< 2 Samweli 17 >

1 Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Nipe ruhusa niwachague watu kumi na mbili elfu na waanze safari usiku huu huu kumfuatia Daudi.
Moreover Ahithophel said unto Absalom: 'Let me now choose out twelve thousand men, and I will arise and pursue after David this night;
2 Nitamshambulia wakati akiwa amechoka na ni dhaifu. Nitampiga na hofu, na kisha watu wote walio pamoja naye watakimbia. Nitampiga mfalme peke yake
and I will come upon him while he is weary and weak-handed, and will make him afraid; and all the people that are with him shall flee; and I will smite the king only;
3 na kuwarudisha watu wote kwako. Kifo cha mtu yule unayemtafuta kitamaanisha kurudi kwa wote, hakuna hata mtu mmoja atakayeumizwa.”
and I will bring back all the people unto thee; when all shall have returned, save the man whom thou seekest, all the people will be in peace.'
4 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Absalomu na kwa wazee wote wa Israeli.
And the saying pleased Absalom well, and all the elders of Israel.
5 Lakini Absalomu akasema, “Pia mwiteni Hushai, Mwariki, ili tuweze kusikia anachokisema.”
Then said Absalom: 'Call now Hushai the Archite also, and let us hear likewise what he saith.'
6 Hushai alipokuja, Absalomu akasema, “Ahithofeli ametoa shauri hili. Je, tufanye anavyosema? Kama sivyo, tupe maoni yako.”
And when Hushai was come to Absalom, Absalom spoke unto him, saying: 'Ahithophel hath spoken after this manner; shall we do after his saying? if not, speak thou.'
7 Hushai akamjibu Absalomu, “Shauri la Ahithofeli alilotoa halifai kwa wakati huu.
And Hushai said unto Absalom: 'The counsel that Ahithophel hath given this time is not good.'
8 Unamfahamu baba yako na watu wake, ni wapiganaji hodari, nao ni wakali kama dubu mwitu aliyepokonywa watoto wake. Zaidi ya hayo, baba yako ni mpiganaji jasiri, usiku hatalala pamoja na vikosi.
Hushai said moreover: 'Thou knowest thy father and his men, that they are mighty men, and they are embittered in their minds, as a bear robbed of her whelps in the field; and thy father is a man of war, and will not lodge with the people.
9 Hata sasa, amefichwa ndani ya pango au mahali pengine. Kama atatangulia kushambulia vikosi vyako, yeyote asikiaye habari hii atasema, ‘Kuna machinjo makubwa miongoni mwa vikosi vinavyomfuata Absalomu.’
Behold, he is hid now in some pit, or in some place; and it will come to pass, when they fall upon them at the first, and whosoever heareth it shall say: There is a slaughter among the people that follow Absalom;
10 Basi hata yule askari hodari kuliko wengine wote, ambaye moyo wake ni kama wa simba, atayeyuka kwa hofu, kwa maana Israeli yote wanajua kwamba baba yako ni mpiganaji na kwamba wale walio pamoja naye ni watu hodari.
then even he that is valiant, whose heart is as the heart of a lion, will utterly melt; for all Israel knoweth that thy father is a mighty man, and they that are with him are valiant men.
11 “Kwa hiyo nakushauri: Israeli wote na wakusanyikie kwako, kuanzia Dani hadi Beer-Sheba, katika wingi wao jinsi walivyo kama mchanga wa ufuoni mwa bahari, wewe mwenyewe ukiwaongoza vitani.
But I counsel that all Israel be gathered together unto thee, from Dan even to Beer-sheba, as the sand that is by the sea for multitude; and that thou go to battle in thine own person.
12 Ndipo tutakapomshambulia popote atakapoonekana, nasi tutamwangukia kama umande unavyoshuka juu ya ardhi. Yeye mwenyewe wala watu wake hakuna atakayeachwa hai.
So shall we come upon him in some place where he shall be found, and we will light upon him as the dew falleth on the ground; and of him and of all the men that are with him we will not leave so much as one.
13 Kama atakimbilia katika mji wowote, basi Israeli wote watazungushia mji ule kamba, nasi tutauburuta mji huo mpaka bondeni hadi isionekane hata changarawe ya huo mji.”
Moreover, if he withdraw himself into a city, then shall all Israel bring up ropes to that city, and we will draw it into the valley until there be not one small stone found there.'
14 Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai, Mwariki, ni jema zaidi kuliko lile la Ahithofeli.” Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kupinga shauri nzuri la Ahithofeli, ili kuleta maafa juu ya Absalomu.
And Absalom and all the men of Israel said: 'The counsel of Hushai the Archite is better than the counsel of Ahithophel.' — For the LORD had ordained to defeat the good counsel of Ahithophel, to the intent that the LORD might bring evil upon Absalom.
15 Hushai akawaambia makuhani Sadoki na Abiathari, “Ahithofeli amemshauri Absalomu na wazee wa Israeli kufanya kadha wa kadha, lakini mimi nimewashauri wao kufanya kadha wa kadha.
Then said Hushai unto Zadok and to Abiathar the priests: 'Thus and thus did Ahithophel counsel Absalom and the elders of Israel; and thus and thus have I counselled.
