< 2 Samweli 13 >
1 Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
Voici ce qui advint ensuite: Absalon, fils de David, avait une sœur extrêmement belle; elle se nommait Thamar, et Amnon, fils de David, l'aimait.
2 Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
Amnon souffrait au point de dépérir, à cause de Thamar sa sœur; car elle était vierge, et il lui semblait téméraire de rien tenter auprès d'elle.
3 Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
Amnon avait un compagnon nommé Jonadab, fils de Samaa, frère de David; or, Jonadab était un homme très rusé.
4 Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
Il dit donc à Amnon: Qu'as-tu, ô fils du roi! pour que tu t'affaiblisses ainsi de jour en jour? Ne me le confieras-tu point? Amnon lui répondit: J'aime Thamar, la sœur de mon frère Absalon.
5 Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
Jonadab lui dit: Mets-toi au lit, et fais-toi malade; ton père viendra te voir, et tu lui diras: Que Thamar, ma sœur, vienne; qu'elle me coupe mes bouchées, qu'elle prépare sous mes yeux des aliments, afin que je la voie faire, et que je mange de sa main.
6 Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
Amnon se mit au lit, et se fit malade; son père l'alla voir, et Amnon lui dit: Que Thamar, ma sœur, vienne auprès de moi; qu'elle fasse cuire devant moi deux petits gâteaux, et je mangerai de sa main.
7 Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
Et David chercha Thamar dans la maison, et il lui dit Va-t'en chez ton frère, et prépare-lui à manger.
8 Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
Et Thamar alla à la maison d'Amnon, son frère, quand il était couché. Elle prit de la pâte, la pétrit, et en fit sous ses yeux de petits gâteaux qu'elle mit cuire.
9 Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
Ensuite, elle prit la poêle, et elle la vida devant lui; mais il ne voulut pas manger, et il dit: Que l'on fasse sortir tous les hommes qui sont debout ici. Tout le monde s'en alla.
10 Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
Et Amnon dit à Thamar: Apporte-moi auprès de mon lit ma nourriture, et je mangerai de ta main; Thamar prit donc les gâteaux qu'elle avait préparés, et elle les porta à son frère Amnon vers son lit.
11 Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
Elle l'engagea à manger, et il la saisit, et il lui dit: Viens, dors avec moi, ma sœur.
12 Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
Et elle lui dit: Mon frère, ne m'avilis pas; car pareille chose ne doit pas se faire en Israël; ne fais pas cette folie.
13 Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
Comment supporterais-je mon opprobre? Et toi, tu passerais pour un insensé en Israël. Parle plutôt à mon père; il ne m'éloignera pas de toi.
14 Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
Mais Amnon ne voulut rien entendre; il fut plus fort qu'elle; il l'humilia, et il dormit avec elle.
15 Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
Et Amnon la prit soudain en grande haine, et sa haine l'emporta sur l'amour qu'il avait auparavant; car sa dernière méchanceté fut plus grande que la première. Amnon lui dit donc: Lève-toi, et va-t'en.
16 Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
Thamar lui parla au sujet de cette grande méchanceté qu'il faisait en la chassant; plus grande, dit-elle, que la première; mais Amnon ne voulut rien entendre.
17 Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
Et il appela le serviteur qui se tenait à l'entrée de l'appartement, et il lui dit: Chasse-moi d'ici cette femme, et ferme la porte sur elle.
18 Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
Elle avait un vêtement à longues manches comme en portaient les filles du roi qui étaient vierges. Et le serviteur la mit dehors, puis il ferma la porte sur elle.
19 Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
Et Thamar prit de la cendre, s'en couvrit la chevelure, déchira son vêtement à longues manches, croisa les mains sur sa tête, et s'en alla, jetant les hauts cris.
20 Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
Absalon, son frère, lui dit: Est-ce qu'Amnon, ton frère, a été avec toi? Alors, ma sœur, sois muette, car c'est ton frère. Ne prends pas à cœur d'ébruiter cette affaire. Ainsi Thamar demeura, comme une veuve, en la maison de son frère Absalon.
