< 2 Samweli 13 >
1 Ikawa baada ya hayo, Amnoni mwana wa Daudi akampenda Tamari, umbu lake Absalomu mwana wa Daudi, ambaye alikuwa mzuri wa sura.
A potom se dogodi ovo: Davidov sin Abšalom imao je lijepu sestru po imenu Tamaru i u nju se zaljubio Davidov sin Amnon.
2 Amnoni akasumbuka sana kuhusu Tamari hata akaugua, kwa kuwa Tamari alikuwa bikira, na ilionekana kwamba haiwezekani Amnoni kumfanyia jambo lolote.
Amnon se toliko mučio da se gotovo razbolio radi svoje sestre Tamare: jer ona bijaše djevica, pa Amnon nije vidio mogućnosti da joj učini bilo što.
3 Basi Amnoni alikuwa na rafiki jina lake Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi. Yonadabu alikuwa mtu wa hila nyingi sana.
Ali imaše Amnon prijatelja po imenu Jonadaba, sina Davidova brata Šimeja; a Jonadab bijaše vrlo domišljat.
4 Akamuuliza Amnoni, “Wewe ni mtoto wa mfalme; kwa nini siku baada ya siku unaonekana kukonda? Hutaniambia?” Amnoni akamwambia, “Ninampenda Tamari, dada yake Absalomu ndugu yangu.”
I upita on Amnona: “Odakle to, kraljev sine, da si svako jutro mlitav? Ne bi li mi kazao?” A Amnon mu odgovori: “Zaljubljen sam u Tamaru, sestru svoga brata Abšaloma.”
5 Yonadabu akamwambia, “Nenda ukalale kitandani na ujifanye kuwa mgonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona mwambie, ‘Ningependa Tamari dada yangu aje kunipatia chochote ili nile. Tafadhali mruhusu aje na kuniandalia chakula mbele yangu ningali ninamwona, ili nipate kula kutoka mkononi mwake.’”
A Jonadab mu reče: “Lezi u postelju i pričini se bolestan, pa kad dođe tvoj otac da te pohodi, ti mu reci: 'Dopusti da dođe moja sestra Tamara da mi dade jesti; ako ona pred mojim očima zgotovi jelo da to vidim, onda ću iz njezine ruke jesti.'”
6 Kwa hiyo Amnoni akalala kitandani kujifanya mgonjwa. Mfalme alipokuja kumwona, Amnoni akamwambia, “Ningependa dada yangu Tamari aje na kuniandalia mikate maalum mbele yangu, ili nipate kula toka mkononi mwake.”
Amnon, dakle, leže i pričini se bolestan. Kad je došao kralj da ga pohodi, reče Amnon kralju: “Dopusti da dođe moja sestra Tamara da pred mojim očima zgotovi koji kolač i ja ću se okrijepiti iz njezine ruke.”
7 Daudi akampelekea Tamari ujumbe huko kwenye jumba la kifalme, kusema: “Nenda katika nyumba ya ndugu yako Amnoni ukamwandalie chakula.”
Tada David poruči Tamari u palaču: “Idi u kuću svoga brata Amnona i priredi mu jelo!”
8 Kwa hiyo Tamari akaenda nyumbani kwa nduguye Amnoni, ndugu ambaye alikuwa amelala. Tamari akachukua unga uliotiwa chachu akaukanda, akaiandaa mikate mbele yake na kuioka.
Tamara ode u kuću svoga brata Amnona. A on ležaše. Uze ona brašna, umijesi ga, načini kolače pred njegovim očima te ih ispeče.
9 Tamari akaondoa mikate kwenye kikaango ili ampatie Amnoni, lakini akakataa kula. Amnoni akamwambia, “Mtoe nje kila mtu aliyeko hapa.” Kwa hiyo kila mmoja akaondoka.
Potom uze tavu i istrese je preda nj, ali Amnon ne htjede jesti nego reče: “Otpremite sve odavde!” I svi iziđoše od njega.
