< 2 Samweli 14 >

1 Yoabu mwana wa Seruya akafahamu kuwa moyo wa mfalme ulikuwa na shauku ya kumwona Absalomu.
Now Joab, the son of Zeruiah, understood that the heart of the king had been turned toward Absalom,
2 Kwa hiyo Yoabu akamtuma mtu fulani kwenda Tekoa na kumleta mwanamke mwenye hekima kutoka huko. Akamwambia huyo mwanamke, “Jifanye uko katika maombolezo. Vaa nguo za kuomboleza, nawe usitumie mafuta yoyote ya uzuri, jifanye kama mwanamke ambaye amekuwa na huzuni kwa siku nyingi kwa ajili ya kufiwa.
so he sent to Tekoa, and he brought from there a wise woman. And he said to her: “Feign that you are in mourning, and put on the clothing of one who mourns. And do not anoint yourself with oil, so that you may be like a woman who is still grieving for someone who died some time ago.
3 Kisha nenda kwa mfalme ukazungumze maneno haya.” Naye Yoabu akaweka maneno kinywani mwa yule mwanamke.
And you shall enter to the king, and you shall speak words to him in this manner.” Then Joab put the words in her mouth.
4 Huyo huyo mwanamke kutoka Tekoa alipofika kwa mfalme, akaanguka kifudifudi kumpa mfalme heshima, akasema, “Ee mfalme, nisaidie!”
And so, when the woman of Tekoa had entered to the king, she fell before him on the ground, and she reverenced, and she said, “Save me, O king.”
5 Mfalme akamuuliza, “Una shida gani?” Akamwambia, “Mimi ni mjane hasa, mume wangu amekufa.
And the king said to her, “What problem do you have?” And she responded: “Alas, I am a woman who is a widow. For my husband has died.
6 Mimi mtumishi wako nilikuwa na wana wawili. Wakapigana wao kwa wao huko shambani wala huko hapakuwa na mtu hata mmoja wa kuwaamua. Mmoja akampiga mwenzake na kumuua.
And your handmaid had two sons. And they quarreled against one another in the field. And there was no one there who would be able to stop them. And one struck the other, and killed him.
7 Sasa ukoo wote umeinuka dhidi ya mtumishi wako, wakisema, ‘Utukabidhi huyo aliyemuua ndugu yake, ili tumuue kwa ajili ya uhai wa ndugu yake ambaye alimuua, nasi hapo tutakuwa tumekatilia mbali na mrithi pia.’ Wakifanya hivyo, watakuwa wamezima tumaini langu lililobaki, mume wangu hataachiwa jina wala mzao katika uso wa dunia.”
And behold, the whole family, rising up against your handmaid, said: ‘Deliver him who struck down his brother, so that we may kill him for the life of his brother, whom he killed, and so that we may do away with the heir.’ And they are seeking to extinguish my spark that is left, so that there may not survive a name for my husband, nor a remnant upon the earth.”
8 Mfalme akamwambia huyo mwanamke, “Nenda nyumbani, nami nitatoa agizo kwa ajili yako.”
And the king said to the woman, “Go to your own house, and I will make a decree on your behalf.”
9 Lakini huyo mwanamke kutoka Tekoa akamwambia, “Mfalme bwana wangu, lawama na iwe juu yangu na juu ya nyumba ya baba yangu, naye mfalme na kiti chake cha enzi na asiwe na hatia.”
And the woman of Tekoa said to the king: “May the iniquity be upon me, my lord, and upon the house of my father. But may the king and his throne be innocent.”
10 Mfalme akajibu, “Ikiwa mtu yeyote atakusemesha lolote, mlete kwangu, naye hatakusumbua tena.”
And the king said, “Whoever will contradict you, bring him to me, and he will never touch you again.”
11 Huyo mwanamke akasema, “Basi mfalme na amwombe Bwana Mungu wake ili kuzuia mlipiza kisasi cha damu kuongeza juu ya uharibifu, ili kwamba mwanangu asije akaangamizwa.” Mfalme akasema, “Hakika kama aishivyo Bwana, hakuna unywele mmoja wa kichwa cha mwanao utakaoanguka chini.”
And she said, “Let the king remember the Lord his God, so that close blood relatives may not be multiplied in order to take revenge, and so that they may by no means kill my son.” And he said, “As the Lord lives, not one hair from your son shall fall to the ground.”
