< 2 Samweli 15 >

1 Baada ya muda, Absalomu akajipatia magari ya vita na farasi pamoja na watu hamsini wa kupiga mbio mbele yake.
And it came to pass after this, that Absalom prepared for him a chariot and horses, and fifty men to run before him.
2 Akawa anaamka asubuhi na mapema na kusimama kando ya barabara inayoelekea kwenye lango la mji. Wakati wowote alipokuja mtu yeyote mwenye mashtaka yanayohitaji kuletwa mbele ya mfalme kwa maamuzi, Absalomu naye angemwita na kumuuliza, “Wewe unatoka mji upi?” Naye angejibu, “Mtumishi wako anatoka katika mojawapo ya makabila ya Israeli.”
And Absalom rose up early, and stood beside the way of the gate. And it was so, that, when any man had a suit which should come to the king for judgment, then Absalom called to him, and said, Of what city are thou? And he said, Thy servant is of one of the tribes of Israel.
3 Kisha Absalomu angemwambia, “Tazama, malalamiko yako ni ya haki na sawasawa, lakini hakuna mwakilishi wa mfalme wa kukusikiliza.”
And Absalom said to him, See, thy matters are good and right, but there is no man appointed by the king to hear thee.
4 Absalomu aliongeza, “Laiti tu ningeteuliwa kuwa mwamuzi katika nchi. Ndipo kila mmoja mwenye mashtaka au shauri angekuja kwangu nami ningeona kwamba anapata haki.”
Absalom said moreover, Oh that I were made judge in the land, that every man who has any suit or case might come to me, and I would do for him justice!
5 Pia, wakati mtu yeyote alipomkaribia ili kusujudu mbele yake, Absalomu alinyoosha mkono wake na kumshika pia kumbusu.
And it was so, that, when any man came near to do him obeisance, he put forth his hand, and took hold of him, and kissed him.
6 Absalomu akaendelea na tabia hii mbele ya Waisraeli wote waliomjia mfalme kumwomba awape haki; kwa hiyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli.
And on this manner Absalom did to all Israel who came to the king for judgment. So Absalom stole the hearts of the men of Israel.
7 Mnamo mwisho wa mwaka wa nne, Absalomu akamwambia mfalme, “Naomba unipe ruhusa niende Hebroni nikatimize nadhiri niliyomwekea Bwana.
And it came to pass at the end of forty years, that Absalom said to the king, I pray thee, let me go and pay my vow, which I have vowed to Jehovah, in Hebron.
8 Wakati mtumishi wako alipokuwa huko Geshuri katika nchi ya Aramu, niliweka nadhiri hii, ‘Ikiwa Bwana atanirudisha Yerusalemu, nitamwabudu Bwana huko Hebroni.’”
For thy servant vowed a vow while I abode at Geshur in Syria, saying, If Jehovah shall indeed bring me again to Jerusalem, then I will serve Jehovah.
9 Mfalme akamwambia, “Enenda kwa amani.” Hivyo akaenda Hebroni.
And the king said to him, Go in peace. So he arose, and went to Hebron.
10 Kisha Absalomu akatuma wajumbe kwa siri katika makabila yote ya Israeli, kusema, “Mara mtakaposikia sauti ya tarumbeta basi semeni, ‘Absalomu ni mfalme huko Hebroni.’”
But Absalom sent spies throughout all the tribes of Israel, saying, As soon as ye hear the sound of the trumpet, then ye shall say, Absalom is king in Hebron.
11 Watu mia mbili kutoka Yerusalemu walikuwa wamefuatana na Absalomu. Walikuwa wamealikwa kama wageni nao walikwenda kwa nia njema, pasipo kujua lolote.
And with Absalom went two hundred men out of Jerusalem who were invited, and went in their simplicity. And they did not know anything.
12 Wakati Absalomu alipokuwa anatoa dhabihu, pia akatuma aitwe Ahithofeli, Mgiloni, mshauri wa Daudi, aje kutoka Gilo, ambao ndio mji wake wa nyumbani. Kwa hiyo mpango wa hila ukapata nguvu, na idadi ya waliofuatana na Absalomu ikaongezeka.
And Absalom sent for Ahithophel the Gilonite, David's counselor, from his city, even from Giloh, while he was offering the sacrifices. And the conspiracy was strong, for the people increased continually with Absalom.