10 Ndipo Amnoni akamwambia Tamari, “Leta mkate hapa ndani ya chumba changu ili nipate kula kutoka mkononi mwako.” Basi Tamari akachukua mikate aliyoiandaa na kumletea Amnoni ndugu yake ndani ya chumba chake.
Tada Amnon reče Tamari: “Donesi mi jelo u spavaonicu da se okrijepim iz tvoje ruke!” I Tamara uze kolače koje bijaše zgotovila i donese ih svome bratu Amnonu u spavaonicu.
11 Lakini alipompelekea ili ale, akamkamata kwa nguvu na kumwambia, “Njoo ulale nami, dada yangu.”
A kad mu je pružila da jede, on je uhvati rukom i reče joj: “Dođi, sestro moja, lezi sa mnom!”
12 Akamwambia, “Usifanye hivyo, ndugu yangu! Usinitende jeuri! Jambo la namna hii halistahili kufanyika katika Israeli! Usitende jambo hili ovu.
A ona mu reče: “Nemoj, brate moj! Ne sramoti me jer se tako ne radi u Izraelu. Ne čini takve sramote!
13 Kwa upande wangu je, itakuwaje? Nitaipeleka wapi aibu yangu? Pia kwa upande wako, itakuwaje? Utakuwa kama mmoja wa wapumbavu waovu katika Israeli. Tafadhali zungumza na mfalme; hatakukatalia wewe kunioa,”
Kuda bih ja sa svojom sramotom? A i ti bi bio kao bestidnik u Izraelu! Nego govori s kraljem: on me neće uskratiti tebi!”
14 Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza, na kwa kuwa alikuwa na nguvu kuliko Tamari, akamtenda jeuri.
Ali je on ne htjede poslušati, nego je svlada i leže s njom.
15 Kisha Amnoni akamchukia Tamari, kwa machukio makuu sana. Kwa kweli, Amnoni alimchukia kuliko alivyokuwa amempenda. Amnoni akamwambia, “Inuka na utoke nje!”
Nato je odmah zamrzi silnom mržnjom te je mržnja kojom ju je zamrzio bila veća od ljubavi kojom ju je prije ljubio. I reče joj Amnon: “Ustani! Odlazi!”
16 Tamari akamwambia, “Hapana! Kunifukuza itakuwa vibaya zaidi kuliko yale uliyonitendea.” Lakini Amnoni akakataa kumsikiliza.
A ona mu odvrati: “Ne, brate moj! Ako me sad otjeraš, bit će to veće zlo od onoga koje si mi učinio!” Ali je on ne htjede slušati,
17 Akamwita mtumishi wake mahsusi na kumwambia, “Mtoe huyu mwanamke hapa na ufunge mlango nyuma yake.”
nego dozva momka koji ga je služio i zapovjedi mu: “Otjeraj ovu od mene, izbaci je i zaključaj vrata za njom!”
18 Kwa hiyo, mtumishi wake akamtoa nje na kufunga mlango nyuma yake. Tamari alikuwa amevaa joho lililopambwa vizuri, kwa maana lilikuwa aina ya mavazi yaliyovaliwa na binti za mfalme waliokuwa mabikira.
(A ona je imala na sebi haljinu s dugim rukavima, jer su se nekoć u takve haljine oblačile kraljeve kćeri dok su bile djevojke.) Sluga je izvede van i zaključa vrata za njom.
19 Tamari akajitia majivu kichwani mwake na kurarua lile joho alilokuwa amevaa. Akaweka mkono wake kichwani, akaenda zake akilia kwa sauti.
Tada Tamara uze prašine i posu se njom po glavi, razdrije haljinu s dugim rukavima koju je imala na sebi, stavi ruku na glavu i ode vičući glasno dok je išla.
