwenyewe. Hivyo akafa na akazikwa katika kaburi la baba yake.
Quand Achitophel vit que son conseil n'était pas suivi, il sella son âne, et se leva pour s'en aller chez lui dans sa ville; puis, après avoir donné ses ordres à sa maison, il s'étrangla, et mourut; et on l'enterra dans le tombeau de son père.
24 Daudi akaenda Mahanaimu, naye Absalomu akavuka Yordani pamoja na watu wote wa Israeli.
David arriva à Mahanaïm; et Absalom passa le Jourdain, lui et tous les hommes d'Israël avec lui.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Amasa alikuwa mwana wa mtu mmoja aliyeitwa Yetheri, Mwisraeli, ambaye alikuwa amemwoa Abigaili binti Nahashi, dada yake Seruya mamaye Yoabu.
Absalom avait mis à la tête de l'armée Amasa, à la place de Joab; Amasa était fils d'un homme appelé Jéthra, l'Ismaélite, qui était allé vers Abigaïl, fille de Naas, sœur de Sarvia, la mère de Joab.
26 Waisraeli na Absalomu wakapiga kambi huko nchi ya Gileadi.
Ainsi Israël et Absalom campaient dans le pays de Galaad.
27 Daudi alipofika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni, Makiri mwana wa Amieli kutoka Lo-Debari, na Barzilai Mgileadi kutoka Rogelimu
Lorsque David fut arrivé à Mahanaïm, Sobi, fils de Naas, de Rabba des fils d'Ammon, Machir, fils d'Ammiel de Lodabar, et Berzellaï, le Galaadite, de Rogelim,
28 wakaleta matandiko ya kitandani, mabakuli na vyombo vya mfinyanzi. Walileta pia ngano na shayiri, unga na bisi, maharagwe na kunde,
vinrent lui offrir des lits, des plats, des vases de terre, du froment, de l'orge, de la farine, du grain rôti, des fèves, des lentilles, du grain rôti,
29 asali na maziwa yaliyoganda, kondoo na jibini kutoka kwenye maziwa ya ngʼombe kwa ajili ya Daudi na watu wake ili wale. Kwa maana walisema, “Watu wameona njaa, tena wamechoka na wamepata kiu huko jangwani.”
du miel, du beurre, des brebis et des fromages de vache: ils apportèrent ces choses en nourriture à David et au peuple qui était avec lui, car ils disaient: « Ce peuple a souffert de la faim, de la fatigue et de la soif dans le désert. »

< 2 Samweli 17 >