12 Ndipo huyo mwanamke akasema, “Mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa mfalme bwana wangu.” Mfalme akajibu, “Sema.”
Then the woman said, “Let your handmaid speak a word to my lord the king.” And he said, “Speak.”
13 Huyo mwanamke akasema, “Mbona basi wewe umewaza jambo kama hili dhidi ya watu wa Mungu? Je, mfalme asemapo hili, hajitii hatiani mwenyewe, kwa maana mfalme hajamrudisha mwanawe aliyefukuziwa mbali?
And the woman said: “Why have you thought such a thing against the people of God, and why has the king spoken this word, so that he sins and does not lead back the one whom he rejected?
14 Kama vile maji yaliyomwagika ardhini, yasivyoweza kuzoleka tena, hivyo sisi kufa ni lazima. Lakini Mungu haondoi uhai, badala yake, yeye hufanya njia ili kwamba aliyefukuzwa asibaki akiwa amefarikishwa naye.
We are all dying, and we are all like waters that flow into the ground and do not return. God does not will to lose a soul. Instead, he renews his efforts, thinking that what has been rejected might not perish altogether.
15 “Nami sasa nimekuja kusema hili kwa bwana wangu mfalme kwa sababu watu wameniogopesha. Mtumishi wako alifikiri, ‘Nitanena na mfalme, labda mfalme atamfanyia mtumishi wake kile anachoomba.
Therefore, now I have come to speak this word to my lord the king, in the presence of the people. And your handmaid said: I will speak to the king, for perhaps there may be some way for the king to accomplish the word of his handmaid.
16 Labda mfalme atakubali kumwokoa mtumishi wake kutoka mkononi mwa mtu anayejaribu kunikatilia mbali, mimi na mwanangu, kutoka kwenye urithi Mungu aliotupatia.’
And the king listened, and he freed his handmaid from the hand of all who were willing to take away me and my son together, from the inheritance of God.
17 “Basi sasa mtumishi wako anasema, ‘Neno la bwana wangu mfalme na linipatie pumziko, kwa maana bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu katika kutambua jema na baya. Bwana Mungu wako na awe pamoja nawe.’”
Therefore, let your handmaid speak, so that the word of my lord the king may be like a sacrifice. For even like an Angel of God, so is my lord the king, so that he is moved by neither a blessing, nor a curse. Then too, the Lord your God is with you.”
18 Basi mfalme akamwambia huyo mwanamke, “Usinifiche jibu kuhusu hilo nitakalokuuliza.” Huyo mwanamke akasema, “Mfalme bwana wangu na aseme.”
And in response, the king said to the woman, “You shall not conceal from me a word of what I ask you.” And the woman said to him, “Speak, my lord the king.”
19 Mfalme akauliza, “Je, mkono wa Yoabu haupo pamoja nawe katika jambo hilo lote?” Huyo mwanamke akajibu, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu mfalme, hakuna yeyote anayeweza kugeuka kulia wala kushoto kutokana na chochote anachosema bwana wangu mfalme. Naam, ni mtumishi wako Yoabu ndiye alinifundisha kufanya hivi, naye ndiye aliweka maneno haya yote kinywani mwa mtumishi wako.
And the king said, “Is not the hand of Joab with you in all this?” And the woman answered and said: “By the welfare of your soul, my lord the king, it is neither to the left, nor to the right, in all these things that my lord the king has spoken. For your servant Joab himself instructed me, and he himself placed all these words in the mouth of your handmaid.
20 Mtumishi wako Yoabu amefanya hivi ili kubadili hali iliyopo. Bwana wangu ana hekima kama ile ya malaika wa Mungu, hufahamu kila kitu kinachotokea katika nchi.”
Thus did I turn to this figure of speech, because your servant Joab instructed it. But you, my lord the king, are wise, just as an Angel of God has wisdom, so that you understand all that is upon the earth.”
21 Mfalme akamwambia Yoabu, “Vyema sana, nitalifanya jambo hili. Nenda, ukamlete kijana Absalomu.”
And the king said to Joab: “Behold, your word has succeeded in appeasing me. Therefore, go and call back the boy Absalom.”
22 Yoabu akaanguka kifudifudi mpaka ardhini kumpa mfalme heshima, naye akambariki mfalme. Yoabu akasema, “Leo mtumishi wako anajua kuwa amepata kibali machoni pako, bwana wangu mfalme, kwa sababu mfalme amemjalia mtumishi wake ombi lake.”
