< 2 Samweli 13 >

1 Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
Après cela, il arriva qu'Absalom, fils de David, ayant une sœur qui était belle et qui s'appelait Thamar, Amnon, fils de David, l'aima.
2 Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
Amnon se tourmentait, jusqu'à se rendre malade, au sujet de Thamar, sa sœur; car elle était vierge, et il semblait impossible à Amnon de lui rien faire.
3 Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
Amnon avait un ami, nommé Jonadab, fils de Sammaa, frère de David, et Jonadab était un homme fort avisé.
4 Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
Il lui dit: « Pourquoi es-tu ainsi défait, fils du roi, chaque matin? Ne me l'indiqueras-tu pas? » Amnon lui répondit: « J'aime Thamar, sœur de mon frère Absalom. »
5 Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
Jonadab lui dit: « Mets-toi au lit et fais le malade. Quand ton père viendra te voir, tu lui diras: Permets, je te prie, que Thamar, ma sœur, vienne me donner à manger, et qu'elle prépare le mets sous mes yeux, afin que je le voie, et je mangerai de sa main. »
6 Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
Amnon se coucha et fit le malade. Le roi vint le voir, et Amnon dit au roi: « Je te prie, que Thamar, ma sœur, vienne faire deux gâteaux sous mes yeux, et que je les mange de sa main. »
7 Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
David envoya dire à Thamar dans la maison: « Va à la maison de ton frère Amnon et prépare-lui un mets. »
8 Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
Thamar alla chez son frère Amnon, qui était couché. Prenant de la pâte, elle la pétrit, la mit en gâteaux sous ses yeux et fit cuire les gâteaux;
9 Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
elle prit ensuite la poêle et les versa devant lui. Mais il refusa de manger. Amnon dit alors: « Faites sortir d'auprès de moi tout le monde. » Lorsque tous furent sortis d'auprès de lui,
10 Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
Amnon dit à Thamar: « Apporte le mets dans l'alcôve, et que je le mange de ta main. » Thamar prit les gâteaux qu'elle avait faits, et les apporta à son frère Amnon dans l'alcôve.
11 Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
Comme elle les lui présentait à manger, il la saisit et lui dit: « Viens, couche avec moi, ma sœur. »
12 Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
Elle lui répondit: « Non, mon frère, ne me déshonore pas, car on n'agit point ainsi en Israël; ne commets pas cette infamie.
13 Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
Moi, où irais-je porter ma honte? Et toi, tu serais comme l'un des infâmes en Israël. Parles-en au roi, je te prie, et il ne refusera pas de me donner à toi. »
14 Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
Mais il ne voulut pas écouter sa voix; plus fort qu'elle, il la violenta et coucha avec elle.
15 Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
Aussitôt Amnon eut pour elle une très forte aversion, et la haine dont il la haït fut plus forte que l'amour dont il l'avait aimée; et Amnon lui dit: « Lève-toi, va-t-en! »
16 Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
Elle lui répondit: « Au mal que tu m'as fait, n'ajoute pas le mal plus grand encore de me chasser. » Mais, sans vouloir l'écouter,
17 Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
il appela le garçon qui le servait et dit: « Jetez cette femme dehors, loin de moi; et ferme la porte derrière elle. »
18 Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
Or elle avait une robe longue, car c'était le vêtement que portaient les filles du roi encore vierges. Le serviteur d'Amnon la mit dehors et ferma la porte derrière elle.
19 Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
Thamar prit de la poussière et la mit sur sa tête; elle déchira la longue robe qu'elle portait et, mettant la main sur sa tête, elle s'en alla en poussant des cris.
20 Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
Absalom, son frère, lui dit: « Ton frère Amnon a-t-il été avec toi? Maintenant, ma sœur, tais-toi, c'est ton frère; ne prends pas cette affaire à cœur. » Et Thamar demeura, désolée, dans la maison de son frère Absalom.
21 Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
Lorsque le roi David apprit toutes ces choses, il fut très irrité. ( La Vulgate ajoute: Mais il ne voulut pas contrister l'esprit d'Amnon, son fils, car il l'aimait comme étant son premier né. ) —
22 Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
Absalom n'adressait plus aucune parole, bonne ou mauvaise, à Amnon, car Absalom haïssait Amnon, à cause de l'outrage fait à Thamar, sa sœur.
23 Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
Deux ans après, Absalom avait les tondeurs à Baal-Hasor, près d'Ephraïm, et Absalom invita tous les fils du roi.
24 Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
Absalom alla trouver le roi et dit: « Voici que ton serviteur a les tondeurs; que le roi et ses domestiques viennent chez ton serviteur. »
25 Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
Et le roi dit à Absalom: « Non, mon fils, nous n'irons pas tous, de peur que nous ne te soyons à charge. » Absalom fit des instances, mais le roi ne voulut pas y aller, et il le bénit.
26 Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
Alors Absalom dit: « Si tu ne viens pas, permets du moins à Amnon, mon frère, de venir avec nous. » Le roi répondit: « Pourquoi irait-il avec toi? »
27 Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
Absalom ayant insisté, le roi laissa aller avec lui Amnon et tous les fils du roi.
28 Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
Absalom donna cet ordre à ses serviteurs: « Faites attention! Quand le cœur d'Amnon sera gavé par le vin et que je vous dirai: Frappez Amnon! vous le tuerez. Ne craignez pas; n'est-ce pas moi qui vous l'ai commandé? Soyez fermes et montrez du courage! »
29 Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
Les serviteurs d'Absalom firent à Amnon comme Absalom l'avait ordonné. Et tous les fils du roi se levant, montèrent chacun sur sa mule et s'enfuirent.
30 Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
Comme ils étaient encore en chemin, ce bruit arriva à David: « Absalom a tué tous les fils du roi, et il n'en est pas resté un seul. »
31 Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
Le roi se leva, déchira ses vêtements et se coucha par terre, et tous ses serviteurs se tenaient là, les vêtements déchirés.
32 Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
Jonadab, fils de Semmaa, frère de David, prit la parole et dit: « Que mon seigneur ne dise point qu'on a tué tous les jeunes gens, fils du roi; Amnon seul est mort. C'est une chose qui était sur les lèvres d'Absalom depuis le jour où Amnon a déshonoré Thamar, sa sœur.
33 Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
Et maintenant, que le roi mon seigneur ne s'imagine pas que tous les fils du roi sont morts; car Amnon seul est mort. »
34 Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
Et Absalom prit la fuite. Or le jeune homme placé en sentinelle leva les yeux et regarda, et voici qu'une grande troupe venait par la route occidentale, du côté de la montagne.
35 Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
Jonadab dit au roi: « Voici les fils du roi qui arrivent; les choses se sont passées comme le disait ton serviteur. »
36 Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
Comme il achevait de parler, les fils du roi arrivèrent et, élevant la voix, ils pleurèrent; le roi aussi et tous ses serviteurs versèrent des larmes abondantes.
37 Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
Mais Absalom s'enfuit et s'en alla chez Tholomaï, fils d'Ammiud, roi de Gessur. Et David faisait le deuil de son fils tous les jours.
38 Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
Absalom s'enfuit et s'en alla à Gessur, et il y fut trois ans.
39 Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.
Et le roi David renonça à poursuivre Absalom, car il s'était consolé de la mort d'Amnon.

< 2 Samweli 13 >