< 2 Samweli 15 >
1 Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
Après cela, Absalom se procura un char et des chevaux, et cinquante hommes qui couraient devant lui.
2 Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
Absalom se levait de bonne heure, et se tenait près de l’avenue de la porte; et chaque fois qu’un homme ayant un procès se rendait vers le roi pour obtenir un jugement, Absalom l’appelait et disait: « De quelle ville es-tu? » Lorsqu’il avait répondu: « Ton serviteur est de telle tribu d’Israël, »
3 Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
Absalom lui disait: « Vois, ta cause est bonne et juste; mais personne ne t’écoutera de la part du roi. »
4 Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
Absalom ajoutait: « Qui m’établira juge dans le pays! Quiconque aurait un procès ou une affaire viendrait à moi, et je lui rendrais justice. »
5 Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
Et lorsque quelqu’un s’approchait pour se prosterner devant lui, il lui tendait la main, le prenait et le baisait.
6 Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
Absalom agissait ainsi envers tous ceux d’Israël qui se rendaient vers le roi pour demander justice; et il séduisait les cœurs des gens d’Israël.
7 Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
Au bout de quatre ans, Absalom dit au roi: « Permets, je te prie, que j’aille à Hébron pour m’acquitter du vœu que j’ai fait à Yahweh.
8 Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
Car pendant que je demeurais à Gessur en Aram, ton serviteur a fait un vœu, en disant: “Si Yahweh me ramène à Jérusalem, je servirai Yahweh.” »
9 Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
Le roi lui dit: « Va en paix! » Il se leva et partit pour Hébron.
10 Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
Absalom envoya des émissaires dans toutes les tribus d’Israël, pour dire: « Dès que vous entendrez le son de la trompette, vous direz: Absalom règne à Hébron! »
11 Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
Avec Absalom partirent deux cents hommes de Jérusalem: c’étaient des invités qui allaient en toute simplicité, sans se douter de rien.
12 Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
Pendant qu’Absalom offrait les sacrifices, il envoya chercher à sa ville de Gilo Achitophel le Gilonite, conseiller de David. La conjuration devint puissante, car le peuple était de plus en plus nombreux autour d’Absalom.
13 Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
On vint en informer David, en disant: « Le cœur des hommes d’Israël s’est mis à la suite d’Absalom. »
14 Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
Et David dit à tous ses serviteurs qui étaient avec lui à Jérusalem: « Levez-vous, fuyons, car il n’y a pas moyen pour nous d’échapper devant Absalom. Hâtez-vous de partir, de peur que, se hâtant, il ne nous surprenne, qu’il ne fasse tomber sur nous le malheur et qu’il ne frappe la ville du tranchant de l’épée. »
15 Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
Les serviteurs du roi lui dirent: « Quelque parti que prenne mon seigneur le roi, voici tes serviteurs. »
16 Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
Le roi partit, avec toute sa famille, à pied, et il laissa dix concubines pour garder la maison.
17 Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
Le roi sortit avec tout le peuple à pied, et ils s’arrêtèrent à la dernière maison.
18 Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
Tous ses serviteurs marchaient à ses côtés, tous les Céréthiens et tous les Phéléthiens; et tous les Géthéens, au nombre de six cents hommes, qui étaient venus de Geth sur ses pas, marchaient devant le roi.
19 Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
Le roi dit à Ethaï le Géthéen: « Pourquoi viendrais-tu, toi aussi, avec nous? Retourne et reste avec le roi, car tu es un étranger et même tu es un exilé sans domicile.
20 Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
Tu es arrivé d’hier, et aujourd’hui je te ferais errer avec nous, alors que moi-même je m’en vais je ne sais où! Retourne et emmène tes frères avec toi; sur toi soient la grâce et la fidélité de Yahweh! »
21 Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
Ethaï répondit au roi et dit: « Yahweh est vivant et mon seigneur le roi est vivant! A l’endroit où sera mon seigneur le roi, soit pour mourir soit pour vivre, là sera ton serviteur. »
22 Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
David dit à Ethaï: « Va, passe! » Et Ethaï le Géthéen passa avec tous ses hommes et tous les enfants qui étaient avec lui.
23 Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
Toute la contrée pleurait et poussait des cris au passage de tout ce peuple. Le roi ayant passé le torrent de Cédron, tout le peuple passa vis-à-vis du chemin du désert.
24 Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
Et voici que Sadoc, et avec lui tous les lévites qui portaient l’arche de l’alliance de Dieu, déposèrent l’arche de Dieu, tandis qu’Abiathar montait, jusqu’à ce que tout le peuple eut achevé de sortir de la ville.
25 Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
Alors le roi dit à Sadoc: « Reporte l’arche de Dieu dans la ville. Si je trouve grâce aux yeux de Yahweh, il me ramènera et me fera voir l’arche et sa demeure.
26 Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
Mais s’il dit: Je n’ai pas de plaisir en toi, — me voici: qu’il me traite comme il lui semblera bon. »
27 Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
Le roi dit encore au prêtre Sadoc: « O toi, voyant, retourne en paix dans la ville, avec Achimaas, ton fils, et Jonathas, fils d’Abiathar: vos deux fils avec vous.
28 Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
Voyez! Moi j’attendrai dans les plaines du désert, jusqu’à ce qu’il m’arrive un mot de vous qui me renseigne. »
29 Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
Sadoc et Abiathar reportèrent donc l’arche de Dieu à Jérusalem, et ils y restèrent.
30 Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
David gravissait la colline des Oliviers; il montait en pleurant, la tête voilée, et il marchait nu-pieds; et tout le peuple qui était avec lui avait aussi la tête couverte, et ils montaient en pleurant.
31 Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
On apporta à David cette nouvelle: « Achitophel est avec Absalom parmi les conjurés. » Et David dit: « Yahweh réduisez à néant, je vous prie, les conseils d’Achitophel. »
32 Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
Lorsque David fut arrivé au sommet, là où l’on adore Dieu, voici que Chusaï l’Arachite vint au-devant de lui, la tunique déchirée et de la terre sur la tête.
33 Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
David lui dit: « Si tu passes avec moi, tu me seras à charge.
34 Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
Mais si, retournant dans la ville, tu dis à Absalom: O roi, je veux être ton serviteur; j’ai été le serviteur de ton père autrefois, je serai maintenant le tien, — tu déjoueras en ma faveur le conseil d’Achitophel.
35 Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
Tu auras là avec toi les prêtres Sadoc et Abiathar, et tout ce que tu apprendras de la maison du roi, tu le feras savoir aux prêtres Sadoc et Abiathar.
36 Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
Et comme ils ont auprès d’eux leurs deux fils, Achimaas, fils de Sadoc, et Jonathas, fils d’Abiathar, vous m’informerez par eux de tout ce que vous aurez appris. »
37 Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.
Et Chusaï, ami de David, retourna à la ville, au même temps qu’Absalom faisait son entrée à Jérusalem.