And falling to the ground upon his face, Joab reverenced, and he blessed the king. And Joab said: “Today your servant has understood that I have found grace in your sight, my lord the king. For you have accomplished the word of your servant.”
23 Ndipo Yoabu akaenda hadi Geshuri akamrudisha Absalomu Yerusalemu.
Then Joab rose up, and he went away to Geshur. And he brought Absalom into Jerusalem.
24 Lakini mfalme akasema, “Lazima Absalomu aende kwenye nyumba yake mwenyewe; kamwe asiuone uso wangu.” Kwa hiyo Absalomu akaenda kwenye nyumba yake na hakuuona uso wa mfalme.
But the king said, “Let him return to his own house, but let him not see my face.” And so, Absalom returned to his own house, but he did not see the face of the king.
25 Katika Israeli yote hakuna mtu yeyote aliyesifiwa kwa uzuri wa sura kama Absalomu. Kuanzia utosi wa kichwa chake hadi wayo wa mguu wake hapakuwa na kasoro.
Now in all of Israel, there was no man so handsome, and so very stately as Absalom. From the sole of the foot to the top of the head, there was no blemish in him.
26 Kila mara aliponyoa nywele za kichwa chake, kwa kuwa alikuwa akinyoa mara kwa mara zilipokuwa zinamwia nzito, alizipima uzito wake ulikuwa shekeli mia mbili kwa kipimo cha kifalme.
And when he shaved off his hair, for he shaved it off once a year, because his long hair was burdensome to him, he weighed the hair of his head at two hundred shekels, by the public weights.
27 Walizaliwa wana watatu na binti mmoja kwa Absalomu. Jina la binti yake aliitwa Tamari, naye akawa mwanamke mzuri wa sura.
Then three sons were born to Absalom, and one daughter, of elegant form, whose name was Tamar.
28 Absalomu akaishi miaka miwili huko Yerusalemu pasipo kuuona uso wa mfalme.
And Absalom remained for two years in Jerusalem, and he did not see the face of the king.
29 Basi Absalomu akamwita Yoabu kwa kusudi la kumtuma kwa mfalme, lakini Yoabu akakataa kuja kwa Absalomu. Ndipo akamwita tena mara ya pili, lakini pia akakataa kuja.
And so, he sent to Joab, so that he might send him to the king. But he refused to come to him. And when he had sent a second time, and he had refused to come to him,
30 Ndipo akawaambia watumishi wake, “Tazama, shamba la Yoabu liko jirani na langu, naye ana shayiri humo. Nendeni mkalitie moto.” Kisha watumishi wa Absalomu wakalitia moto shamba hilo.
he said to his servants: “You know that the field of Joab, the one that is near my field, has a harvest of barley. Therefore, go and set it on fire.” And so, the servants of Absalom set fire to the grain field. And the servants of Joab, arriving with their garments torn, said, “The servants of Absalom have set fire to part of the field!”
31 Basi Yoabu akaenda nyumbani kwa Absalomu, akamwambia, “Kwa nini watumishi wako wametia moto shamba langu?”
And Joab rose up, and he went to Absalom at his house, and he said, “Why have your servants set fire to my grain field?”
32 Absalomu akamwambia Yoabu, “Tazama, nilikutumia ujumbe na kusema, ‘Njoo ili niweze kukutuma kwa mfalme kuuliza, “Kwa nini nimekuja kutoka Geshuri? Ingekuwa bora zaidi kwangu kama ningebaki huko!”’ Sasa basi, nataka kuuona uso wa mfalme, na ikiwa nina hatia ya jambo lolote, basi na aniue.”
And Absalom responded to Joab: “I sent to you, begging that you might come to me, and that I might send you to the king, and that you might say to him: ‘Why was I brought from Geshur? It would have been better for me to be there.’ I beg you, therefore, that I may see the face of the king. And if he is mindful of my iniquity, let him put me to death.”
33 Basi Yoabu akaenda kwa mfalme na kumwambia jambo hili. Kisha mfalme akamwita Absalomu, naye akaingia ndani akasujudu uso wake mpaka ardhini mbele ya mfalme. Naye mfalme akambusu Absalomu.
And so, Joab, entering to the king, reported everything to him. And Absalom was summoned. And he entered to the king, and he reverenced on the face of the earth. And the king kissed Absalom.

< 2 Samweli 14 >