21 Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
Le roi David apprit tout, et il en fut violemment courroucé, mais il ne chagrina point Amnon; car il l'aimait, parce que c'était son premier-né.
22 Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
Quant à Absalon, il ne dit mot à son frère, ni en bien ni en mal; mais il le prit en haine pour avoir avili Thamar, sa sœur.
23 Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
Et ceci advint: au bout de deux années, on faisait la tonte pour Absalon en Belasor, sur le territoire d'Ephraïm, et Absalon invita tous les fils du roi.
24 Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
Absalon, d'abord, alla trouver le roi, et lui dit: Voilà que l'on fait la tonte pour ton serviteur, que le roi et tous ses fils viennent chez ton serviteur.
25 Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
Le roi répondit à Absalon: Non, mon fils, nous n'irons pas tous; nous ne voulons point t'être à charge. Absalon le pressa; mais il ne céda point, et il le bénit.
26 Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
Alois, Absalon lui dit: Si tu refuses, que du moins mon frère Amnon vienne avec nous. Le roi lui répondit: Pourquoi donc irait-il avec toi?
27 Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
Absalon le pressa, et David laissa partir avec lui Amnon et tous ses fils. Absalon leur fit un festin comme un festin de roi.
28 Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
Puis, il donna ses ordres à ses serviteurs, disant: Faites attention; quand le cœur d'Amnon se complaira dans le vin, je vous dirai: Frappez Amnon et le mettez à mort; n'ayez point de crainte; n'est-ce point moi qui vous le commande? Soyez hommes, agissez en fils de la force.
29 Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
Les serviteurs d'Absalon exécutèrent contre Amnon ce que leur avait prescrit leur maître. Et tous les fils du roi se levèrent; chacun d'eux se mit en selle sur sa mule, et ils s'enfuirent.
30 Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
Pendant qu'ils étaient encore en route, on vint dire à David: Absalon a tué tous les fils du roi, et il n'en reste pas un seul.
31 Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
A ces mots, le roi se leva; il déchira ses vêtements, et il se jeta à terre; et tous ses serviteurs qui l'entouraient déchirèrent leurs vêtements.
32 Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
Et Jonabab, fils de Samaa, frère de David, prit la parole, et il dit: Que le roi mon maître ne dise pas que tous ses serviteurs les fils du roi ont été mis à mort, car Amnon seul a péri; et c'était sur les lèvres d'Absalon depuis le jour où sa sœur Thamar a été humiliée.
33 Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
Maintenant donc, que le roi mon maître n'ait pas à cœur tout ce qu'on lui a rapporté, quand on a dit: Tous les fils du roi sont morts, car Amnon seul n'existe plus.
34 Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
Or, Absalon s'était enfui; cependant, le serviteur qui faisait sentinelle leva les yeux, et il vit une nombreuse troupe qui accourait et descendait de la montagne; il entra pour l'apprendre au roi, et il dit: J'ai vu des hommes sur le chemin d'Oronen; ils descendent la montagne.
35 Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
Et Jonabab dit au roi: Tu vois, les fils du roi sont vivants; il est advenu ce qu'avait dit ton serviteur.
36 Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
Comme il achevait de parler, les fils du roi entrèrent; ils élevèrent la voix et ils pleurèrent; le roi aussi et tous ses serviteurs se prirent à pleurer amèrement.
37 Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
Or, Absalon s'était enfui; il se réfugia chez Tholmi, fils d'Emiud, roi de Gedsur, en la terre de Chamaachad, et le roi David pleura tous les jours son fils.
38 Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
Absalon s'était donc enfui, et il s'était retiré à Gedsur, où il demeura trois ans.
39 Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.
Le roi David renonça à le faire poursuivre, parce qu'il était consolé de la mort d'Amnon.