13 Mjumbe akaja na kumwambia Daudi, “Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana na Absalomu.”
And there came a messenger to David, saying, The hearts of the men of Israel are after Absalom.
14 Ndipo Daudi akawaambia maafisa wake wote waliokuwa pamoja naye huko Yerusalemu, “Njooni! Ni lazima tukimbie, la sivyo hakuna hata mmoja wetu atakayeokoka kutoka mkononi mwa Absalomu. Ni lazima tuondoke kwa haraka, la sivyo atakuja mbio na kutupata, atatuangamiza na kuupiga mji kwa upanga.”
And David said to all his servants who were with him at Jerusalem, Arise, and let us flee, for otherwise none of us shall escape from Absalom. Make speed to depart, lest he overtake us quickly, and bring down evil upon us, and smite the city with the edge of the sword.
15 Maafisa wa mfalme wakamjibu, “Watumishi wako tu tayari kufanya lolote mfalme bwana wetu analochagua.”
And the king's servants said to the king, Behold, thy servants are ready to do whatever my lord the king shall choose.
16 Mfalme akatoka, pamoja na watu wa nyumbani mwake wakimfuata; lakini akawaacha masuria kumi ili kuangalia jumba la kifalme.
And the king went forth, and all his household after him. And the king left ten women, who were concubines, to keep the house.
17 Hivyo mfalme akaondoka, pamoja na watu wote wakimfuata, wakatua mahali mbali kiasi.
And the king went forth, and all the people after him, and they remained in Beth-merhak.
18 Watu wake wote wakatembea, wakampita wakiwa wamefuatana na Wakerethi na Wapelethi wote; pia Wagiti wote mia sita waliokuwa wamefuatana naye kutoka Gathi wakapita mbele ya mfalme.
And all his servants passed on beside him; and all the Cherethites, and all the Pelethites, and all the Gittites, six hundred men who came after him from Gath, passed on before the king.
19 Mfalme akamwambia Itai, Mgiti, “Kwa nini ufuatane na sisi? Rudi ukakae pamoja na Mfalme Absalomu. Wewe ni mgeni, mkimbizi kutoka nchini mwako.
Then the king said to Ittai the Gittite, Why do thou also go with us? Return, and abide with the king, for thou are a foreigner, and also an exile. Return to thine own place.
20 Ulikuja jana tu. Nami leo nikufanye utangetange pamoja nasi, wakati sijui niendako? Rudi, nawe ukawachukue watu wa kwenu. Wema na uaminifu na viwe pamoja nawe.”
Whereas thou came but yesterday, should I this day make thee go up and down with us, seeing I go where I may? Return thou, and take back thy brothers. Mercy and truth be with thee.
21 Lakini Itai akamjibu mfalme, “Hakika kama Bwana aishivyo na kama mfalme bwana wangu aishivyo, popote mfalme bwana wangu atakapokuwa, ikiwa ni kuishi au kufa, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa.”
And Ittai answered the king, and said, As Jehovah lives, and as my lord the king lives, surely in what place my lord the king shall be, whether for death or for life, even there thy servant will also be.
22 Daudi akamwambia Itai, “Songa mbele, endelea.” Kwa hiyo Itai, Mgiti, akaendelea pamoja na watu wake wote, pia jamaa zote waliokuwa pamoja naye.
And David said to Ittai, Go and pass over. And Ittai the Gittite passed over, and all his men, and all the little ones that were with him.
23 Watu wote wa nje ya mji wakalia kwa sauti wakati watu wote walipokuwa wakipita. Mfalme naye akavuka Bonde la Kidroni, nao watu wote wakaelekea jangwani.
And all the country wept with a loud voice, and all the people passed over. The king himself also passed over the brook Kidron, and all the people passed over toward the way of the wilderness.
24 Sadoki pia alikuwako, kadhalika Walawi wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wamechukua Sanduku la Agano la Mungu. Wakaweka chini Sanduku la Mungu, naye Abiathari akatoa dhabihu mpaka watu wote walipokuwa wameondoka mjini.
And, lo, Zadok also came, and all the Levites with him, bearing the ark of the covenant of God. And they set down the ark of God, and Abiathar went up until all the people had finished passing out of the city.
25 Kisha mfalme akamwambia Sadoki, “Rudisha Sanduku la Mungu mjini. Ikiwa nitapata kibali mbele za Bwana, atanirudisha, nami nitaliona Sanduku hili tena pamoja na Maskani yake.
