< 2 Samweli 13 >
1 Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
And it came to pass after this, that Amnon the son of David loved the sister of Absalom the son of David, who was very beautiful, and her name was Thamar.
2 Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
And he was exceedingly fond of her, so that he fell sick for the love of her: for as she was a virgin, he thought it hard to do any thing dishonestly with her.
3 Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
Now Amnon had a friend, named Jonadab the son of Semmaa the brother of David, a very wise man:
4 Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
And he said to him: Why dost thou grow so lean from day to day, O son of the king? why dost thou not tell me the reason of it? And Amnon said to him: I am in love with Thamar the sister of my brother Absalom.
5 Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
And Jonadab said to him: Lie down upon thy bed, and feign thyself sick: and when thy father shall come to visit thee, say to him: Let my sister Thamar, I pray thee, come to me, to give me to eat, and to make me a mess, that I may eat it at her hand.
6 Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
So Amnon lay down, and made as if he were sick: and when the king came to visit him, Amnon said to the king: I pray thee let my sister Thamar come, and make in my sight two little messes, that I may eat at her hand.
7 Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
Then David sent home to Thamar, saying: Come to the house of thy brother Amnon, and make him a mess.
8 Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
And Thamar came to the house of Amnon her brother: but he was laid down: and she took meal and tempered it: and dissolving it in his sight she made little messes.
9 Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
And taking what she had boiled, she poured it out, and set it before him, but he would not eat: and Amnon said: Put out all persons from me. And when they had put all persons out,
10 Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
Amnon said to Thamar: Bring the mess into the chamber, that I may eat at thy hand. And Thamar took the little messes which she had made, and brought them in to her brother Amnon in the chamber.
11 Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
And when she had presented him the meat, he took hold of her, and said: Come lie with me, my sister.
12 Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
She answered him: Do not so, my brother, do not force me: for no such thing must be done in Israel. Do not thou this folly.
13 Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
For I shall not be able to bear my shame, and thou shalt be as one of the fools in Israel: but rather speak to the king, and he will not deny me to thee.
14 Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
But he would not hearken to her prayers, but being stronger overpowered her and lay with her.
15 Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
Then Amnon hated her with an exceeding great hatred: so that the hatred wherewith he hated her was greater than the love with which he had loved her before, And Amnon said to her: Arise, and get thee gone.
16 Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
She answered him: This evil which now thou dost against me, in driving me away, is greater than that which thou didst before. And he would not hearken to her:
17 Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
But calling the servants that ministered to him, he said: Thrust this woman out from me: and shut the door after her.
18 Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
And she was clothed with along robe: for the king’s daughters that were virgins, used such kind of garments. Then his servant thrust her out: and shut the door after her.
19 Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
And she put ashes on her head, and rent her long robe and laid her hands upon her head, and went on crying.
20 Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
And Absalom her brother said to her: Hath thy brother Amnon lain with thee? but now, sister, hold thy peace, he is thy brother: and afflict not thy heart for this thing. So Thamar remained pining away in the house of Absalom her brother.
21 Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
And when king David heard of these things he was exceedingly grieved: and he would not afflict the spirit of his son Amnon, for he loved him, because he was his firstborn.
22 Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
But Absalom spoke not to Amnon neither good nor evil: for Absalom hated Amnon because he had ravished his sister Thamar.
23 Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
And it came to pass after two years, that the sheep of Absalom were shorn in Baalhasor, which is near Ephraim: and Absalom invited all the king’s sons:
24 Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
And he came to the king, and said to him: Behold thy servant’s sheep are shorn. Let the king, I pray, with his servants come to his servant.
25 Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
And the king said to Absalom: Nay, my son, do not ask that we should all come, and be chargeable to thee. And when he pressed him, and he would not go, he blessed him.
26 Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
And Absalom said: If thou wilt not come, at least let my brother Amnon, I beseech thee, come with us. And the king said to him: It is not necessary that he should go with thee.
27 Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
But Absalom pressed him, so that he let Amnon and all the king’s sons go with him. And Absalom made a feast as it were the feast of a king.
28 Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
And Absalom had commanded his servants, saying: Take notice when Amnon shall be drunk with wine, and when I shall say to you: Strike him, and kill him, fear not: for it is I that command you: take courage, and be valiant men.
29 Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
And the servants of Absalom did to Amnon as Absalom had commanded them. And all the king’s sons arose and got up every man upon his mule, and fled.
30 Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
And while they were yet in the way, a rumour came to David, saying: Absalom hath slain all the king’s sons, and there is not one of them left.
31 Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
Then the king rose up, and rent his garments: and fell upon the ground, and all his servants, that stood about him, rent their garments.
32 Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
But Jonadab the son of Semmaa David’s brother answering, said: Let not my lord the king think that all the king’s sons are slain: Amnon only is dead, for he was appointed by the mouth of Absalom from the day that he ravished his sister Thamar.
33 Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
Now therefore let not my lord the king take this thing into his heart, saying: All the king’s sons are slain: for Amnon only is dead.
34 Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
But Absalom fled away: and the young man that kept the watch, lifted up his eyes and looked, and behold there came much people by a by-way on the side of the mountain.
35 Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
And Jonadab said to the king: Behold the king’s sons are come: as thy servant said, so it is.
36 Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
And when he made an end of speaking, the king’s sons also appeared: and coming in they lifted up their voice, and wept: and the king also and all his servants wept very much.
37 Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
But Absalom fled, and went to Tholomai the son of Ammiud the king of Gessur. And David mourned for his son every day.
38 Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
And Absalom after he was fled, and come into Gessur, was there three years.
39 Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.
And king David ceased to pursue after Absalom, because he was comforted concerning the death of Amnon.