< 2 Samweli 17 >

1 Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Nipe ruhusa niwachague watu kumi na mbili elfu na waanze safari usiku huu huu kumfuatia Daudi.
And Achitophel said to Absalom: I will choose me twelve thousand men, and I will arise and pursue after David this night.
2 Nitamshambulia wakati akiwa amechoka na ni dhaifu. Nitampiga na hofu, na kisha watu wote walio pamoja naye watakimbia. Nitampiga mfalme peke yake
And coming upon him (for he is now weary, and weak handed) I will defeat him: and when all the people is put to flight that is with him, I will kill the king who will be left alone.
3 na kuwarudisha watu wote kwako. Kifo cha mtu yule unayemtafuta kitamaanisha kurudi kwa wote, hakuna hata mtu mmoja atakayeumizwa.”
And I will bring back all the people, as if they were but one man: for thou seekest but one man: and all the people shall be in peace.
4 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Absalomu na kwa wazee wote wa Israeli.
And his saying pleased Absalom, and all the ancients of Israel.
5 Lakini Absalomu akasema, “Pia mwiteni Hushai, Mwariki, ili tuweze kusikia anachokisema.”
But Absalom said: Call Chusai the Arachite, and let us hear what he also saith.
6 Hushai alipokuja, Absalomu akasema, “Ahithofeli ametoa shauri hili. Je, tufanye anavyosema? Kama sivyo, tupe maoni yako.”
And when Chusai was come to Absalom, Absalom said to him: Achitophel hath spoken after this manner: shall we do it or not? what counsel dost thou give?
7 Hushai akamjibu Absalomu, “Shauri la Ahithofeli alilotoa halifai kwa wakati huu.
And Chusai said to Absalom: The counsel that Achitophel hath given this time is not good.
8 Unamfahamu baba yako na watu wake, ni wapiganaji hodari, nao ni wakali kama dubu mwitu aliyepokonywa watoto wake. Zaidi ya hayo, baba yako ni mpiganaji jasiri, usiku hatalala pamoja na vikosi.
And again Chusai said: Thou knowest thy father, and the men that are with him, that they are very valiant, and bitter in their mind, as a bear raging in the wood when her whelps are taken away: and thy father is a warrior, and will not lodge with the people.
9 Hata sasa, amefichwa ndani ya pango au mahali pengine. Kama atatangulia kushambulia vikosi vyako, yeyote asikiaye habari hii atasema, ‘Kuna machinjo makubwa miongoni mwa vikosi vinavyomfuata Absalomu.’
Perhaps he now lieth hid in pits, or in some other place where he list: and when any one shall fall at the first, every one that heareth it shall say: There is a slaughter among the people that followed Absalom.
10 Basi hata yule askari hodari kuliko wengine wote, ambaye moyo wake ni kama wa simba, atayeyuka kwa hofu, kwa maana Israeli yote wanajua kwamba baba yako ni mpiganaji na kwamba wale walio pamoja naye ni watu hodari.
And the most valiant man whose heart is as the heart of a lion, shall melt for fear: for all the people of Israel know thy father to be a valiant man, and that all who are with him are valiant.
11 “Kwa hiyo nakushauri: Israeli wote na wakusanyikie kwako, kuanzia Dani hadi Beer-Sheba, katika wingi wao jinsi walivyo kama mchanga wa ufuoni mwa bahari, wewe mwenyewe ukiwaongoza vitani.
But this seemeth to me to be good counsel: Let all Israel be gathered to thee, from Dan to Bersabee, as the sand of the sea which cannot be numbered: and thou shalt be in the midst of them.
12 Ndipo tutakapomshambulia popote atakapoonekana, nasi tutamwangukia kama umande unavyoshuka juu ya ardhi. Yeye mwenyewe wala watu wake hakuna atakayeachwa hai.
And we shall come upon him in what place soever he shall be found: and we shall cover him, as the dew falleth upon the ground, and we shall not leave of the men that are with him, not so much as one.
13 Kama atakimbilia katika mji wowote, basi Israeli wote watazungushia mji ule kamba, nasi tutauburuta mji huo mpaka bondeni hadi isionekane hata changarawe ya huo mji.”
And if he shall enter into any city, all Israel shall cast ropes round about that city, and we will draw it into the river, so that there shall not be found so much as one small stone thereof.
14 Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai, Mwariki, ni jema zaidi kuliko lile la Ahithofeli.” Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kupinga shauri nzuri la Ahithofeli, ili kuleta maafa juu ya Absalomu.
And Absalom, and all the men of Israel said: The counsel of Chusai the Arachite is better than the counsel of Achitophel: and by the will of the Lord the profitable counsel of Achitophel was defeated, that the Lord might bring evil upon Absalom.
15 Hushai akawaambia makuhani Sadoki na Abiathari, “Ahithofeli amemshauri Absalomu na wazee wa Israeli kufanya kadha wa kadha, lakini mimi nimewashauri wao kufanya kadha wa kadha.
And Chusai said to Sadoc and Abiathar the priests: Thus and thus did Achitophel counsel Absalom, and the ancients of Israel: and thus and thus did I counsel them.
16 Sasa tumeni ujumbe haraka na kumwambia Daudi, ‘Usiku huu usilale kwenye vivuko katika jangwa; vuka bila kukosa, la sivyo, mfalme pamoja na watu wote waliofuatana naye watamezwa.’”