16 Sasa tumeni ujumbe haraka na kumwambia Daudi, ‘Usiku huu usilale kwenye vivuko katika jangwa; vuka bila kukosa, la sivyo, mfalme pamoja na watu wote waliofuatana naye watamezwa.’”
Now therefore send quickly, and tell David, saying: Lodge not this night in the plains of the wilderness, but in any wise pass over; lest the king be swallowed up, and all the people that are with him.'
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwa wakingoja huko En-Rogeli, naye mtumishi mmoja wa kike akawa anakwenda kuwapasha habari nao wakawa wanakwenda kumwambia Mfalme Daudi, kwa maana wasingetaka kujihatarisha kuonekana wakiingia mjini.
Now Jonathan and Ahimaaz stayed by En-rogel; and a maid-servant used to go and tell them; and they went and told king David; for they might not be seen to come into the city.
18 Lakini kijana mmoja mwanaume akawaona, naye akamwambia Absalomu. Basi wote wawili wakaondoka haraka, wakaenda mpaka kwenye nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu. Mtu huyo alikuwa na kisima katika ua wa nyumba yake, nao Yonathani na Ahimaasi wakateremka ndani ya kisima hicho.
But a lad saw them, and told Absalom; and they went both of them away quickly, and came to the house of a man in Bahurim, who had a well in his court; and they went down thither.
19 Mkewe akachukua kifuniko, akakiweka kwenye mdomo wa kile kisima na kuanika nafaka juu yake. Hakuna mtu yeyote aliyefahamu chochote kuhusu jambo hilo.
And the woman took and spread the covering over the well's mouth, and strewed groats thereon; and nothing was known.
20 Watu wa Absalomu walipofika kwa huyo mwanamke, wakamuuliza, “Wako wapi Ahimaasi na Yonathani?” Huyo mwanamke akawajibu, “Walivuka kijito.” Watu wa Absalomu wakapekua lakini hawakuwaona hata mmoja, hivyo wakarudi Yerusalemu.
And Absalom's servants came to the woman to the house; and they said: 'Where are Ahimaaz and Jonathan?' And the woman said unto them: 'They are gone over the brook of water.' And when they had sought and could not find them, they returned to Jerusalem.
21 Baada ya watu hao kuondoka, wale watu wawili yaani Yonathani na Ahimaasi wakapanda kutoka mle kisimani na kwenda kumpasha Mfalme Daudi habari. Wakamwambia, “Ondoka, uvuke haya maji haraka. Ahithofeli ameshauri kadha wa kadha dhidi yako.”
And it came to pass, after they were departed, that they came up out of the well, and went and told king David; and they said unto David: 'Arise ye, and pass quickly over the water; for thus hath Ahithophel counselled against you.'
22 Kwa hiyo Daudi na watu wote aliokuwa nao waliondoka na kuvuka Yordani. Kufika wakati wa mapambazuko, hapakuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa hajavuka Mto Yordani.
Then David arose, and all the people that were with him, and they passed over the Jordan; by the morning light there lacked not one of them that was not gone over the Jordan.
23 Ahithofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka kwenda nyumbani kwake kwenye mji wake. Akaiweka nyumba yake katika utaratibu, kisha akajinyonga mwenyewe. Hivyo akafa na akazikwa katika kaburi la baba yake.
And when Ahithophel saw that his counsel was not followed, he saddled his ass, and arose, and got him home, unto his city, and set his house in order, and strangled himself; and he died, and was buried in the sepulchre of his father.
24 Daudi akaenda Mahanaimu, naye Absalomu akavuka Yordani pamoja na watu wote wa Israeli.
When David was come to Mahanaim, Absalom passed over the Jordan, he and all the men of Israel with him.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Amasa alikuwa mwana wa mtu mmoja aliyeitwa Yetheri, Mwisraeli, ambaye alikuwa amemwoa Abigaili binti Nahashi, dada yake Seruya mamaye Yoabu.
And Absalom had set Amasa over the host instead of Joab. Now Amasa was the son of a man, whose name was Ithra the Jesraelite, that went in to Abigal the daughter of Nahash, sister to Zeruiah Joab's mother.
26 Waisraeli na Absalomu wakapiga kambi huko nchi ya Gileadi.
And Israel and Absalom pitched in the land of Gilead.
27 Daudi alipofika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni, Makiri mwana wa Amieli kutoka Lo-Debari, na Barzilai Mgileadi kutoka Rogelimu
And it came to pass, when David was come to Mahanaim, that Shobi the son of Nahash of Rabbah of the children of Ammon, and Machir the son of Ammiel of Lo-debar, and Barzillai the Gileadite of Rogelim,
28 wakaleta matandiko ya kitandani, mabakuli na vyombo vya mfinyanzi. Walileta pia ngano na shayiri, unga na bisi, maharagwe na kunde,
brought beds, and basins, and earthen vessels, and wheat, and barley, and meal, and parched corn, and beans, and lentils, and parched pulse,
29 asali na maziwa yaliyoganda, kondoo na jibini kutoka kwenye maziwa ya ngʼombe kwa ajili ya Daudi na watu wake ili wale. Kwa maana walisema, “Watu wameona njaa, tena wamechoka na wamepata kiu huko jangwani.”
and honey, and curd, and sheep, and cheese of kine, for David, and for the people that were with him, to eat; for they said: 'The people is hungry, and faint, and thirsty, in the wilderness.'

< 2 Samweli 17 >