20 Absalomu nduguye akamuuliza, “Je, huyo Amnoni ndugu yako, amekutana nawe kimwili? Sasa nyamaza umbu langu, yeye ni ndugu yako. Usilitie jambo hili moyoni.” Naye Tamari akaishi nyumbani kwa Absalomu nduguye, akiwa mwanamke mwenye huzuni.
A njezin je brat Abšalom upita: “Je li možda tvoj brat Amnon bio s tobom? Ali sada, sestro moja, šuti: brat ti je! Ne uzimaj to k srcu!” Tako je Tamara ostala osamljena u kući svoga brata Abšaloma.
21 Mfalme Daudi aliposikia mambo haya yote, akakasirika sana.
Kad je kralj David čuo sve što se dogodilo, vrlo se razgnjevi, ali ne htjede žalostiti svoga sina Amnona, koga je ljubio jer mu bijaše prvorođenac.
22 Absalomu hakusema neno lolote na Amnoni, likiwa zuri au baya, kwa kuwa alimchukia Amnoni kwa sababu alikuwa amemtia aibu Tamari, dada yake.
A Abšalom ne reče Amnonu ni riječi, ni zle ni dobre, jer je Abšalom zamrzio Amnona što mu osramoti sestru Tamaru.
23 Miaka miwili baadaye, wakati wakata manyoya ya kondoo wa Absalomu walipokuwa huko Baal-Hasori karibu na mpaka wa Efraimu, alialika wana wote wa mfalme kuja huko.
A poslije dvije godine imao je Abšalom striženje ovaca u Baal Hasoru kod Efrajima; i Abšalom pozva svu kraljevu obitelj.
24 Absalomu akaenda kwa mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako ninao wakata manyoya ya kondoo waliokuja. Tafadhali, je, mfalme na maafisa wake wanaweza kuungana nami?”
Abšalom dođe kralju i reče mu: “Evo, tvoj sluga ima striženje ovaca, pa neka se kralj i njegovi dvorani udostoje doći svome sluzi.”
25 Mfalme akajibu, “La hasha, mwanangu si lazima sisi sote tuje, tutakuwa tu mzigo kwako.” Ingawa Absalomu alimsihi sana, mfalme alikataa kwenda, lakini alimbariki.
Ali kralj odgovori Abšalomu: “Ne, sine, nećemo doći svi, da ti ne budemo na teret.” Abšalom ustraja, ali kralj ne htjede ići, nego ga blagoslovi i otpusti.
26 Basi Absalomu akasema, “Kama hutakuja, tafadhali mruhusu ndugu yangu Amnoni twende pamoja naye.” Mfalme akamuuliza, “Kwa nini aende pamoja nawe?”
Ali Abšalom nastavi: “Ako ti nećeš, dopusti da bar moj brat Amnon pođe s nama.” A kralj ga upita: “Zašto da ide s tobom?”
27 Lakini Absalomu alimsihi, kwa hiyo mfalme akamtuma Amnoni pamoja na wana wengine wa mfalme waliobaki.
Ali je Abšalom i dalje navaljivao te David naposljetku pusti s njim Amnona i sve kraljeve sinove. Abšalom priredi kraljevsku gozbu
28 Absalomu aliagiza watu wake, “Sikilizeni! Wakati Amnoni atakapokuwa amekunywa mvinyo na kulewa sana nami nikiwaambia, ‘Mpigeni Amnoni,’ basi muueni. Msiogope. Je, si mimi niliyewapa amri hii? Kuweni hodari na wenye ushujaa.”
i zapovjedi svojim slugama ovako: “Pazite! Kad se Amnonu razveseli srce od vina i ja vam viknem: 'Ubijte Amnona!' tada ga pogubite! Ne bojte se, jer vam tako zapovijedam! Ohrabrite se i pokažite se junaci!”
29 Kwa hiyo watu wa Absalomu wakamtendea Amnoni kama vile Absalomu alivyokuwa amewaagiza. Ndipo wana wote wa mfalme wakainuka, wakapanda nyumbu zao, wakakimbia.