Now therefore send quickly, and tell David, saying: Tarry not this night in the plains of the wilderness, but without delay pass over: lest the king be swallowed up, and all the people that is with him.
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwa wakingoja huko En-Rogeli, naye mtumishi mmoja wa kike akawa anakwenda kuwapasha habari nao wakawa wanakwenda kumwambia Mfalme Daudi, kwa maana wasingetaka kujihatarisha kuonekana wakiingia mjini.
And Jonathan and Achimaas stayed by the fountain Rogel: and there went a maid and told them: and they went forward, to carry the message to king David, for they might not be seen, nor enter into the city.
18 Lakini kijana mmoja mwanaume akawaona, naye akamwambia Absalomu. Basi wote wawili wakaondoka haraka, wakaenda mpaka kwenye nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu. Mtu huyo alikuwa na kisima katika ua wa nyumba yake, nao Yonathani na Ahimaasi wakateremka ndani ya kisima hicho.
But a certain boy saw them, and told Absalom: but they making haste went into the house of a certain man in Bahurim, who had a well in his court, and they went down into it.
19 Mkewe akachukua kifuniko, akakiweka kwenye mdomo wa kile kisima na kuanika nafaka juu yake. Hakuna mtu yeyote aliyefahamu chochote kuhusu jambo hilo.
And a woman took, and spread a covering over the mouth of the well, as it were to dry sodden barley: and so the thing was not known.
20 Watu wa Absalomu walipofika kwa huyo mwanamke, wakamuuliza, “Wako wapi Ahimaasi na Yonathani?” Huyo mwanamke akawajibu, “Walivuka kijito.” Watu wa Absalomu wakapekua lakini hawakuwaona hata mmoja, hivyo wakarudi Yerusalemu.
And when Absalom’s servants were come into the house, they said to the woman: Where is Achimaas and Jonathan? and the woman answered them: They passed on in haste, after they had tasted a little water. But they that sought them, when they found them not, returned into Jerusalem.
21 Baada ya watu hao kuondoka, wale watu wawili yaani Yonathani na Ahimaasi wakapanda kutoka mle kisimani na kwenda kumpasha Mfalme Daudi habari. Wakamwambia, “Ondoka, uvuke haya maji haraka. Ahithofeli ameshauri kadha wa kadha dhidi yako.”
And when they were gone, they came up out of the well, and going on told king David, and said: Arise, and pass quickly over the river: for this manner of counsel has Achitophel given against you.
22 Kwa hiyo Daudi na watu wote aliokuwa nao waliondoka na kuvuka Yordani. Kufika wakati wa mapambazuko, hapakuwa na mtu hata mmoja ambaye alikuwa hajavuka Mto Yordani.
So David arose, and all the people that were with him, and they passed over the Jordan, until it grew light, and not one of them was left that was not gone over the river.
23 Ahithofeli alipoona kwamba shauri lake halikufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka kwenda nyumbani kwake kwenye mji wake. Akaiweka nyumba yake katika utaratibu, kisha akajinyonga mwenyewe. Hivyo akafa na akazikwa katika kaburi la baba yake.
But Achitophel seeing that his counsel was not followed, saddled his ass, and arose and went home to his house and to his city, and putting his house in order, hanged himself, and was buried in the sepulchre of his father.
24 Daudi akaenda Mahanaimu, naye Absalomu akavuka Yordani pamoja na watu wote wa Israeli.
But David came to the camp, and Absalom passed over the Jordan, be and all the men of Israel with him.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Amasa alikuwa mwana wa mtu mmoja aliyeitwa Yetheri, Mwisraeli, ambaye alikuwa amemwoa Abigaili binti Nahashi, dada yake Seruya mamaye Yoabu.
Now Absalom appointed Amasa in Joab’s stead over the army: and Amasa was the son of a man who was called Jethra of Jezrael, who went in to Abigail the daughter of Naas, the sister of Sarvia who was the mother of Joab.
26 Waisraeli na Absalomu wakapiga kambi huko nchi ya Gileadi.
And Israel camped with Absalom in the land of Galaad.
27 Daudi alipofika Mahanaimu, Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni, Makiri mwana wa Amieli kutoka Lo-Debari, na Barzilai Mgileadi kutoka Rogelimu
And when David was come to the camp, Sobi the son of Naas of Rabbath of the children of Ammon, and Machir the son of Ammihel of Lodabar, and Berzellai the Galaadite of Rogelim,
28 wakaleta matandiko ya kitandani, mabakuli na vyombo vya mfinyanzi. Walileta pia ngano na shayiri, unga na bisi, maharagwe na kunde,
Brought him beds, and tapestry, and earthen vessels, and wheat, and barley, and meal, and parched corn, and beans, and lentils, and fried pulse,
29 asali na maziwa yaliyoganda, kondoo na jibini kutoka kwenye maziwa ya ngʼombe kwa ajili ya Daudi na watu wake ili wale. Kwa maana walisema, “Watu wameona njaa, tena wamechoka na wamepata kiu huko jangwani.”
And honey, and butter, and sheep, and fat calves, and they gave to David and the people that were with him, to eat: for they suspected that the people were faint with hunger and thirst in the wilderness.

< 2 Samweli 17 >