< 2 Samweli 15 >

1 Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
Après cela, Absalom s'équipa de chars et de chevaux, et il avait cinquante hommes qui couraient devant lui.
2 Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
Et Absalom se levait de bon matin, et se tenait au bord du chemin de la porte. Et s'il se présentait un homme ayant quelque affaire pour laquelle il venait en justice devant le roi, Absalom l'appelait et lui disait: De quelle ville es-tu? Et s'il répondait: Ton serviteur est de l'une des tribus d'Israël,
3 Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
Absalom lui disait: Vois, ta cause est bonne et droite; mais tu n'as personne pour t'écouter de la part du roi.
4 Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
Et Absalom disait: Que ne m'établit-on juge dans le pays! Tout homme qui aurait un procès ou une affaire à juger viendrait vers moi, et je lui ferais justice.
5 Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
Et si quelqu'un s'approchait pour se prosterner devant lui, il lui tendait la main, et le prenait et le baisait.
6 Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
Absalom faisait ainsi à tous ceux d'Israël qui venaient vers le roi pour avoir justice; et Absalom gagnait le cœur des hommes d'Israël.
7 Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
Et il arriva, au bout de quarante ans, qu'Absalom dit au roi: Je te prie, que j'aille à Hébron pour acquitter le vœu que j'ai fait à l'Éternel.
8 Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
Car, quand ton serviteur demeurait à Gueshur en Syrie, il fit un vœu, disant: Si l'Éternel me ramène à Jérusalem, je servirai l'Éternel.
9 Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
Et le roi lui répondit: Va en paix! Il se leva donc, et s'en alla à Hébron.
10 Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
Or Absalom envoya des espions dans toutes les tribus d'Israël, pour dire: Quand vous entendrez le son de la trompette, dites: Absalom est proclamé roi à Hébron!
11 Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
Et avec Absalom s'en allèrent deux cents hommes de Jérusalem, qu'il avait invités; or ils y allaient en toute simplicité, ne sachant rien.
12 Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
Et Absalom, pendant qu'il offrait les sacrifices, envoya appeler Achithophel, le Guilonite, conseiller de David, de sa ville de Guilo; et il se forma une puissante conjuration; et le peuple allait en augmentant auprès d'Absalom.
13 Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
Alors il vint vers David un messager, qui lui dit: Le cœur des hommes d'Israël se tourne vers Absalom.
14 Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
Et David dit à tous ses serviteurs qui étaient avec lui à Jérusalem: Levez-vous et fuyons, car nous ne saurions échapper à Absalom. Hâtez-vous de partir, de peur qu'il ne se hâte, qu'il ne nous atteigne, qu'il ne précipite le mal sur nous, et ne fasse passer la ville au fil de l'épée.
15 Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
Et les serviteurs du roi répondirent au roi: Tes serviteurs sont prêts à faire tout ce que le roi, notre seigneur, trouvera bon.
16 Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
Le roi sortit donc, et toute sa maison le suivait; mais le roi laissa dix femmes, de ses concubines, pour garder la maison.
17 Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
Ainsi le roi sortit, et tout le peuple à sa suite; et ils s'arrêtèrent à Beth-Merchak.
18 Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
Et tous ses serviteurs marchaient à côté de lui, et tous les Kéréthiens, tous les Péléthiens, et tous les Guitthiens, au nombre de six cents hommes venus de Gath à sa suite, marchaient devant le roi.
19 Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
Mais le roi dit à Itthaï, le Guitthien: Pourquoi viendrais-tu aussi avec nous? Retourne-t'en, et demeure avec le roi, car tu es étranger, et tu dois même retourner en ton lieu.
20 Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
Tu es arrivé hier, et te ferai-je aujourd'hui errer çà et là avec nous? Quant à moi, je vais où je puis; retourne-t'en, et emmène tes frères avec toi. Que la miséricorde et la vérité t'accompagnent!
21 Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
Mais Itthaï répondit au roi, en disant: L'Éternel est vivant, et le roi, mon seigneur, vit! au lieu où sera le roi mon seigneur, soit pour mourir, soit pour vivre, ton serviteur y sera aussi.
22 Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
Alors David dit à Itthaï: Viens et marche. Et Itthaï, le Guitthien, marcha, avec tous ses gens, et tous les petits enfants qui étaient avec lui.
23 Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
Or tout le pays pleurait à grands cris; et tout le peuple passait. Et le roi passa le torrent du Cédron, et tout le peuple passa vis-à-vis du chemin qui mène au désert.
24 Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
Tsadok était aussi là, et avec lui tous les Lévites qui portaient l'arche de l'alliance de Dieu; et ils posèrent là l'arche de Dieu; et Abiathar montait, pendant que tout le peuple achevait de sortir de la ville.
25 Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
Mais le roi dit à Tsadok: Reporte l'arche de Dieu dans la ville. Si je trouve grâce devant l'Éternel, il me ramènera, et il me fera voir l'arche et sa demeure.
26 Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
Que s'il dit ainsi: Je ne prends point de plaisir en toi; me voici, qu'il fasse de moi ce qui lui semblera bon.
27 Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
Le roi dit encore à Tsadok, le sacrificateur: Vois-tu? Retourne en paix à la ville, ainsi qu'Achimaats, ton fils, et Jonathan, fils d'Abiathar, vos deux fils, avec vous.
28 Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
Voyez, je vais attendre dans les plaines du désert, jusqu'à ce qu'on vienne m'apporter des nouvelles de votre part.
29 Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
Tsadok et Abiathar reportèrent donc l'arche de Dieu à Jérusalem, et ils y demeurèrent.
30 Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
Et David montait par la montée des Oliviers, et en montant il pleurait; il avait la tête couverte, et marchait nu-pieds. Tout le peuple aussi qui était avec lui montait, chacun ayant la tête couverte; et en montant ils pleuraient.
31 Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
Alors on fit ce rapport à David, et on lui dit: Achithophel est parmi les conjurés avec Absalom. Et David dit: Je te prie, ô Éternel, déjoue le conseil d'Achithophel!
32 Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
Et lorsque David fut venu jusqu'au sommet, où il se prosterna devant Dieu, voici, Cushaï l'Arkite, vint à sa rencontre, ayant sa tunique déchirée et de la terre sur sa tête.
33 Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
Et David lui dit: Si tu passes plus avant avec moi, tu me seras à charge.
34 Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
Mais si tu t'en retournes à la ville, et que tu dises à Absalom: Je suis ton serviteur, ô roi! j'ai servi ton père dès longtemps, et maintenant je te servirai; alors tu déjoueras en ma faveur le conseil d'Achithophel.
35 Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
Et n'auras-tu pas là avec toi les sacrificateurs Tsadok et Abiathar? Et tout ce que tu apprendras de la maison du roi, tu le rapporteras aux sacrificateurs, Tsadok et Abiathar;
36 Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
Voici, ils ont là avec eux leurs deux fils, Achimaats, fils de Tsadok, et Jonathan, fils d'Abiathar; vous me ferez savoir par eux tout ce que vous aurez appris.
37 Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.
Ainsi Cushaï, l'ami de David, retourna dans la ville. Et Absalom vint à Jérusalem.

< 2 Samweli 15 >