And the king said to Zadok, Carry back the ark of God into the city. If I shall find favor in the eyes of Jehovah he will bring me again, and show me both it, and his habitation.
26 Lakini kama yeye atasema, ‘Mimi sipendezwi nawe,’ basi mimi niko tayari; yeye na anifanye chochote aonacho chema kwake.”
But if he says thus, I have no delight in thee, behold, here I am. Let him do to me as seems good to him.
27 Pia mfalme alimwambia kuhani Sadoki, “Je, wewe si mwonaji? Rudi mjini kwa amani pamoja na mwanao Ahimaasi na Yonathani mwana wa Abiathari. Wewe na Abiathari wachukueni wana wenu wawili.
The king said also to Zadok the priest, Are thou not a seer? Return into the city in peace, and your two sons with you, Ahimaaz thy son, and Jonathan the son of Abiathar.
28 Nitasubiri kwenye vivuko katika jangwa mpaka neno litakapotoka kwenu kuniarifu.”
See, I will remain at the fords of the wilderness until there comes word from you to report to me.
29 Kwa hiyo Sadoki na Abiathari wakarudisha Sanduku la Mungu mpaka Yerusalemu na kukaa huko.
Therefore Zadok and Abiathar carried the ark of God again to Jerusalem, and they abode there.
30 Bali Daudi akaendelea, akapanda Mlima wa Mizeituni, akaenda huku analia, akiwa amefunika kichwa chake na bila viatu miguuni. Watu wote waliokuwa pamoja naye nao wakafunika vichwa vyao, wakawa wanapanda mlima huku wanalia.
And David went up by the ascent of the mount of Olives, and wept as he went up, and he had his head covered, and went barefoot. And all the people who were with him covered every man his head, and they went up, weeping as they went up.
31 Basi Daudi alikuwa ameambiwa, “Ahithofeli alikuwa miongoni mwa washiriki wa shauri baya la Absalomu.” Ndipo Daudi akaomba, akisema, “Ee Bwana, geuza shauri la Ahithofeli kuwa ujinga.”
And it was told David, saying, Ahithophel is among the conspirators with Absalom. And David said, O Jehovah, I pray thee, turn the counsel of Ahithophel into foolishness.
32 Daudi alipofika kwenye kilele cha mlima, mahali ambapo watu walikuwa wamezoea kumwabudu Mungu, Hushai, Mwariki, alikuwako huko kumlaki, joho lake likiwa limeraruka na mavumbi kichwani mwake.
And it came to pass, that, when David came to the top of the ascent, where God was worshiped, behold, Hushai the Archite came to meet him with his coat torn, and dirt upon his head.
33 Daudi akamwambia, “Kama ukienda pamoja nami, utakuwa mzigo kwangu.
And David said to him, If thou pass on with me, then thou will be a burden to me,
34 Lakini ikiwa utarudi mjini na kumwambia Absalomu, ‘Nitakuwa mtumishi wako, ee mfalme; nilikuwa mtumishi wa baba yako wakati uliopita, lakini sasa nitakuwa mtumishi wako,’ basi utaweza kunisaidia kwa kupinga shauri la Ahithofeli.
but if thou return to the city, and say to Absalom, I will be thy servant, O king. As I have been thy father's servant in time past, so I will now be thy servant, then thou will defeat for me the counsel of Ahithophel.
35 Je, makuhani Sadoki na Abiathari hawatakuwa pamoja nawe? Waambie lolote utakalosikia katika jumba la mfalme.
And have thou not there with thee Zadok and Abiathar the priests? Therefore it shall be, that whatever thing thou shall hear out of the king's house, thou shall tell it to Zadok and Abiathar the priests.
36 Wana wao wawili, Ahimaasi mwana wa Sadoki na Yonathani mwana wa Abiathari, wako pamoja nao huko. Watume kwangu na lolote utakalosikia.”
Behold, they have there with them their two sons, Ahimaaz, Zadok's son, and Jonathan, Abiathar's son. And by them ye shall send to me everything that ye shall hear.
37 Kwa hiyo Hushai, rafiki wa Daudi, akafika Yerusalemu wakati Absalomu alipokuwa anaingia mjini.
So Hushai, David's friend, came into the city, and Absalom came into Jerusalem.

< 2 Samweli 15 >