I Abšalomove sluge učiniše s Amnonom kako im zapovjedi Abšalom. Tada skočiše svi kraljevi sinovi, pojahaše svaki svoju mazgu i pobjegoše.
30 Wakati wakiwa njiani, taarifa ilimjia Daudi, kusema: “Absalomu amewaua wana wote wa mfalme; hakuna hata mmoja aliyesalia.”
Dok su oni još bili na putu, dođe ovakva vijest Davidu: “Abšalom je pobio sve kraljeve sinove, nije ostao od njih ni jedan jedini.”
31 Mfalme akasimama, akararua nguo zake, akalala chini ardhini; nao watumishi wake wote wakasimama kando yake na nguo zao zikiwa zimeraruliwa.
Kralj ustade, razdrije svoje haljine i baci se na zemlju; i svi njegovi dvorani koji stajahu oko njega razdriješe svoje haljine.
32 Lakini Yonadabu mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akasema, “Bwana wangu asifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme; ni Amnoni peke yake ndiye alikufa. Hili limekuwa kusudi la moyo wa Absalomu tangu siku ile Amnoni alipomtendea jeuri Tamari, dada yake.
Ali Jonadab, sin Davidova brata Šimeja, progovori ovako: “Neka ne govori moj gospodar da su pobili sve mladiće, kraljeve sinove, jer je poginuo samo Amnon: na Abšalomovu licu mogla se predviđati nesreća od onoga dana kad je Amnon osramotio njegovu sestru Tamaru.
33 Mfalme bwana wangu asisumbuliwe na taarifa kwamba wamewaua wana wote wa mfalme. Ni Amnoni peke yake aliyekufa.”
Zato neka sada moj gospodar i kralj ne misli u srcu da su svi kraljevi sinovi poginuli. Poginuo je samo Amnon,
34 Wakati huo, Absalomu akawa amekimbia. Basi mlinzi akaangalia, naye akaona watu wengi barabarani magharibi yake, wakishuka kutoka upande wa kilima. Mlinzi akaenda akamwambia mfalme, “Naona watu wakitokea upande wa Horonaimu, huko upande wa kilimani.”
a Abšalom je pobjegao.” A momak koji bijaše na straži podiže oči i ugleda mnoštvo naroda gdje silazi cestom od Horonajima. Stražar dođe i javi kralju: “Vidio sam ljude gdje silaze cestom od Horonajima po gorskom obronku.”
35 Yonadabu akamwambia mfalme, “Tazama, wana wa mfalme wako hapa; imekuwa kama vile mtumishi wako alivyosema.”
Tada Jonadab reče kralju: “Evo stigoše kraljevi sinovi! Dogodilo se kako je rekao tvoj sluga.”
36 Mara alipomaliza kusema, wana wa mfalme wakaingia ndani wakiomboleza kwa makelele. Pia mfalme na watumishi wake wote wakalia sana kwa uchungu.
Tek što je to izrekao, a to kraljevi sinovi uđoše i zaplakaše u sav glas; a i kralj i svi njegovi dvorani plakahu.
37 Absalomu akakimbia na kwenda kwa Talmai mwana wa Amihudi, mfalme wa Geshuri. Lakini Mfalme Daudi akaomboleza kwa ajili ya mwanawe kila siku.
Abšalom pak bijaše pobjegao i otišao k Talmaju, sinu Amihudovu, gešurskom kralju. A David tugovaše za svojim sinom bez prestanka.
38 Baada ya Absalomu kukimbia na kwenda Geshuri, akakaa huko miaka mitatu.
A pošto je Abšalom pobjegao i otišao u Gešur, ostao je ondje tri godine.
39 Roho ya Mfalme Daudi ikatamani kumwendea Absalomu, kwa maana mfalme alikuwa amefarijika kuhusu kifo cha Amnoni.
Kralj David prestao se srditi na Abšaloma jer se utješio zbog smrti Amnonove.